Wakenya 99 kati ya 100 wangependa kuzaliwa Tz au kama c hivyo wakawe mbwa ulaya kuliko kuzaliwa Kenya na ndiyo maana wako ladhi hata kudandia ndege kuondoka nchini kwao.
View attachment 2213147View attachment 2213148View attachment 2213149
Mimi huwa najivunia sana kuzaliwa Tanzania naona Mungu alitupendelea sana Watanzania nchi yetu ni nzuri mno, maisha yetu ni mazuri mno sijawahi kuregret hata siku moja eti niondoke nikaishi maisha ya nchi nyingine, na sidhani kama itatokea.
Yaani unaenda shambani unachuma parachichi, embe, chungwa, pilipilli za kila aina,ndizi mbivu na mbichi, samaki wa kila aina ukiwa karibu na mto au ziwa unaloa kwa ndoano.
Mvua ikinyesha unatumia maji ya mvua msimu mzima mmoja hadi mwingine mpaka wenye maji yao ya bomba wanakuuliza vipi mbona bili yako haisomi umeharibu miundombinu?
Ukija kwenye mboga mboga sasa ndio usiseme. Yaani hivi vitu vyote viko ndani ya shamba moja tu.
Ukija ufugaji una kuku wa mayai, kuku wa nyama, mbuzi na ng'ombe wa maziwa katika shamba moja tu.
Msimu wa mahindi na maharage unafanya kutupia tu yanajiotea yenyewe maana Mungu katubarikia mvua nyingi na udongo wenye rutuba na hatuna watu wenye njaa eti watatuibia mazao yetu shambani Kama wenzetu wanaotembea na makaratasi eti wamesoma kutushinda huku wafa kwa njaa maajabu.
Siku mkisikia Tanzania kuna watu wamekufa kwa njaa mjue Kenya nusu yake iko taabani. Hatuwezi kwasababu sisi hatuna uchoyo wa vyakula asilimia kubwa tunalima kwahiyo tutatoa msaada hata kabla serikali haijafika.
Wakenya hatuwacheki kwa njaa zenu tunawaombea ukame uishe kinachotokea ni kwamba mnajifanya mnajua sana mko juu yetu kwa maisha mazuri kuliko sisi sasa tunaamua kuwaumbua.
Nchi nzuri kama hii nawezaje kuikimbia, nifuate nini huko nje, ukitaka ardhi unanunua sehemu yoyote ile ya Tanzania na maisha yanaendelea na unaowakuta hapo ndg zako. Hatuna ukabila bwana kama nyinyi mnachinjana kwa kisa kidogo tu.
Wakenya kuweni wawazi kujua kiingereza siyo kigezo cha maisha mazuri na elimu yenu siyo nzuri kiivyo mna vilaza wengi hata huko serikalini na hata hampigi kelele mnadanganywa na mnakubali.
Mbona sisi watoto wetu wanasoma medium schools na wanaongea kiingereza kizuri tu kuwashindeni nyinyi mbona hawasemi wna akili nyingi na wako juu yetu?
Tanzania ni nchi nzuri, watanzania wana upendo na watu wote hatuwachukii ila mkimwaga mboga hakika ugali tunautia mchanga.
USIKU MWEMA GUYS.