stakehigh
JF-Expert Member
- Aug 9, 2019
- 35,318
- 33,837
mwaiofhawaii anashangaa transfer za tanzania players ni billions
View: https://vt.tiktok.com/ZSQUfbsPa/
View: https://vt.tiktok.com/ZSQUfbsPa/
Dah we jamaa upo kweli?Mhhh! Kuna dalili ya upigaji hpa🤔
Na huwezi waona wakijadili, uzalendo wao huwa ni kwenye mambo ya kijinga tu. 😂😂😂Nafikiri hapa kuna matatizo makubwa ya kifedha either zimepigwa na uwanja ni wa bei poa or something. Ngoja tuwape muda tuone.
Nchi ikishafika sehemu inakopa ili ilipe mishahara, inakopa ili ilipe mikopo ujue hakuna nchi hapo, kunyaland ni failed state. 😂😂😂2. NAMNA PESA INAYOBAKI NDANI INAFANYA KAZI ZA MAENDELEO
TANZANIA: TZS Trilioni 57.6
KENYA: KSh Trilioni 3.32
Hizi pesa ndizo zitakazobaki ndani ya chi katika kulipa mishahara, kutoa posho, kulipa madeni ya ndani na kuhudumia kazi za maendeleo. Hizi pesa hazibadilishwi kwenda kwenye pesa za kigeni ni pesa. Kama ni Tsh inabaki hivyo hivyo na kama ni Ksh inabaki hivyo hivyo.
UCHAMBUZI KUHUSU TANZANIA
Madeni ya ndani - TZS Trilioni 5.3 (Hizi ndizo zinazoenda kulipa madeni ya ndani kwenye mabenki na mifuko ya jamii)
Mishahara, Posho na Miradi ya Maendeleo - TZS Trilioni 52.3 (inaingia moja kwa moja mitaani ambapo inagawanyika kulipa mishahara ya watumishi; walimu, madaktari, polisi na kugharamia miradi ya maendeleo -ujenzi wa shule, zahanati, barabara, na ununuzi wa saruji - nondo nk.
Kutokana na pesa hizi ukwasi wa mtu mmoja mmoja unakua.
UCHAMBUZI KUHUSU KENYA
Madeni ya ndani - KSh Trilioni 1.05 (Hii ni theluthi moja kamili ya fedha zote za ndani inayenda kulipa riba ya madeni kwenye mabenki makubwa ya Kenya)
Mishahara na Posho (Matumizi ya Kiofisi) - KSh Trilioni 2.27 (Fedha hizi zote zinaishia kulipa mishahara ya watendaji wa serikali kuu na kaunti pamoja na uendeshaji wa ofisi kama safari na mafuta).
Miradi ya Maendeleo - KSh 0 (Kulingana na maelezo haya, hakuna fedha ya kutosha ya ndani inayobaki kwenda kwenye miradi mipya ya maendeleo nchini Kenya baada ya kulipa madeni na mishahara)
Naomba nisiwachoshe sana na maelezo haya. Next comment nitakuja sasa kuonesha na kuelezea kwanini exchange rate ya Tanzania inapanda dhidi ya dolla huku ya kenya inapanda kidogo kidogo. Kaa makao wa kula
Teargass mwaiofhawaii IamLee nyangau mkenya nairobae nairobae Nicxie
REAL Comrade Kipepe The best 007 stakehigh Geza Ulole NairobiWalker RRONDO Magonjwa Mtambuka Traveller D Apeche alolo kennedy0000 ChoiceVariable chongchung Chill Kifaru254 Lemzy mwathadan BlietzKrieg AMARII babayao255 ndughuri msuya NDINDA concordile 101 Reborn Ktb The Icebreaker Mgagaa na Upwa game over Mpwimbe Filaria Na wengine ambao sijawa taga
Kwani Kunyaland maisha ni magumu vipi? Bila kuja Tanzania kuna vyakula wataingia kaburini hawajui harufu zake
View: https://x.com/i/status/2064753898057843075
Kunyaland poverty normalcy can't figure how everything ic cool here!
View: https://x.com/i/status/2064648670801252420
Sasa hauoni kwamba hiyo ni moja ya level ya kudumisha ustaarabu, ingekuwa Kenya hapo hata dereva angeweza uwawa ili mradi tu watu waibeMnajifanyanga waastaarabu kumbe ni authoritarianism. Yani mnamezea mate ila mnaogoba risasi maanake huko kwenu polisi kupiga raia risasi ni kitu cha kawaida. 🤣 🤣
Some things to addLeo ninataka tuongee in details kuhusu bajeti ya hizi nchi mbili TANZANIA (TZS TRILIONI 62.3) vs KENYA (KSh TRILIONI 4.82) ni ipi bajeti itabaki ndani ya nchi na kuzunguka kwa watu wake na kuongeza ukwasi na maendeleo ya mtu mmoja mmoja?
Hii ni serious discusion yenye lengo la kujua na kutoa elimu ili tunapoendelea na mjadala huu watu wajue.
1. TUANGALIE KILA NCHI KIASI GANI KINABADILISHWA KUWA DOLA AU PESA NYINGINE NA KWENDA NJE
TANZANIA(Dola Bilioni 7.1 = TZS Trilioni 18.6)
KENYA (Dola Bilioni 11.5 = KSh Trilioni 1.52)
TANZANIA
Uzalishaji ($5.4 Billion) - Kulipia manunuzi ya vifaa na mafuta toka nje ya nchi.
Deni la Nje ($1.7 Billion) - Zitatumika kwaajili ya malipo ya Deni la Taifa
Kenya
Deni la Taifa($8.5 Billion) - Zitatumika kulipia deni la Taifa
Uzalishaji ($3.0 Billion) - Kulipia manunuzi ya vifaa na mafuta toka nje ya nchi.
NB: Mpaka hapo tumeona namna ya matumizi ya pesa za kigeni zinavyotumiwa na nchi hizi mbili. Ili nisiwachoshe katika hili Comment inayofuata nitaongelea sasa pesa inayobaki ambayo haibadilishwi kwenda pesa ya kigeni inafanya nini ndani ya nchi
Teargass mwaiofhawaii IamLee nyangau mkenya nairobae nairobae Nicxie
REAL Comrade Kipepe The best 007 stakehigh Geza Ulole NairobiWalker RRONDO Magonjwa Mtambuka Traveller D Apeche alolo kennedy0000 ChoiceVariable chongchung Chill Kifaru254 Lemzy mwathadan BlietzKrieg AMARII babayao255 ndughuri msuya NDINDA concordile 101 Reborn Ktb The Icebreaker Mgagaa na Upwa game over Mpwimbe Filaria Na wengine ambao sijawa taga
also too low turns to be a deficit, a country has to take loans to fund the imports
A perfect balance is the place to be, meaning you earn exports and they match exactly whats going on inside the nation
Yes if it is too expensive!Did he say the food is not available in Kenya? Shida yenu huwa kizungu.
WRONGTunaendelea.....
KWANINI EXCHANGE RATE DHIDI YA DOLA TANZANIA INAPANDA NA HUKO KENYA HAIPANDI SANA - HAYA NI MAMBO YA KISOMI.
Mienendo ya viwango vya kubadilishia fedha kati ya nchi hizi mbili dhidi ya Dola inatawaliwa na kanuni za ugavi na mahitaji (Supply and Demand). Hii ni kanuni ya Uchumi watu wengi wanaijua.
TANZANIA;
Kiwango cha ubadilishaji cha Tanzania kinapanda siku hadi siku (kuhitaji Shilingi nyingi zaidi kununua Dola moja) kwa sababu kuna mahitaji makubwa sana ya Dola sokoni.
Serikali and wakandarasi wanatafuta Dola kila siku kwa ajili ya kuagiza vifaa vya ujenzi wa SGR na gridi ya taifa. Hata hivyo, kushuka huku kwa Shilingi ni kwa kimkakati na kwa utaratibu (Orderly Depreciation) kwa sababu Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ina akiba kubwa ya Dola (zaidi ya $5.3 Billion) inayotumika kutuliza soko pale linapozidiwa.
KENYA
Kiwango cha ubadilishaji cha Kenya kimesimama au hakipandi kila siku si kwa sababu uchumi wao una nguvu ya uzalishaji, bali ni kutokana na mbinu za ulinzi za dharura (Defensive Mechanics).
IMF na Benki ya Dunia:- Kenya imepokea mikopo mikubwa ya mabilioni ya Dola hivi karibuni kwenda kuinusuru isifilisike. Dola hizi zimeingizwa kwenye Benki Kuu (CBK) na zinatumiwa kwa nguvu kusukuma soko ili shillingi isishuke.
Riba Kubwa za Ndani:- CBK imepandisha viwango vya riba vya mikopo hadi juu sana ili kuzuia wafanyabiashara wa ndani kukopa Shilingi na kununua Dola. Hii imesimamisha uagizaji wa bidhaa nje, hivyo mahitaji ya Dola yameshuka kwa nguvu (Artificial Stability).
NB: Kwenye uchumi Kanuni ya Supply and Demand inasema kuwa bei hupanda pale mahitaji yanapokuwa makubwa kuliko ugavi, na bei hushuka pale ugavi unapokuwa mkubwa kuliko mahitaji. Kwa kifupi, bei ya bidhaa huamuliwa na uwiano kati ya kile watu wanachotaka kununua na kile kinachopatikana sokoni.
Nitaendelea next comment kueleza kuhusu local purchasing power kutokana na pesa hizi zinazobaki kwa wananchi na tuone ni wananchi wa nchi ipi wenye maisha bora na kwanini. Usicheze mbali ninakuja...
Teargass mwaiofhawaii IamLee nyangau mkenya nairobae nairobae Nicxie
REAL Comrade Kipepe The best 007 stakehigh Geza Ulole NairobiWalker RRONDO Magonjwa Mtambuka Traveller D Apeche alolo kennedy0000 ChoiceVariable chongchung Chill Kifaru254 Lemzy mwathadan BlietzKrieg AMARII babayao255 ndughuri msuya NDINDA concordile 101 Reborn Ktb The Icebreaker Mgagaa na Upwa game over Mpwimbe Filaria