mwaiofhawaii Teargass nairobae
Mfumo wa Tanzania unaenda mpaka kwenye street level.
Ngoja niwafundishe na muelewe real devolution maana nyie wakenya mlirukia tu treni.
Tanzania siasa zinaanza kwenye grassroots.
Mwenyekiti wa Mtaa
Huyu anachaguliwa katika mtaa au kijiji husika. Kila chama cha siasa kinaweka mgombea wake.
Baada ya hapo inaundwa serikali ya kijiji au mtaa. Ndani ya kijiji hicho kunakuwa na wajumbe nao wanachaguliwa kwa kupiwa kura.
Kijiji au mtaa kinakuwa na kamati mbalimbali yaani kama wizara.
Katika kijiji hicho kunakuwa na mtumishi wa serikali anayeitwa Executive (VEO kwa kijiji na MEO kwa mtaa)
Kitu hiki hakipo huko kenya.
Juu ya kijiji utakutana na Kata.
Kila kata Inakuwa na kiongozi anayeitwa Diwani. Vilevile huyu hupigiwa kura na kata yote. Kila Chama cha Siasa kinaweka mgombea wake. Hapo kwenye kata kunakuwa na kamati mbalimbali. Yaani diwani anaundwa Serikali ya Kata. Kwenye kata kunakuwa na mwakilishi wa Serikali anayeitwa WEO.
Kata zote ndani ya halmashauri moja zinaungana na kutengeneza council.
Madiwani wanachagua diwani mmoja atakayekuwa mwenyekiti wao (Kwenye Municipal and City anaitwa Mayor) Kwenye council ambazo hazijafikia level ya municipal anaitwa mwenyekiti wa council. Huyo mwenyekiti aliyechaguliwa na madiwani ni sawa na gavana kwenu kenya.
Ndani ya council kunakuwa na mkurugenzi anaitwa DED. Yeye anakuwa Katibu wa Council.
Sasa mpaka hapo mmejifunza nini wakenya kuhusu devolution ya Tanzania?
NB: Kijiji kinakuwa na own source of revenue kwa maendeleo ya kijiji.
Kinakusanya pesa kupitia ulinzi shirikishi, sungusungu nk.