Kwa sababu Mungu amewabariki na rasilimali nyinyi ndio mlikuwa mnastahili kuongoza East Africa kiuchumi. Hata ni aibu sana kwenu kwamba nchi ambayo 75% ni jangwa kama Kenya inawapiga kiuchumi. Kenya hata haina minerals zozote za maana. Hata gold industry yetu ni ndogo sana kushinda yenu. Sisi tunachimba dhahabu kidogo sana kwa sababu Mungu hakutubariki na dhahabu kibao kama nyinyi. Sisi tuna kampuni za mining mbili kubwa pekee na mining industry yetu inagenerate revenue kidogo sana. Kampuni moja inachimba titanium ores na nyingine inachimba soda ash. Yaani ndio maana huwa tunawaita Malazy maana kulingana na rasilimali mliobarikiwa nayo nyinyi ndio mnastahili kuwa na Gdp kubwa. Wacha tuone kama haya makampuni yatabadilisha mambo. Lakini muwe na aibu kidogo kwamba nchi nusu size yenu, jangwa karibu yote, madini hakuna, population ndogo kushinda yenu bado inawachapa kwenye Gdp. Hio sio lazyness? Fanyeni kazi mje mtupite maana hamfai kuwa nyuma yetu ikiwa mna madini zote na mna amani. Kuweni serious hakuna kitu cha kusherehekea hapa, bali mnastahili kuwa na huzuni kwamba mumekuwa mkilala kwa miongo mingi sana. Nyinyi mnastahili kuwa mnakimbizana na SA lakini sasa mnafanya catch up na Kenya, nchi ambayo haina madini isipokuwa rasilimali ya watu. Serikali ya Kenya inategemea ubongo na nguvukazi ya watu wake ili kujipatia ushuru. Kwa sababu hatuna madini, tuna watu na hawa watu ndio wanaofanya kazi na kulipa ushuru na kujenga uchumi. Hawa watu ndio wanaoanzisha makampuni yanayojenga uchumi. Kwa sababu Kenya inategemea watu wake kama rasilimali ya nchi inabidi serikali itilie maanani masomo ili watu hao wawe na uwezo wa kuchangia vilivyo kiuchumi. Wakenya wengi Wameenda ulaya kufanya kazi na kutuma nyumbani pesa. Hii yote ni bidii ya mchwa ambayo lazima Wakenya wafanye maana hatuna madini na serikali yetu sio ya ujamaa, haitupatii vitu vya bwerere kama huko kwenu. Hapa kila mtu lazima afanye kazi maana serikali haitakupatia kitu chochote bure isipokua masomo. Jambo hilo linalazimisha kila Mkenya kufanya kazi kwa bidii. Huko kwenu shamba ni ya bwerere, afya ni ya bwerere, maji ni ya bwerere, masomo ni ya bwerere mbona usiwe lazy? Huwezi kujua kujitafutia ikiwa unapewa kila kitu bila malipo.