Mkuu mm mda mrefu nimekuwa na Idea kwa hz tm zetu hz kuhusu kujitegemea, mfano niichukilie tm yangu pendwa ya Yanga wanashindwa nn kujenga uwanja? Tm yenye rasilimali watu km Yanga? Wafanye hv

Waingie ubia na benki flani mfano crdb au nmb zen kupitia benki husika wawahimize washabiki wa Yanga wachukue kadi ya kielektroniki ya Yanga ambayo kupitia hyo kadi shabiki ataweza ku deposit au ku withdraw amount kwenda au kutoka benki.
Hizo kadi zitolewe bure ila ziwe na kianzio fulani ambacho hakitakuwa kikwazo kwa shabiki kumiliki, yn hyo kadi ipatikane ktk kila branch ya benki husika nchi nzima na washabiki wahimizwe nchi nzima kupitia vyombo vyote vya habari.
Baada ya hapo Yanga iwe ina hakiki idadi kamili ya mashabiki zen Yanga wachukue mkopo toka benki husika kwa kuanzia inaweza kuchukua hata bilioni 30 zen watafute eneo ambalo km wataomba serikalini watapewa bure, zen watangaze tenda ma engineer wajenge uwanja.
Wakati uwanja unajengwa kuwe na update za kila mara zikionesha hatua za ujenzi na hapo hapo mashabiki wahimizwe wawe wanachangia rejesho, mfano kima kiwe kuanzia elfu moja yn kila mwezi shabiki awe anachangia buku kima cha chini ili tuwe tunarejesha rejesho.
Hiyo accnt ya rejesho iwe wazi yn kiasi mtu akichangia akione live bila chenga, hv unadhani kwa mshabiki wa kweli atashindwa kuchangia tm yake wakati uwanja anauona? Na nadhani WaTz nadhani wanajulikana kwa mapenzi ya kweli pale anapoona ukweli umetawala ktk jambo fulani.
Hiyo bilioni 30 unapata uwanja mzr tu wa kuanzia ambapo baada ya kukamilika na kumaliza deni tutauongeza taratibu kulingana na mahitaji mpk tunakuwa na uwanja wa kimataifa, hilo nalo linatushinda kweli mpk tm zetu kubwa hivi zenye mvuto na credibility ya kutosha zinakosa viwanja???