Si huwa mnasema Tanzania hamna ubaguzi. Nini hii tena.😂😂
Ubaguzi wa Wapi, kisa stadium. Mbona kila mkoa una fail share ya Miradi, iwe masoko, barabara, bandari, meli za majini, Madaraja, Ulinzi, Usafiri, Viwanja vya Ndege, Hospital.
Kwanza mara nyingi miradi mikubwa inaangaliwa kua strategic.
Sasa Mwanza wana Daraja la mabilioni, Meli kubwa ya kisasa, Bandari inakarabatiwa, Stend Imewekwa ya kisasa hata kuliko Mbeya. Njia nne zipo mbioni barabara iliyobusy.
Same to Bukoba, Mara kuna hospital ya msoma, barabara zinazounganisha maeneo muhimu, TARIME-NYAMWAGA-NYAMONGO-MUGUMU.
Na sera ya Madini imefanya watu wa Nyamongo waanze kula mema baada ya Twiga Minerals kuingia na sheria ya Local Contractors.
Na Kanda ya Ziwa inachangia asilimia kubwa ya Jeshi la Nchi, Polisi, Magereza.
Ni kua tu kuna sehemu inapata mradi tofauti na ambao kwingine haupo na kule kwingine wanautaka inakua kurushiana maeno.
Kesho utasikia Mbeya wanataka stend, Kwingine Daraja la kisasa, hivyo kila kukicha kunakua na improvement ya ukali wa miundombinu. Ilikua Stand ya Morogoro inawika, kejeli zikaanza stand ya Dar mbona hamna, Dar Ikatandikwa kitu we unaona, Mwanza haoo,nao wakapewa kitu kikali.unaona, Dodoma hao wamepewa.
Now Arusha wanadai wameachwa wamepewa uwanja, the cycle continue uzuri. Kila sehemu haitaki unyonge.
Ila Nchi kubwa hii Miradi ya kimkakati kwanza. Hata umeme ulilalamikiwa sana kua mijini wanabagua kuliko vijijini REA hii hapa, now kelele imechange Vijijini umeme bei nafuu mjini ghali.