NDINDA
Platinum Member
- Apr 4, 2011
- 10,726
- 49,572
Dogo kajitahidi sana mimi o level nilipiga phyics C Chemistry B Biology C na mtaani nikawa mtamu sanaNikazama PCB kuhenya na msuli mzito usiopimika
Noma sana Mkuu, mimi Physics siwezi isahau ilinidhalilisha siku ya paper
. Nilikuaga siisomi kabisa na sikua na mpango nayo. Mwaka huo paper la mock nilipiga D safi, Masela wakanipamba duh, hujawahi soma hili soma na unapiga D, noma sana. Kumbe kuna swali lilikosewa tukapata marks za bure
.Basi Miezi kadhaa mbele NECTA nikaingia zangu kupiga Paper la Physics. Kwenye practical masela wakakimbilia vifaa wanavyojua wakaliacha lile la dude sijui pendulum Bob lipo wazi. Nikaaa zangu pale nikawa nachezea chezea . Basi wire ule nikaukata kipande, Baada ya muda invigilator kapita kashangaa kidogo kaniuliza wire niliokupa upo wapi? Nikamwambia Nimeukata mrefu sana


, kumbe ile kitu ilikua Constant wakuu
, Alinifokea kwenye chumba cha Mtihaani “WE FALAA NINI” kamwita Askari nikapewa wire mwingine nikaendelea kuchezea hadi kuda ukaisha.Matokea yakatoka nina mswaki kama kawa ila haijaharibu mambo yangu, Nikapiga ABB nikaenda zangu CBG , Nikasoma Miezi kadhaa ila walikuja walimu wa chuo somo moja walimu kibao
, Yaani kila mwalimu na topic yake, nikaona ni fujo nikakimbilia HGL 

. Piga zangu ABC huko NECTA A-Level , Nahisi ningebaki CBG nisengetoboa.




