Of course sio Swala geni duniani, lakini ni swala geni kwetu na pia hujaniambia umuhimu wake ni upi.
Moja ya malengo ya Nyerere kuhamisha capital somewhere else ni kujenga national identity ambayo haihusiani na colonial rule. Dar es Salaam ilikuwa capital ya wakoloni, Kwa hiyo Nyerere akaamua kuhamisha makao makuu ya nchi kwenda Dodoma kujenga identity ya taifa, hasa inayohusisha ujamaa.
Wakoloni waliigawa Dar es Salaam Mara tu walipoanza utawala. Msasani peninsula (Oyster Bay na Masaki) ilikuwa ni ya Europeans halafu Kariakoo ya waafrika weusi. Downtown ilijazwa na wahindi na waarabu. Na mpaka leo hizi demographics zinaonekana.
Dodoma ni mji mkuu wa serikali. Huo mji mwingine unaotengenezwa ni mji gani? Kwanini capital isiwe abstract? Ukiweka taasisi zote za serikali kwenye district ndogo unafanya zoning. Kwanza uta-weaken Dodoma Maana watu wengi watajaribu kusogea karibu na huo “mji wa serikali.” Pili unatengeneza class divide. Clearly watumishi pia watapata makazi kwenye hayo hayo maeneo ya “mji wa serikali” halafu wananchi wa “kawaida” wataendelea kuishi Dodoma. Pia social services zitakuwa directed mainly kwenye “mji wa serikali.” Hakuna sehemu yoyote Dodoma iliyopangiwa sophisticated infrastructure kama huo “mji wa serikali.” Paved roads, a planned tram system, underground electric cables, sewerage systems, street lighting etc
Kama taasisi zingechanganyikana kwenye maeneo yote ya mji wa Dodoma basi maendeleo yangeonekana mahali pote. Usisifie system inayotumika nchi nyingine bila kufahamu ni jinsi gani itakavyoathiri jamii yako!