Hakuna sehemu nimewahi kumsifia JK and I will never. Magufuli alikuwa kipenzi cha wengi ikiwemo mimi. But life goes on, tunaachilia na kusonga mbele.
Masuala ya udini naomba tusiyaingize hapa yanaleta hisia kali na kuchochea visasi.
Mimi ni yuleyule sijawahi kubadilika but, nilisoma kitabu kimoja na kukielewa vizuri "The Art of War", nakuomba ukitafute.
Kuna watu waliokuwa upande wetu walitusaliti na wakashindwa kuwajibika wakaendekeza tamaa zao na madaraka. Ujinga na lack of exposure ikawafanya wakashindwa kumlinda jiwe.
So unataka mimi nifanye nini katika situation hiyo. Kuna watu kabisa walikuwa na wajibu wa kulinda maslah mapana ya Taifa letu lakini wakaendekeza utoto.
Mambo haya hayaitaji emotion bali intelligence. People like Polepole walikuwa na nafasi kubwa sana ya ku solve vitu kwa akili. But waliendekeza ubnafsi, u Mungu mtu bila kuwa na plan zinazoeleweka.
Kuna siku moja nilihudhuria kikao kimoja Mwenyekiti wa Kikao alikuwa Polepole, alikuwa anaongea yeye tu haruhusu watu waongee. Mpaka kikao kinaisha hakuna cha maana tulijadili baadae watu wanachukua posho na kuondoka.
Hakuna aliye mwema, Iwe kikwete, Polepole, Gwajima, Tundu Lisu, Mnyika, Mbowe au Slaa wote hao wanapambania maslah yao.
Mimi angalau kidogo ninaweza kuwa upande wa Samia baada ya Magufuli. She is trying, Nchi aliichukua katika mazingira magumu sana. Makundi ya akina Makamba, Lowasa, Rostam, JK na kundi jipya la Sukuma gang yalianza kupambana na kumuweka yeye mtu kati ili achague upande.
Aliyaweka makundi yote kwenye baraza la mawaziri, baadae akaanza kuchomoa mmoja mmoja na mwisho kabisa asilimia kubwa ya baraza lake la mawaziri lilikuwa na watu wa JPM.
Sasa hata hili kaka hulioni. Mimi nikachagua kuwa upande wa Samia badala ya JK na kundi lake.