Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Status
Not open for further replies.
Baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA), na Baraza kuu la Answar suna Tanzania(BASUTA), kwa pamoja wamelaani kitendo cha viongozi wa CDM Kumvua hijabu DC Fatuma kimario wamesema kitendo hicho walichofanya chadema kwa mujibu wa uislam ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani kwa hiyo amewataka viongozi wa chadema kuwaomba radhi waislamu alisema Naibu mufti akiwa mjini Tabora, Fatuma ana imani yake japo ni DC, heshimuni imani yake kwani waliomchagua wanajua kuwa imani yake inamtaka avae hijab alisema sheikh mohamed issa wa Answar Sunna. taarifa ya habari Radio Imani.
Asanteni masheikh kwakuwa makini na wanaotaka kuhujumu dini yetu na alama za dini yetu

Wanaweza kukataza muadhana mkinyamazia mambo haya...
 
Baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA), na Baraza kuu la Answar suna Tanzania(BASUTA), kwa pamoja wamelaani kitendo cha viongozi wa CDM Kumvua hijabu DC Fatuma kimario wamesema kitendo hicho walichofanya chadema kwa mujibu wa uislam ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani kwa hiyo amewataka viongozi wa chadema kuwaomba radhi waislamu alisema Naibu mufti akiwa mjini Tabora, Fatuma ana imani yake japo ni DC, heshimuni imani yake kwani waliomchagua wanajua kuwa imani yake inamtaka avae hijab alisema sheikh mohamed issa wa Answar Sunna. taarifa ya habari Radio Imani.
<br />
<br />
teh teh teh.! Tutawavua hadi kufuli kama mtaficha shahada za raia..kama vipi andamaneni
 
asanteni masheikh kwakuwa makini na wanaotaka kuhujumu dini yetu na alama za dini yetu

wanaweza kukataza muadhana mkinyamazia mambo haya...
siku hizi sio adhana tu inayopigwa kwenye spikers ni swala nzima ya asubuhi. Hii imeifanya nchi kurindima kwa sauti za kuhamasisha dini kuliko hata turkey nilipokua hivi karibuni kwenye misikiti mikubwa inayoongoza duniani
 
siku hizi sio adhana tu inayopigwa kwenye spikers ni swala nzima ya asubuhi. Hii imeifanya nchi kurindima kwa sauti za kuhamasisha dini kuliko hata turkey nilipokua hivi karibuni kwenye misikiti mikubwa inayoongoza duniani

ndio uhuru wa kuabudu ambao tutaulinda kwa nguvu zote,

Siyo CDM wala CUF tutakubali itanyang'anye mkuu..ikiwemo alama zake kama hijabu, kanzu nk.
 
ndio uhuru wa kuabudu ambao tutaulinda kwa nguvu zote,

Siyo CDM wala CUF tutakubali itanyang'anye mkuu..ikiwemo alama zake kama hijabu, kanzu nk.
Mkuu samahani, hivi hapa nchini hatuna sheria ya uchavuzi wa mazingira kwa kelele? (noise pollution related law).
 
Hizo ni kukurukakara za Ccm za kuwapotosha waislam wa Tanzania kwa kutoa kauli bila ya kuelewa nini wanachokizungumza.
mara nyingi wanatakiwa wawe makini kabla awajatoa kauli. Tanzania amna matatizo ya dini bali mfumo wa watawala wetu wa
kutumia mabavu (Regime) kwa kutaka kutawala maisha na kurithishana madaraka. Kauli aliyoitoa DC ni ya upotovu na ya
kupangwa.
 
Katika majadiliano haya, yalianza na kadhia ya BAKWATA na BASUTA kutaka kuombwa radhi na CDM, lakini kadiri majadiliano yanavyoendelea, tumewawacha wahusika (BAKWATA, BASUTA kama vile hawa ni wawakilishi wa waislamu wote, na CDM kama kwamba ni chama cha wakristo). Tunakwenda wapi? Hatuoni kwa kufanya hivi tunajitenga na sifa ya kuwa Great Thinkers?

Hivi BAKWATA na BASUTA wanawawakilisha waislamu wote au ni kikundi cha wachache kujali maslahi yao?
Hivi CDM ni chama cha Kikristo au ni chama cha kuwakomboa Watanzania wote?
Hivi hakuna waislamu katika CDM? Ikiwa wamo, hawa ni sehemu ya BAKWATA na BASUTA?

Ndugu zangu, tuwacheni udini tushughulike na kujenga nchi, tuishughulikie wanaoiua Tanzania ambapo naamini si waislamu wala wakristo, bali walafi wasiojali maslahi ya Watanzania, watoke dini wanayotoka.
 
CDM ile dhana ya udini iliyokuwepo wakati wa uchaguzi sasa ndio wanaidhibitisha! Hii ni hatari. Kama DC alifanya kikao na kutaka kuchakachua,basi wangechukua hatua kama watu wazima wenye busara na si kufanya na kuzungumza waliyozungumza. Kwahili mimi nazidi kujikusanyia ushahidi wa udini na chuki dhidi ya Uislam. Kama dhana hii itaendelea! Tutaikumbuka miaka 50 ya amani,kwani tutakuwa katika hali nyingine ya chuki ya hali ya juu.Ni kweli tumeichoka CCM na mfumo uliooza! Hivyo lengo ni kung'oa mfumo wote na kuanza upya,lakini kwa dalili nizionazo si njema kwani kunamgawanyiko na kudharauliana. Lakini kumbukeni jipu huanza kipele na mbuyu ulianza kama mchicha. Tusipouziba ufa huu wa udini basi tutajenga ukuta kwa damu. Chadema tuombeni radhi Waislam kwa kitendo hicho! Kupuuzia,tutatangaza mgogoro mkubwa dhidi yenu. Kwani lengo lenu ni kuwatenga Watanzania kwa dini zao? Kuweni makini!
hatushangai sana hivi nini ilibidi kikemewe pale DC alikuwa akifanya dhambi ya kutotenda haki lakini wao haya hawaoni ni ule mtandio na hakuna ushaidi wowote kuwa ile hijabu ilivuliwa kama sasa wameona ni vema kuongoza dini kwa propaganda mwisho tutauona.............
 
Katika majadiliano haya, yalianza na kadhia ya BAKWATA na BASUTA kutaka kuombwa radhi na CDM, lakini kadiri majadiliano yanavyoendelea, tumewawacha wahusika (BAKWATA, BASUTA kama vile hawa ni wawakilishi wa waislamu wote, na CDM kama kwamba ni chama cha wakristo). Tunakwenda wapi? Hatuoni kwa kufanya hivi tunajitenga na sifa ya kuwa Great Thinkers?

Hivi BAKWATA na BASUTA wanawawakilisha waislamu wote au ni kikundi cha wachache kujali maslahi yao?
Hivi CDM ni chama cha Kikristo au ni chama cha kuwakomboa Watanzania wote?
Hivi hakuna waislamu katika CDM? Ikiwa wamo, hawa ni sehemu ya BAKWATA na BASUTA?

Ndugu zangu, tuwacheni udini tushughulike na kujenga nchi, tuishughulikie wanaoiua Tanzania ambapo naamini si waislamu wala wakristo, bali walafi wasiojali maslahi ya Watanzania, watoke dini wanayotoka.
Mkuu maswali yako yanajibiwa wazi na michango ya watu hapa JF. Walolitaka CCM hakika limetimia na sasa hivi inabidi uzoee na kukubali kwamba jumuiya ya Watanzania tayari imekwisha gawanyika. Mimi nimejaribu sana kuondoa fikra hizi lakini inaonyesha wazi kuwa haiwezekani, hivyo hao BAKWATA na BASUTA ni binadamu kama hawa hapa wanaCHADEMA ambao wanawakilisha mawazo yao ya kiutengano kupitia vyombo hivi. Soon itabidi uchague upande gani you belong!
 
Bakwata hivi hawana mambo ya kufanya mwishowe watakuja sema sambusa zipigwe marufuku (kwa kukosa la kusema)kama kudhalilishwa sio uislamu uliodhalilishwa na hiyo hijabu ni sawa na kilemba tu,acheni kulilia yu enyi Bakwata

mbona tunawavuaga tu mara nyingi TENA kwa ridhaa yao AU udhalilishaji unakuaje!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Huo ni unafiki tu. Mbona yule mbunge wa CUF (V/M - Tabora) alipokamatwa kule Tabora na kukaguliwa mwilini na askari wa kiume hizi taasisi hazikulaani kitendo hicho? Aliposwekwa kwenye rumande mchanganyiko na wanaume mbona hawakupiga kelele hizo? Tatizo hapa ni hijabu na si haki ya mwanamke. Si kwamba naunga mkono hicho kitendo cha mtu kuvuliwa alama ya dini fulani lakini lazima tuwe fair kwa kila upande.
 
Hivi ile Albadil mliomsomea Mrema ili awe kichaa ilifua dafu? (kazi kweli kweli)

Kwa hiyo mkuu unaamini kabisa kwamba Mrema ni mzima? Basi kama ni mzima basi msiwe mnamlaumu kwa anayoyafanya!
 
Baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA), na Baraza kuu la Answar suna Tanzania(BASUTA), kwa pamoja wamelaani kitendo cha viongozi wa CDM Kumvua hijabu DC Fatuma kimario wamesema kitendo hicho walichofanya chadema kwa mujibu wa uislam ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani kwa hiyo amewataka viongozi wa CHADEMA kuwaomba radhi waislamu.

Naibu mufti akiwa mjini Tabora alisema Fatuma ana imani yake japo ni DC, heshimuni imani yake kwani waliomchagua wanajua kuwa imani yake inamtaka avae hijab alisema sheikh mohamed issa wa Answar Sunna.

CHANZO: Taarifa ya habari Radio Imaan

Jamani, DC anachaguliwa na nani!!!!!!!!!!!!!!????????????????? Kama ingekuwa kulaani nadhani kwanza wangemlaani DC kwa kwenda kuiba huku kavaa hijabu. Alikuwa anaudhalilisha uislam.
 
Jamani, DC anachaguliwa na nani!!!!!!!!!!!!!!????????????????? Kama ingekuwa kulaani nadhani kwanza wangemlaani DC kwa kwenda kuiba huku kavaa hijabu. Alikuwa anaudhalilisha uislam.

DC ameiba nini? wapi? kivipi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom