Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Yani mambo yote yaliyofanywa awamu iliyopita yameonekana ni ya hovyo, kila mahali pametolewa dosari, ss hapa km hawajitii doa wao wenyewe sijui imekaaje, nadhani wanajichimbia kaburi wao wenyewe, tatizo la nchi hii hakuna upinzani imara ila kiukweli huu ndiyo ulikuwa mwisho wa hiki chama.

Chuki mbaya sana aisee.
Mzee yale maneno ya magufuli "siku moja mtanikumbuka" nmeamin Leo yani hawa jamaa wanapinga kila kitu hamna hata mmoja anayeonekana kumuunga daah bora niamie Burundi tuu huu unafki ndio siutakagi
 
NITAKUWA TOFAUTI NA MH SPIKA KUHUSU HILI LA BANDARI YA BAGAMOYO.

Na Thadei Ole Mushi.

Spika wa Bunge kaishangaa Serikali kuanzia kutengeneza Reli badala ya Kuanzia na bandari. Si mara ya kwanza Kwa Mh Ndugai kusema kuhusu ujenzi wa BANDARI hii mwaka 2019 alisema hata wachina wanatushangaa na wakatufananisha na MTU aliyetanguliza mkokoteni mbele halafu punda nyuma. Kwa maana ya kwamba kujenga Reli ni kutanguliza Mkokoteni Mbele halafu Punda nyuma.

Wachina wana hamu na ujenzi wa Bandari hiyo kuliko hata watanzania wenyewe. Je ni kweli wachina wanatupenda kiasi hicho?

Fact

Mwaka juzi China ilianza kushikilia mashirika muhimu ya Zambia baada ya Zambia kushindwa kulipa madeni inayodaiwa na China.

China ilishikilia Shirika la Utangazaji la nchi hiyo pamoja na Shirika la Umeme la Zambia (ZESCO) na bado wataendelea kutaifisha mashirika mengine kadri muda utakavyokwenda.

Huko Sri-Lanka nako wameshikilia Bandari ya nchi hiyo kwa Lengo lile lile la kulipa madeni ya China.

John Perkins kupitia kitabu chake Confession of an Economic Hit man anatufunulia jinsi sera ya Conspiracy inavyofanya kazi.

Perkins anaelezea kazi aliyokuwa akiifanya bila yeye kujua kwenye Kampuni la MAIN (Consulting and engineering Company)

Aliajiriwa kama mfanyakazi kwenye kampuni hilo ambalo ni Kampuni binafsi ila shughuli zake ziliathiriwa na mkono wa Serikali (Ujasusi) bila yeye kujua.

Kazi yake kubwa ilikuwa ni kushawishi nchi maskini zikope mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa katika nchi zao. Miradi kama vile ujenzi wa miundombinu ya Reli,Ujenzi ya Umeme ambayo utasaidiwa kukopeshwa aidha na World bank, IMF au USAID.

Perkins alikuja kugundua kuwa njia hii ya kukopesha mikopo mikubwa ambayo hailipiki ni njia mojawapo ya Taifa la Marekani kuendelea kupata maeneo ya kunyonya katika nchi maskini.

Perkins anatoa mifano jinsi alivyofanikisha kuingiza Indonesia kwenye Mtego huo na nchi nyingine nyingi.

Kwa nchi ambazo zinaendelea na zenye rasilimali kama Gesi, Madini na mafuta Marekani huwa hawalali kwenye kuhakikisha inatafuta kuwakopesha.

China nayo imeaanza kunufaika na Sera hii ya conspiracy kila mahali wanajenga ushawishi mkubwa kutoa mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa. Wanajua mikopo hii hailipiki hivyo wanaweza kunufaika wao.

Bandari ya Bagamoyo ikikamilika inafunika zote Afrika Mashariki, hivyo wateja wengi watahamia Bagamoyo ambayo itakuwa inaendeshwa na mchina baada ya sisi kukosa fedha za kumlipa mchina. Najiuliza Je China inaweza kutupenda kwa kiasi hicho? Je tunaweza kumlipa mchina?
 
Kwa extent Fulani ukweli sikuujua. Na hata ukweli nilioujua sikupenda kuuongea kwasababu nilikuwa nasoma atmosphere ya huu uzi. Kabla sijachukua break kidogo kwenye huu uzi miezi michache iliyopita niliongea ukweli na wengi walinipinga. Kiukweli siwezi kubadisha mawazo ya mtu lakini muhimu ni kuwajulisha watu. Ukweli waupende wasiupende ilimradi uwepo hewani.
nitupie short summary kwa mimi mkuu nijue tatizo lako,letu lipo sehemu nina jambo nataka tufaidishane kama wa Tz
 
Eti Magufuli stand itasababisha foleni kwamba haikuzingatia ujenzi wa barabara ya kimara-kibaha

Na kwamba bwawa la JNHP linajengwa kwa hesabu za kizamani za 70s

Kwahiyo ilani yao waliyoitengeneza wenyewe leo wanaikosoa, kwahiyo mapesa yote yaliyozama pale tumeyatupa tu tuanze upya

Yani kiukweli mambo mengine hata wapinzani wanashangaa, hakuna jema lililofanywa awamu iliyopita, kesho tutaambiwa mradi wa sgr hauna tija mana tayari spika anasema ilipaswa utegemee ujenzi wa Bagamoyo port

Wallahi Africa ni shit hole.
Asad ndiye alikuwa jembe alikuwa anatoa vitu nondo vyenye mashiko
 
Hii yote ni njia za kumpinga jpm mm hawa jamaa siwaelewi tena upinzani washike nchii tuu yani ccm watu wamekaa kimaslai tuu
miaka yote hiyo ipo wazi CCM ni chama chenye wanachama wanafki kuliko chama chochote duniani,,
ukiwabana tu kimaslai wanakuchukia
 
kwa kifupi mama yupo kwenye lile genge tulilokuwa tukilisema mda wote. over..

nashukuru sijawahi kaa na kusikiliza speech zake sababu nilishajua yafuatayo ,,,niliamini kupitia vitendo si maneno,naona vitendo vishaanza kufail kupitia maneno

tuendelee kuenjoy,,,yaani msimamizi wa nchi unamuomba alinde madini wakati anajua wajibu wake kisheria ni lazima alinde,unaomba watu wafanye kazi kiuadilifu wakati wajibu wao yapaswa ni lazima wafanye hivyo

unawaomba nini wakati wanakula mishara kupitia pesa za kodi za watanzania.
 
Naona mfano wa Kenya umewakwaza wengi. Situmii maneno ya ajabu Bali nasema ukweli. Ukweli ni mgumu siku zote hasa kwa wale ambao hawautaki.
Yaa uko sahihi, hatupaswi kuifanya kenya kama yardstick. Wakati kenya is worse in corruption than us.
 
Kwa extent Fulani ukweli sikuujua. Na hata ukweli nilioujua sikupenda kuuongea kwasababu nilikuwa nasoma atmosphere ya huu uzi. Kabla sijachukua break kidogo kwenye huu uzi miezi michache iliyopita niliongea ukweli na wengi walinipinga. Kiukweli siwezi kubadisha mawazo ya mtu lakini muhimu ni kuwajulisha watu. Ukweli waupende wasiupende ilimradi uwepo hewani.

Ukweli upi unaousema?
 
kazi kweli kweli

“CAG naomba ulimi wao usiwe mzito kuongea yaliyopo kwenye reports “

 
Back
Top Bottom