I mean hii miradi ilishaanzishwa sasahivi inaendelezwa, hivi vinapaswa viendelee huku miradi mipya inazidi kuongezwa, si kila siku tunaambiwa uchumi wetu unakua kwa kasi
Just imagine uanzilishi wa Megaprojects kama
1. Mradi wa SGR
2. Mwalimu Nyerere HEP Project
3. Ujenzi wa mji wa kiserikali Dodoma
4. Ujenzi wa Flyovers Tanzania
5. BRT
6. Madaraja makubwa Dar na Mwanza
Hizi zilikuwa project chache lakini ni kubwa sana ukifananisha na project za sasahivi na zilianzishwa ndani ya awamu ya 5 pekee lakini uanzilishi wa project hizi ulikuwa unaenda sambamba na project nyingine za kati mfano bus stations kubwa kila kona ya Tanzania, ujenzi wa modern hospital kubwa ya Mloganzila, hospitali mbili mbili kila wilaya, usambazaji umeme kwa kasi vijijini, maeneo mengi yalijengeka kipindi hiki, mtandao mkubwa wa lami, upanuzi wa Airport ya Mwl Nyerere, shule za kutosha. Yani kipindi hicho hadi ofisini watu walikuwa wanapiga kazi kuhofia kutumbuliwa. Rushwa ilipungua sana. Na kumbuka Magufuli hakutuwekea tozo za ajabu ajabu, na bado tukaingia uchumi wa kati
Sasa hii awamu ya 6 si tunaambiwa uchymi wetu ni mkubwa zaidi na unakua kwa kasi, pia kipindi hiki cha tozo, na ukizingatia tunakopa sana kwa hiyo hela zipo nyingi zaidi kipindi hiki. Niwe tu mkweli nilitarajia tuwe na even more projects kushinda enzi za Magufuli kwa sababu sasahivi hela ipo ya kutosha. Lakini karibia kila mradi sikuhizi naona ni hiihii ya level ya kati ambayo hata enzi za Magufuli ilikuwepo tena mingi zaidi. Ila zile strong hakuna