Lengo lako unataka tuwe na space program ili tutatue tatizo gani ambalo ni kipaumbele kwasasa hapa Tanzania?, Mkuu kupanga ni kuchagua, hizi nchi zetu ni masikini Sana na uwezo wetu ni mdogo Sana wa kufanya Mambo mengi kwa pamoja, "space program" kwa nchi ambazo hata maji ya kunywa hayajawafikia wananchi wote, bado hakuna madawa ya kutosha, wananchi hawana chakula, bado barabara nyingi ni vumbi hazipitiki kipindi cha mvua, ni serikali isiyojitambua ndio itakimbilia kuwekeza katika space programs.