Mimi nilipenda kuelimishwa faida za uchumi wa kununua bidhaa za wengine bila kuzalisha sisi wenyewe.
Tuchukulie biashara ya mitumba, ilipoanza kipindi kile cha Mwinyi, wachuuzi wengi walifaidika sana (ajira). Kadhalika wafanyabiashara wa maduka ya jumla na reja reja pamoja na watu wachache wanaowazunguka walinufaika (ajira). Kwa upande mwingine, zao la pamba lilikufa kibudu.
Wakati wa Mwalimu watu walivaa nguo za pamba za kushona. Hapa kulikuwa na ajira kubwa sana ya mafundi cherehani (nchi nzima), hasa kipindi cha siku kuu. Kulikuwa na maduka mengi ya kuuza vitambaa (ajira), vilivyotengenezwa kwenye viwanda vya Tanzania kama Urafiki (ajira). Viwanda hivi vilinunua pamba kutoka kwa wakulima wa Tanzania (ajira), wakulima hawa walinunua pembejeo kutoka viwanda vya Tanzania kama ZZK (ajira). Ukiangalia mlolongo huo utaona wanaonufaika walikuwa wengi sana.
Sasa naomba kuelimishwa faida za uchumi wa uchuuzi kwa taifa ni zipi?