Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Status
Not open for further replies.
mahakama ya kadhi ingeamua akatwe mikono kwa kufanya vikao ili aibe kura za wana igunga khaaa
 
Bakwata huwa inashutumiwa hapa na pale na waislamu kwa baadhi ya wakati kuwa karibu na watawala kuliko na waislamu wanaowaongoza.Lakini kwa hili si Basuta tu waliowaunga mkono watafuata mashia na madhehebu nyengine.
Kuhusiana na mahakama ya kadhi wala usidhani mwisho wake ni kauli ya Kikwete na maaskofu.Hii mahakama kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu itakuja kwa kishindo huko mbele katika namna ambayo nyote mtashangaa.Chadema na wakristo wala hawatoiweza shari yake.
Mkuu sasa hivi si tayari mko kwenye mchakato wa kuanzisha mahakama ya Kadhi? au kuna mahakama ya Kadhi nyingine itakayokuja baadaye zaidi ya hii mnayoiandaa sasa hivi?
Kuhusu hayo mambo ya shari sisi wakristu kwa kweli hatuyawezi....sisi ni kama kondoo tu...kama mna majambia huko njooni mtuchinjilie mbali tu...maana tumefundishwa ..'Tusiwapinge waovu/adui....mtu akikupiga shavu la kushoto , mpe na la kulia'. Sisi tunaomba uzima na afya njema ili tuweze kuiona hiyo mahakama ya Kadhi ya kishindo!
 
CCM inacheza sana na akili za waisilamu maana ni rahisi sana kuwanasa. Wao ukitaka kuwateka tumia dini tu hata kama jana uliwatoa ngeo kama ni mwenzao mtapatana. Nadhani pengine ndivyo wananavyo fundishwa(ubinafisi wa kidini mpendelee mwisilami mwenzako)
Cha ajabu ni kwamba hawaamini kwamba CCM kamwe hawataweza kutimiza matakwa ya waisilamu yaliyo kinyume na katiba ya nchi hii hata kama mwenyekiti wake ni mwiisilamu. Atawandanganya tu na mwisho wa siku atawaambia hayo ni mambo yenu fanyeni wenyewe na huo ndo ukweli.

Hakuna Raisi nchi hii hata kama atakuwa shehe,padre au mchungaji atakayekubali kuvunja katiba ya nchi kwa ajili ya kuipendelea dini moja dhidi ya nyingine. Wenzetu waisilamu hawataki kukubaliana na hili wanadhani Raisi akiwa mwisilamu basi anaweza kupendelea uisilamu kitu ambacho hakitakaa kitokee nchi hii!

Kama Raisi wa Tanzania anataka asimalize hata mwezi Ikulu basi apendelee dini yake kwa uwazi aone kama kundi la pili litaogopa na kukaa kimya.

Kama kuna waisilamu wanaona CDM haimtendei haki (japo haijawahi kuwa na mamlaka ya kutenda au kutowatendea haki watanzania) aendelee kubaki ccm kama anaona kwake issue ni dini zaidi kuliko vita vya ufisadi na maisha magumu tuliyonayo watanzania kwa sasa. Hakuna anayemlazimisha mtu kuwaunga mkono chadema ila ni watu wenyewe wameua kutoka mioyoni mwao.

Hatuwadharau wenzetu waisilamu ila Imekuwa too much utafikiri wao ni yule mtoto kitinda mimba ambaye hagusi hata kidogo analia 'mamaaaaaa eti ....... ananishikakichwani'! Ndugu zetu lazima wajiamini waondokane na ile inferiority comprex na kudhani kuwa kuna mtu anawdharau.

Inashangaza sana kwanini kunakuwa na watu wao hujihisi kunyanyaswa tu kila wakati bila hata kuyaona manyanyaso yenyewe.
But nina marafiki zangu tumesoma nao ni waisilamu lakini wanajiamini sana na ni wapenzi wa chadema wa kufa mtu.

ndugu zetu jiaminini kwanza bila hivyo itasumbua sana na hatutakaa tutatue matatizo ya msingi ya nchi yetu. Kumbukeni mtaendelea kutumiwa tu na ccm kama toilet paper wakati wa uchaguzi wakishapata mnabaki palepale labda na nyie muwe mafisadi wakati dini hairusu.

Tuweni kitu kimoja bila kujali dini zetu tumshughulikie adui wa watanzania wote ambaye ni ccm. Hata Kama baadhi yenu mtakataa bado Mungu akisema ndiyo hakuna atakayezuia.

Mungu ibariki Tanzania!
 
Hivi mzee Mwinyi alivyozabwa kibao kwenye hutba na kijana wa kiislam....

kitendo cha ukosefu wa nidhamu kwa rais mstaafu na akasamehe,

sikuona such 'tamkos' au malumbano meeeengi, tulikemea na mzee wa watu alipotezea
Kwa hili la rais mtaafu Mwinyi, mtazamo wa waislam wengi ni kama wa yule kijana aliyemchapa kibao mzee wetu. Kwa mtazamo wao ni Mwinyi ndiye aliyekosa maadili eti kwa kuhimiza matumizi ya condom kujikinga na ukimwi. Ni vigumu sana kujua waislam huwa wanasukumwa na nini wawanapofanya maamuzi yao!
 
Kwanza kabisa neno hijabu(mtadio) haimfanyi mtu kuwa muslim au christian kimantiki ila kidini mwanamke yeyote yule anabidi ajistili awe mwisilam au mkristo neno hili lipo kwenye Biblia pamoja na Quran.
Hatuwezi sema kuwa huyu DC alivulia vazi la uislam au ukristu alafu tufanye itimisho eti wameizalilisha dini fulani tutajikuta buyers of phenomena than talking the essence of phenomena.
DC yawezekana alitaka fanya ujuma ambayo ata Quran haikubali sasa watu hakotayari kuona hili, hawa waliomsaidia asipate dhambi kwakufanya hujuma wamemsaidia na wamepata dhawabu.
Hao wanao komaa kusudi waombwe samahani ingawa SAYING SORRY IS LIKELY TO BE CHEAP kama hautaifanyia tadhimin kwa yaweza pia kuwa costful.Wakuu Elimu ya uislam wengi wanadhani ukienda madrasa basi wewe umemaliza utasikia mwengine anajiita Ulamah nk.. lkn mlete kwenye msahafu atakuambia hapo ustadhi umeniacha.
DC alikuwa kwenye kazi na majukumu ya dini au siasa na Quran inasemaje kuhusu mwanamke kwenye siasa na uongozi?
BAKWATA na BASUTA nyie ndo mnabidi kuiomba radhi CHADEMA na WaTZ kwa sababu ya kukurupuka na kuweka masilai yenu mbele u deviant.
Hizi ni hujuma za dirty and nasty CCM ambazo vyama vingi vikongwe vinazitumia sana mara utasikia wapinzani wanataka kuvuruga amani lkn hawajiulizi kwa nini wananchi wamefikia hapo.SOLVING PROBLEM ISNT THE BEST WAY RATHER THE ESSENCE OF THE PROBLEM.
 
Huyo mama anafahamu nini maana ya uislamu?
 
kuna rafiki yangu muislam kutoka pakistan, yeye alisha niambia uislamu ni dini unayo takiwa kutumia akili ili uweze kuifuata na kutoa matamko, na kuna wakati alinipa mfano wa yule bennaziar bhuto alivyo kuwa ana shangiliwa na watu wakati yeye marehemu bennaziar ana kasri uingereza, mumewe alikuwa mtu wa ten percent etc etc. sasa ukitumia masaburi kwa kweli utaupotosha uislamu.
na sasa wale vibaka wakiwa wamevaa zile kofia zetu , katika kurupshani na polisi kofia ikadondoka, polisi atakuwa amefanya kosa?
au wakafanya maandamano kama vile Bi Mushumbusi , polisi katika pirika pirika zao hijab etc vikadondoka, polisi atakuwa amefanya makosa?
 
BAKWATA ni mapapeti tu. Hamna kitu. Ni wadau wa CCM.
 
Ngoja waongee ongee wakifikiria mahakama ya "kadhia" wataonewa huruma wapewe
 
"Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (HAY-AT) umetoa tamko lililosomwa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti Kuu ya Umoja huo, Shehe Sherali Hussein Sherali na kuipa Chadema siku tatu iombe radhi".

Majina ya kuiga yana matatizo yake umoja unaitwa hayati duh.
 
CHADEMA waachane na siasa katika hili watekeleze agizo la Bakwata na Basuta.Kinyume cha hivyo chama kimekufa kabisa.
Mwanzo Chadema mlijitetea kwa taabu kwenye kampeni.Hapa kwenye hili ndio mmepiga muhuri kwamba Chama chenu kina chuki na uislamu.
Ingekuwa huyu DC ni mkristo wala kikao alichokuwa akifanya isingekuwa nongwa.
Ikiwa ni wizi wa kura mara ngapi mumekuwa na hisia hizo mbona haijawahi kutokea DC akakokotwa kama ng'ombe kwa kutumia hijabu!.

Duh!!! bongo kweli tambarareeeeeeeee!!
 
Hili si suala la Bakwata au kundi fulani la waislaam, muislaam mmoja amedhalilishwa ni sawa na kuudhalilisha umma wote wa Kiislaam. Walaaniwe laana zaidi ya walionazo sasa hao waliofanya fanya hivyo.
 
Kila issue na wakati wake..

Mahakama itabaki kuwa issue na kuvua mwanamke hijabu itabaki kuwa issue

Besides kwani nini msimamo wa chadema kuhusu mahakama ya kadhi?

hauna tofauti na matakwa ya maaskofu...so ccm na cdm kwa issue ya waislamu wako pamoja mkuu hawana tofauti yoyote...
jitambue.
Mkuu wangu unanifanya naanza kuamini maneno ya wakristu kuhusu elimu za waislaam na yawezekana kweli imechangia sana kuwa wajinga pamoja na kwamba Mtume alisistiza elimu...

Mkuu wangu, hijab ni vazi la kike na limesisitizwa kwa malengo na makusudi kama vile mzungu anavyosisitiza kuvaa tai kwa mwanamme. Ina maana yake na sababu zake mwanamke kuvaa hijab, na akivaa haimfanyi kuwa muislaam isipokuwa tunafuata mafundisho kama vile wewe unapovaa suruali ama nguo inayovuka magoti ni maagizo ya mitume vile vile ktk mavazi.

Na kisha ebu waulize hao masheikh je mwanamke aliyevaa mtandio wa Khanga kufunika kichwa chake ni Hijab? watakwambia hiyo sio Hijab isipokuwa Hijab ni mtandio ule ulotoka Dubai au Oman na ndivyo mnavyoitafsiri Kanzu kuwa vazi la waislaam. Kesho mtu akivamia na kuchaniwa kanzu basi ni kuudhalilisha Uislaam..
Hawa waarabu wamewaharibu sana kiasi kwamba hata majina mnaamini kabisa ni majina ya kiislaam mtu akiitwa Omar au Hamza lakini sii yule anayeitwa Richard, wakati huo huo huwezi kunambia swahaba yeyote wa mtume aliyebadilisha jina lake baada ya kuuukubali Uislaam kwani majina hayo waarabu wa imani zote huyatumia. Baba yake mtume aliiitwa Abdallah na hakuwa Muislaam lakini ukienda Bongo ukisema jina lako Abdallah basi lazima utakuwa Muislaam.. Tembeeni mkaizunguke dunia myajue mengi jamani, waarabu wanayatumia majina haya bila kujali dini zao. Jamani eeeeh Uislaam ni Imani na ibada, majina, hijab na kanzu sio Uislaam ...Abu Talib mtamweka wapi nyie!

Nitarudia kusema kwamba Hijab ni vazi la kike na limesisitizwa na mitume kwa wanawake wote (ustaarabu) na sii Uislaam, bali jinsi ya mwanamke to carry herself and be respected kama ilivyo hulka ya kidunia tunapomwona mwanamme amevaa shati na tai, tai inaongeza heshima fulani hata kama hakuna sababu ya maana kwa mtu asiyevaa tai, lakini ukweli utabakia kwamba mvaa tai atatazamwa na kupokelewa na heshima fulani ndivyo inavyokuwa kwa mwanamke na Hijab..Hii ni ktk moja ya mapungufu ya kibinaadam hatujakamilika.

Ama kweli mtume alisikitika sana na kusema hakika Umma wake ni wachache sana wataingia peponi!...na hakika dalilizote zinajionyesha, hapo hapo mimi naongezea kusema Uislaam ni dini isiyokuwa na watu, hali Wakristu ni watu wasiokuwa na dini...
- Ukweli unauma, mtanisamehe nyote.
 
Sikujua kama umekalia tango.
Acha hasira bibie, hutaweza kufukia kiwango cha FF. We endelea kuwastarehesha kina Slaa huko Igunga na achana na siasa, si ndio kazi uliopewa. Hizi hela zitawaua
 
This isn't my place to comment but let me say something bit .... huyo mama ni anafanya kazi ya bakwata au serikali? Just simple q.

Mnaonekana kweli wapo ignorant wengi ndani ya hivi vyombo vya ccm.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom