yaan kitu kimoja wakenya kinachowaponza ni kuwa mmekariri kuwa nyinyi ni dominant sasa kitu msichojua ni kuwa karibia kila nchi inayowazunguka inazid kudevelop na kuzidi kuwanyanganya soko. kenya kwa miaka unayosema ilikuwa na advantage kwa sababu tanzania kupitia central corridor ilikuwa haijafunguka na kwa kukumbusha tu miaka ya 2007 kurudi nyuma ili kuja dar iliwalazimu watu wapitie namanga sababu kuwepo ubovu wa barabara ila kwa sasa kupitia central corridor imekuwa njia rahisi sana.
tukija kwenye exports kuja kwenu
usafirishaji mkubwa hasa mahindi na mazao kama avacado ilitoka tanzania kenya halafu nyinyi mkawa mnafanya exportation. lakini kwa sasa kuna viwanda lukuki vimefungwa kwa mfano ukienda songea kuna mohamed enterprises super feo na viwanda kadha wa kadha ambavyo vinafanya processing kwa ajili ya kupeleka moja kwa congo, rwanda mpaka sudani kwa hiyo lazima mahindi kwenu yamepunbue lakini bei haijashuka .
central corridor inaenda kuwapiga kwenye biashara ya mizigo mpaka mtashangaa
barabara ya kutoka tanga kiteto kwenda singi inajengwa hivi na bandari ya tanga tayari inafanya kazi, hivyo tegemeni mombasa kushindana na banadri tatu yaani tanga, dar es salaam na mtwara ambazo mpaka sasa zote zinafanya kazi wakati ya lamu hata foundation stone bado.
hivi rwanda atakubali kweli kuendelea kutumia mombasa wakati kutoka tanga kwenda kigali anapunguza zaid ya km 500 barabara ya tanga-kiteto -singida ikimalizika