@Chamoto hivi kweli wewe ni msomi?. Hakuna popote pale ambako imethibitika kisayansi kwamba vyakula vya GMO vina matatizo, Kama upo na "reputable and approved research results" zinazothibitisha tafadhali tuwekee tuone.
Tatizo ni kwamba Kuna baadhi ya watu katika nchi mbalimbali Kama wewe ambao walionyesha wasiwasi duniani na kuzikataa kwa kutumia maneno ya mitaani, na kwasababu ni hiari kwa watu kutumia au kutotumia, ndio wakawa wanaweka "label" kwa wanaopenda.
Mkuu, hapa Tanzania ni Sheria kwa wanaouza Nyama ya nguruwe "pigs" kuweka maandishi kuonyesha kwamba hiyo Nyama ni nguruwe katika Hotel, butcher, au Supermarket, hiyo Haina maana kwamba Nyama hiyo ni hatari, japo hao wasiokula "pigs" kwa Imani zao wanasema kwamba Nyama ya nguruwe ipo na madhara kiafya bila hata kutoa ushahidi wa kisayansi, wewe unaliamini Hilo?.
Sayansi imethibitisha kuwepo na madhara katika sigara na tahadhari imewekwa katika kila pakiti ya sigara, mbona bado tunalima na kuvuta sigara, vivyo hivyo katika pombe?
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app