Nairobi hata bidhaa ni nyingi kuliko Bongo kuna vitu huwa natafuta Tanzania sipati ila Nairobi napata na pengine dar inatumia Miaka mingi badae kuvipata nitakutajia vitu nilivyowahi tafuta muda dar sikupata nikapata Nairobi
1. HiTi photo Kiosk Printer
2. 3D printer
3. Infinix na Xiami phone kabla hajaanza kuziagiza agiza china kwa njia ya mtandao Nairobi zimejaa
4. Spea za Magari mara mbili nimeagiza Nairobi dar hakuna moja ilikiwa ya Nissan Xtrail ilikuwa 2011 nyingine ya Subaru
5. Kuna DSLR camera pia niliipata Nairobi hapa ilikuwepo duka moja posta bei ilikuwa Moto.
6. Soap base aisee hii mpk leo sijawai ipata ni blah blah tu mtu anakwambia fata huku mara kule lakini Nairobi hata uki google utapata mtandaoni
7. Nairobi vitu vingi wanaweka online na info unaweza kujua kipo hata kwa ku google
Mnyonge mnyongeni Wakenya haki yao Wapeni wapo mbele yetu.