Mkuu, nchi hizi ambazo zinaongozwa kwa misingi ya Katiba, yaani viongozi kupigiwa kura na wananchi, Moja ya matatizo yake ni hayo, kwamba mamlaka na maamuzi ya mwisho ni wananchi walio wengi, sio wasomi wenye akili nyingi, Wala serikali.
Kazi kubwa ya kiongozi Bora, ni kuwaunganisha wananchi wote, wajinga na wasomi ili waende kwa pamoja. Kiongozi jukumu lake ni kuwaelimisha wajinga ili wamuelewe, sio watu wote wana upeo ulio sawa sawa ktkt kuelewa Mambo, Sasa hao wajinga haina maana kwamba wanamchukia.
Kiongozi ambaye hawezi kuwashawishi wananchi ili waweze kuelewa kile anachowafanyia, atakimbilia kusema watu wananichukia, mwisho wake ataigawa nchi kwa misingi ya udini, jinsia, mikoa, uchama, au kabila.
Muhimu kwa wale wanaomuelewa (wanaompenda), lazima wajitahidi kuwaelimisha na kuwashawishi wale wasiomuelewa(wasiopenda), ili wamuelewe(wampende) waweze nao kumuunga mkono.
Mwisho wa siku walio wengi ndio wasikilizwe na wawe na maamuzi ya mwisho, bila kujali Kama ni wajinga au wenye akili, ndivyo Katiba inavyotaka, kinyume na hapo atakuwa amepoteza uhalali wa kuongonza nchi kwa misingi ya Katiba iliyomuweka madarakani, hatufai.
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app