Umesoma hii article Kweli? Maana inaongelea sababu za wangi wa Mimba za utotoni huko Meru, Kenya.
Na kama elimu ni haki ya kila mtoto hapa Tanzania, Kwa nini watoto waliopata ujauzuto wisipate hiyo haki? Denying them access to attend school violates their constitutional right to education!
Hili swala si la kukurupuka kusema kuwa hao watoto wasiende shule si la busara. Unaposema watoto hawa waliopata ujauzito wasirudi shule ni Sawa na kuwaondolea fursa kujiendeleza kimaisha. Wakifukuzwa shule watoto hawa it is highly likely wanaangukia kwenye Kuolewa, wanakubwa na Ugumu wa maisha, wanakuwa discriminated na jamii, ambayo huwapelekea kuwa prone to mental health issues na depression, na bila kusahau kiujumla wanaingia kwenye Wimbi la umasikini. Mtu mwenye potential ya kujiendeleza kielimu anaishia kuuza karanga huku akitafuta kwa ajili ya yeye na mtoto wake.
Inabidi tujiulize Kwa nini Afrika Ndiyo inayoongoza duniani kwa underage pregnancies! Kwasababu jamii zetu na familia kiujumla zinachangia kwa kiasi Kikubwa kwenye Hili swala. Hatuwapi watoto wetu sex education. Ni familia chache sana za kiafrika/ kitanzania unakuta wazazi wanaelimisha watoto wao kuhusu mambo ya adolescence na kujikinga! Ndio, kuna watoto wanaosikia wakiambiwa jambo lakini lazima kuwepo na wale wasiosikia na ni vyema kushauri watumie Kinga ili kunjilinda dhidi ya mimba na magonjwa ya ngono kama HIV/AIDS!
Na hii elimu isiwe Kwa wasichana tu Bali na watoto wa kiume. Unakuta Mzazi anamkanya mtoto wake wa kike halafu hamkanyi yule wa kiume. Matokeo yake? Yule wa kiume Ndio anaenda kumpa Mimba mtoto wa mzazi mwingine!
Kiufupi ni vyema kuwaelimisha watoto wetu na kama kwa bahati mbaya mtoto amepata ujauzito kuwepo na program za kuwaruhusu warudi shule. Baada ya kujifungua inabidi mtoto msichana arudi shule na shuleni kuwepo na counseling services za kuwasaidia hawa watoto Maana mara nyingi huwa nwanaathirika kisaikolojia.
Inabidi Jamii zetu zibadilike kwanza ili tuone matokeo. Kukatisha masomo ya wanafunzi au kuwafunga will NEVER break the cycle! Lakini kwa wale watoto wanaopata ujauzito kutokana na sexual assault, inatakiwa wafanyiwe counseling services na watu responsible wachukuliwe Hatua za kisheria.
Ninakaribisha maoni yenu.