Kwanza uelewe kila awamu ina mambo yake ya kutekeleza kuanzia pale ilipoishia nyingine na kuanzisha mambo mapya
1.JK alijenga mitambo ya umeme wa gas na mabomba,hakuona haja ya umeme wa maji maana kila awamu na zama zake nadhani unakumbuka uchumi/umeme wa gas ndio ulikua kauli mbiu ya awamu iliyopita sasa huyu kapiga chini
Niongeze volume ya kulinganisha hasa kwenye uchumi?
2.Kujenga jengo sio kwamba ndio soko,kwani kuna siku ulikuta madini hayauziki eti yamekosa jengo linaloitwa soko? Ko hii sio hoja bali serikali kuleta ujamaa
3.Aliyeasisi mchakato wa reli ya sgr ni Jk kupitia wachina,Magu kateka nyara na kuleta mkandarasi wake kama alivyoizima bandari ya bagamoyo
4.Barabara zote anazozindua Magu hajawahi kuzianzisha yeye kuanzia brt hadi flyovers..Jk aliunganisha mikoa ya iringa-dodoma-singida,mbeya-sumbawanga-mpanda,Kigoma-burundi,Songea-masasi-mtwara nk nk..Hadi leo hii Magu kashindwa kuunganisha kagera-kigom,mbeya-tabora/singida,tabora-kigoma nk nk kachemka
5.Elimu bure ilianzia kwa kushusha ada tangu enzi ya mkapa kwa shule ya msingi,jk akashusha ada ya o level na kujenga mashule ya kata nchi nzima hadi vyuo vikuu sio kama saizi watu wanajenga mabweni wanajipiga kifua