Chamoto
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 9,856
- 22,191
Sera nyingi zilibadilishwa baada ya kufuata masharti ya restructuring ya WB na IMF, ili kupunguza gharama za kiuendeshaji. Ndiyo maana waliondoa JKT, kuacha kulisha wanafunzi mashuleni, viwanda kubinafsishwa n.k. Ukiangalia kiundani yote hiyo ilikuwa ni kutudhoofisha kiulinzi na kiuchumi.Viwanda vya Kijeshi (Nyumbu, Kiwanda cha Mizinga na risasi, ila walikiua) Uganda kabeba somo vizuri.
Naweza sema hakuna viwanda vinavyoniuma kama hivi.
1. General Tyres hadi leo kina potential ya kua revenue generator wa serikali ila hawakioni wanaona kuongeza tozo ndio kupata pesa.
2. Viwanda vya Nguo (Urafiki, Mwatex, Musoma Textile) dah yaani hakuna mwendeleo sisi wa kuexport mafamba hivyo?.
3. Viwanda vya Baisikeli ya Swala (NABISCO) Naamini sasa bajaji isingekua tabu.
4. Kiwanda cha chuma (chenye kuunda kila aina ya pembejeo au chuma) mashine aliuziwa Mchungaji Rwakatare like Seriously?
Ile sheria ya sovereignty ni moja ya vitu vya kujivunia sana kama taifa. Kitendo cha awamu hii kutaka kuiondoa inaonekana wazi kuna watu wa nje wanaoshikilia remote ya viongozi wetu.Ikiwa kipindi cha Sakata la Dp World walitaka sheria ya Magufuli ya Permanent Sovereignty on Natural resources ibadilishwe itakuaje hivyo. Maana walishindwa kupitisha.
Hiyo sheria ya 2017 ina ipa Nchi Permanent Sovereignty, inamaanisha mkataba wa milele hauwezekani, na ikiwa muwekezaji haifaidishi nchi inaweza kuvunjwa akarudi kwao, na kushtaki ni kushitakia hapa hapa sio nje.
Sheria kama hiyo unaenda ibadili ili iweje?