Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Nilikaa na mdada wa kikenya mm nikiwa dirishani wa kiti cha pembeni pia ni mkenya mwanaume katoka kufunga mziko kampala wakaanza kuongea kilugha basi zima yule mwanaume akaniambia nyanyuka njoo ukae hapa nije kukaa na bibi yangu mtu
 
Sasa tulivyofika malaba border tukagonga vizuri tukalifata basi kwa mbele tukapanda kumbe lilikuwa limepakiza kifaa cha gari kufika mbele tukakutana na block ya police kama km 25 wakaomba kukagua bus kwenye but imebeba non dereva kagoma akasema gari imeshakaguliwa custom kwakua tulikuwa tuna haraka tuka
 
Wakati kabla hatujaenda kuongea nae kuna polisi mmoja yeye alikuwa anakagua id card bila id card au passport huingii Kenya sasa kuna mganda kiswahili hajui kingereza hawakuelewana yeye alikuwa na kama barua ndo alitumia kugongesha kwahyo akasema I'd card
 
I'd card hana akawa anashushwa ikabidi sisi tumsaidie tumwambie toa ulionyesha custom ndo akatoa polisi akaelewa na akampiga dongo mujifunze na kiswahili waganda ikawaimeisha kimbembe kwa dereva kagoma kukaguliwa anasema sio kazi yenu ikabidi tushuke maana sisi tulikuwa team ya watu wasiopungua 14 tukaenda kuongea na yule askari tukajitambulisha akatuelewa akasema dereva afungue muondoke kwa heshima yenu maana tulijuana waraabu wapemba twajuana kwa vilemba.
Bado dereva akagoma akasema kama munataka kukagua turudi customer tukarudishwa kumbe washachomeana basi tulilofatana nalo lilimuaona wakati anapaika
 
Kurudi costomer na kipande kirefu kutoka kwenye block wakaongea wakati huo kuna mkubwa wao alikuwa amekuja vile vifaa vikaonekana vina nyaraka halali wakamgeuzia kibao kwakukataa kutii agizo halali la kufungua buti tukaenda kituoni kule wanaita kumfungulia mashitaka tukajikuta mpaka saa nane ndo tunatoka pale safari ikaanza nililala nilikuja kuamka kumi na moja na baridi ndo lililoniamsha sehemu inaitwa erditol kama sikosei kuna baridi hatari nilienda kutafuta shuka la Masai kwenye begi
 
Na yule jamaa alieniamia nitoke kwenye kiti alishuka kumbe sio bibi yake wamekutana kwenye gari tu akashusha mizigo yake na akaomba namba akapewa mpaka saa tatu tukawa Nakuru ni mji fulani unataka kufanana na arusha hapo tulishuka na kuywa chai na yule dada akashuka safari ikaendelea kuna jamaa alikuwa siti jirani aliusoma ulemchezo was Jana akaniuliza ww mtz nikamwambia ndio akaanza kuniambia wakenya wa huku ndo wal
 
Walivyo wanapenda ukabila Ila tofauti na Nairobi kule mchanganyiko nikawa nimepata rafiki mpya akawa ananitajia miji .
Nikirudi nyuma kwa nakuru ni mji uliochangamka kwakweli na kuna fly over moja tuliipita ,kingine ardhi ya Kenya kwa maeneo yale inafanana sana na ardhi ya arusha na kuna sehemu kama uwanda
 
Wa jagwa na kwa njia ile niliona watu wengi kule wanafuga bata kuna mji mwingine tukakutana nao kama unakaribia Nairobi nadhani naivasha kama sijakosea tulivyokuwa tunaingia Nairobi kulikuwa na ujenzi wa barabara unaendele pamoja na madaraja tukakunja kushoto ndo tunaianza Nairobi kiukweli tulikutana na foleni kutokana na ujenzi wa barabara
 
Mpaka kwenye flyovers alafu mpangilio kelele tupo za on mpaka tunashuka saa nane hiyo na hatukushukia kwenye stand kama ubungo no gari inabaki pembeni tu ya barabara nikaongozana na mwenyeji wangu kwenda kuchange pesa nimetoa elfu kumi nimepewa 400 mwezangu katoa dola kumi kapewa 1200 tukaondoka kwenye stand ya namanga nauli 500 mpaka namanga tukachukua noha mbili tukaanza kupangua foleni nyingine tuliganda sana ambapo Julia kwetu kuna uwanja wa mpila nadhani nyayo stadium tulivyo fanikiwa tukaingia namanga kumi na moja
 
Lazima niwe mkweli pamoja na foleni Ila jamaa kwenye barabara wamejitaidi na kingine nilichokiona kutoka njia ya namanga wamejenga project za nyumba kama mladi wa avic town au iyumbu nyingi japo niliambiwa ardhi ni bei sana na dereva na arusha tulilala japo kesho yake tulivyoanza safari ya dar tukakwama korogwe daraja kujaa maji tulilala korogwe hii
 
Japo tuna sema wakenya wabaguzi lakini kwangu waganda wa Kampala sitawasahau jamaa wana dharau alafu wanapenda starehe sana tena kiswahili ndo wanajifanya hawajui kabisa tofauti na kenya sikupata shida
 
Safari hii niliifanya tarehe 21 mwezi wa 10 mwaka Jana na kwasasa nipo Kongo wakati wakurudi nilipitia mtukura to Kampala sorry kwa niliowakwaza
 
Japo najiuliza mbona foleni nikubwa sana magari mengi au mji ni mdogo kuliko idadi ya watu foleni mpaka kwenye fryover .
Kingine japo sijauzunguka mji wote lakini ukiacha foleni naamini sijajua vipimo viko vipi vya kieneo Ila Nairobi ni ndogo kuliko dar maana isingekuwa foleni tungeimaliza haraka
 
Back
Top Bottom