Wachina waliamua kuendelea kama Nchi, Africa tuliamua kutopiga hatua Hadi kuendelezwa huwa nawashangaa sana Waafrika wanaotaka kujifananisha na Watu Wamagharibi....
Miji yote ya Magharibi tayari ilikuwepo tangu miaka 1800s ila China, Korea, Japan walikuwa ni hermit Kingdoms au kwa maana nyingine walikuwa wako nyuma na hakutaka kuwa kama wageni wa Kimagharibi.
Japan ndio ikawa ya Kwanza katika kipindi kinaitwa Meiji Restoration mwishoni mwa Karne ya 19 na mwanzo mwa Karne ya 20 walitumia muda mfupi sana kupata maendeleo ambayo Ulaya walitumia Karne nyingi.
Wakaja China (Qin Dynasty) Na Joseon (Korea) Hawa wote walisumbuliwa na Japan kidogo ila Baada ya vita ya pili ya Dunia wakaanza kujiamulia Nchi zao zitaendelea....
Just imagine haya mataifa yaliathiriwa sana na vita za ndani na hata Ile ya Dunia lakini leo hii hawapangini Nini cha Kufanya na Watu wa Magharibi na tena wanaheshimiwa sana.
Kuna mtazamo mbaya sana na Taifa la North Korea ni maskini, Umaskini unaosemwa wa North Korea unatokana na Kutopewa fursa sawa ya kushindana na kuishi kama Kila mtu.
North Korea inaweza Kurusha Satellite yake yenyewe iliyotengenezwa na Watu wake wa ndani, ila ukija Afrika hakuna nchi Africa kuanzia Misri Hadi South Africa anayeweza kwa sasa. North Korea inawataalam wa Nuclear ambao wanatengeneza hadi mabomu, ila Africa Nzima hatuna....
Africa lazima tujue Nini tunataka na tunavipataje.
NOTE: Uhuru wa kuwatukana viongozi sio maendeleo