Marcelly
JF-Expert Member
- May 23, 2020
- 3,156
- 9,577
Hebu rudia kusoma vizuri ujumbe ama mimi ndiyo sijaelewa au ni wewe amesema siasa za Tanzania sio saizi siasa za Tanzania nadhani huwa unakurupuka kama ngiri
Sema nini Siasa za Tanzania zinakwamisha mambo mengi sana.
Tungeacha professionalism iongoze sekta nyeti zote nchi hii kama infrastructures tungekuwa mbali sana...
Tulipata maendeleo sana kipindi cha Magu kwa sababu ni mtu aliyekuwa anawaza mbali na alikuwa ana exposure kubwa sana ya jinsi Tanzania inatakiwa iwe. Hata waliomzunguka wakina Mfugale, kijazi etc wote ni watu ambao Tungekuwa nao Miaka 10 wakenya wangekuwa wanakuja kushangaa mambo mengi sana hapa Tanzania kama ambavyo hawachoki kuja kutry SGR tu.
Siasa ndo zinafanya baadhi ya mambo muhimu kama infrastructures zifanyike kijuakali. Kama sasa hiv wanakimbiza kimbiza vitu ili 2025 wachaguliwe tena
Siasa ndo zinafanya Bodaboda na bajaji ziruhusiwe kupiga route za mjini...zamani waliondoa vipanya kisa vinabana mji ..sasa wameruhusu tena vibajaji
Nitawashangaa sana wakiijenga Mandela road kuwa 6 lanes tena wakati ni moja ya Barabara muhimu sana kwa uchumi wa nchi hii. Mimi binafsi sitawasamehe kama wakifanya makosa kwa Barabara hii.
Kungekuwa na watu wenye kuwaza mbali kule Kibaha...wangeongeza hata km 30 kufika Mlandizi iwe 6 lanes. Kwa miaka hii mitatu toka 2021 wana uwezo wa kufanyw hivyo tena kwa pesa za ndani
Kwanza sijabisha hiyo hoja yake nilichokataa nimkusema kwamba eti saizi siasa zinaharibu na blaa blaa zingine za kijinga.
Nimemaliza Kwa kusema kama Kuna uhitaji itafanyika hivyo maana wanaofanya hayo ni wataalamu na wapo na sio Rais.
Wewe ndio umekurupuka bila kuelewa maelezo yangu.
Tunajenga hoja Kwa misingi ya chuki zako.