Mbona mnazidi kuja Nairobi kama Nairobi ni mbaya? Karibu kila siku nakutana na Mtanzania huku. Na sio kwamba wanafanya kazi ya ofisi inayohitaji masomo. La hasha, wao wanafanya biashara ndogo ndogo. Wengi wamefungua kiosk yaani duka. Wengine wanauza nguo za mitumba, wengine ni waiters kwenye mahoteli. Kuna wengine ni omba omba huku hata kiswahili chao ni cha kitanzania. Yaani sio kwamba wanafanya kazi inayohitaji kisomo. Hata wakati MP Jaguar alisema kwamba Watanzania wafukuzwe huku maana ni wengi sana, baadhi ya wafanyibiashara wa Kenya walisupport maana mpo wengi sana huku. Halafu hawana work permit na polisi wa huku wanakula hongo tu badala ya kuwakamata kwa kukosa work permit. Hata wengine hawana passport na kama wewe ni Mtanzania lazima uwe na passport ili uingie Kenya. Huwa tunawaacha tu maana nyinyi ni jirani ila kisheria tunastahili kuwakamata hawa watu kwa kukosa vibali. Mnasema tuna roho mbaya ilhali tunawaachia mnachanganyika na Wakenya wengine na kuleta competition za kibiashara kwa Wakenya. Kuna mfanyibiashara Mtanzania mahali ambapo naishi amefungua supermarket na Wakenya wananunua bidhaa bila kumbagua. Hata mimi huwa naenda huko kununua bidhaa. Halafu ameajiri Watanzania tu. Kuna siku nilipiga gumzo naye, anasema anatokea Tanga. Sasa huko Tanga sijui ni wapi lakini hamtubagui
Cc
MK254