Inashangaza kudhani leo Ukraine ghafla wamekuwa wema kutaka kusaidia waafrika chakula wakati vita ilipoanza waliwazuia wanafunzi wa kiafrika kupanda treni ili kukimbia vita.
Lengo kuu la vita hii (physical and economic) lilikuwa ni kudhoofisha uchumi wa Urusi ili iwe banana republic. Ambapo ingekuwa rahisi Ulaya kuigawa Urusi na kujichukulia rasilimali watakavyo (kama Libya). Hii ni ndoto yao toka zamani. Napoleon pamoja na Hitler walijaribu pia walijaribu kuivamia Urusi lakini walishindwa.
Urusi kupata soko inazuia uchumi wake kutetereka na hivyo kuzuia lengo la Ulaya kuitenga duniani na kuidhoofisha.
Ulaya wameshashindwa hiyo vita. Ukraine inaendelea kumegwa zaidi. Urusi itachukua Odessa, mpaka Transnistria. Na Poland itakuja kuichukua Lyviv, ambayo zamani ilikuwa sehemu ya yake.
Sababu ya vita ni kuisambaratisha Urusi, ili waweze kuitawala dunia. Ukishaitawala Urusi, China haitakuwa na jeuri kiuchumi kwasababu madini yote na nishati za aina zote ziko zilizojaa Siberia zitakuwa chini yao.