Hayo ni mawazo yako. Baki hivyo hivyo. unawazidi watu wote wa security Tanzania uelewa. Yaani mpaka watu kwenye bunge la ulaya wanapiga kelele ili kuweka shinikizo, bado huelewi.
Sijui kama mambo mazito utayajua.
Lisu hana power. But nyuma ya pazia kuna guvu yenye lengo la kuiangusha TZ kutoka Ubelgiji.
SIoni kama ni busara kujadili mambo haya kwenye huu uzi.
Watu wa nje kupiga kelele wala siyo jambo geni.
Tanzania ilikuwa mpaka inagawa PASSPORT za kusafiria kwa wanaharakati wa nje, wanaopingana na nchi zao.
Nenda Mazimbu hapo Morogoro, ukaone waanaharakati wa nje walipokuwa wanapewa mafunzo ya kuoigana na nchi zao.
Leo wafanzania mnaandamana kuhusu Israel anavyoua watoto palestine, kwani hizo nchi zinawahusu?
Kuna mambo ya ahusu UTU tu na ubinadamu, na huwa hayana mipaka.
Na wauaji wengi nchi hii hawafanyi hiyo kazi bure, wanalipwa.
Mojawapo ya watu wanaotoa pesa ni hao umoja wa ulaya.
TZ ilisusa kufanya biashara na alikuwa haitambui serikali ya Makaburu wa Afrika Kusini.
TZ tulifukuza balozi wa Israel.
Balozi wa Morocco.
Sasa kama wao Ulaya wanaona wanatoa pesa kwa serikali zisizo na utu, kwanini wasijadili?
Wanaweza kujadili, waone kama watasitisha au watavunja mahusiano kwasababu hawataki pesa zao zitumike muwaga damu za watu.