JICA ni partners wazuri sana kwenye mambo ya upanuzi wa bandari na kuchora masterplan na kufadhili ujenzi wa bandari. Wao ndio wafadhili wakuu wa Mombasa port. Mna bahati mmepata hawa wafadhili katika port ya Kigoma. Hizi port zenu za Mwanza na Kigoma zinastahili kupanuliwa kabisa kwa sababu bado ni ndogo sana. Pia mnastahili kujenga meli nyingi kubwa kubwa kwenye ziwa Victoria na Tanganyika. Mimi najua mnajenga meli kubwa moja pekee katika ziwa Victoria.
Mnastahili kujenga meli kama tano kubwa ndani ya ziwa Victoria na nne kubwa ndani ya ziwa Tanganyika. Kisha muwashinikize majirani wenu pia wapanuwe port zao. Hio itafanya biashara yenu na DRC na nchi zingine kudouble au kutriple. Potential mnayo kubwa lakini kwa maoni yangu sioni kama mnainvest ya kutosha kwenye upanuzi wa mabandari na ujenzi wa meli kubwa katika haya maziwa mawili. Japo tangu wakati wa Magufuli angalau mumeanza kuivest kwenye inland ports na meli, nadhani kabla ya Magufuli marais wa awali walikuwa wametelekeza ujenzi wa hizi inland ports. Ni maoni yangu tu.