UDART ndio Kampuni inayotoa huduma Morogoro Road mwekezaji wake ni UDA ndio maana ya jina UDART. Inasemekana Simon Group iliyonunua UDA ndani yake kuna Mstaafu maana Simon Group ilikuwa ni kampuni ndogo inayojishughulisha na kuuza mazao ya kilimo kama Ufuta etc lakini ghafla ikapewa UDA na hatimaye UDART. Na wakati huo serikali ilikataa mapendekezo ya WB kuhusu private investor wa kutoka nje mwenye uzoefu wa kuendesha BRT ili wajifunze kutoka kwake lakini hili likapingwa sana Bungeni kipindi hiko Pinda alikuwa PM akalivalia njuga kisawasawa katika kukataa ushauri wa WB. Mwishowe walishindwa kwenye mifumo ya ticket wakapigwa hela nyingi sana na pia mfumo wa kutoa taarifa kwenye vituo kujua basi litafika baada ya muda gani haukuwekwa ikaendeshwa kienyeji bila uzoefu madhara yake ndio tunaona leo kampuni ikijifia na hata yale mabasi machache waliyokuwa nayo yalipigwa kiberiti. UDART haiwezi ku recorver tena na tender ya hiyo route ameshapewa kampuni nyingine kutoka nje itaanza kazi January mabasi yatakapofika.