Ujumbe wa Askofu Niwemugizi Krismasi ya 2023: Muhtasari, maswali na tafakari

Mama Amon

JF-Expert Member
Mar 30, 2018
2,021
2,478
1704225423134.png



I. Utangulizi

Askofu Severine NiweMugizi ni miongoni mwa Maaskofu wa Kanisa Katoliki machachari sana.

Huwa hataki kulala na dukuduku moyoni mwake hata siku moja.

Pia historia yake kama Askofu inaonyesha kwamba ni mtu asiyependa wala kuvumilia ukaidi dhidi ya mamlaka halali.

Hata hivyo, salamu zake za Krismas ya 2023 ziliambatana na maoni yake binafsi kuhusu tamko liitwalo "Fiducia Supplicans" lililotolewa na Papa Francis, hapo 18 Desemba 2023, akiwa anaonyesha ukaidi wa wazi dhidi ya Papa, ambaye ni mamlaka yake ya kinidhamu.

Askofu NiweMugizi ametoa maoni yake wakati ambapo tayari makuhani kadhaa, wakiwemo Askofu Ruwaichi wa Dar es Salaam, Flavian Cassala wa Geita, na Padre Titus Amigu wa Songea, wametoa maoni yao dhidi ya agizo la bosi wao Papa Francis.

Kuna maoni mseto ndani na nje ya Afrika, wanaompinga Papa wakidai kuwa tamko la Papa linapingana na "hazina ya imani," yaani "deposit of faith," tuliyorithishwa na Yesu. Wanaomuunga mkono Papa wanasema "hazina ya imani" husika haijaguswa kabisa na tamko la Papa.

Lakini pia, kuna baadhi ya maoni yaliyotolewa yanawaweka makuhani husika katika kundi moja na dikteta maarufu Adolf Hitler wa Ujerumani aliyefundisha kwamba mashoga, wayahudi, gypsies, wazee na walemavu ni "uchafu" unaopaswa kuondolewa kwenye jamii ili kutengeneza kizazi bora cha Watu.

Mpaka leo dunia inampinga Hitler kwa sababu ya kuwaita wanadamu hawa "uchafu," na kisha kuwateketeza kwenye chemba za gesi, na hivyo kusigina utu wao.

Kwa sababu hizi, hapa chini nitafupisha salamu za Askofu NiweMugizi na kisha kufanya udadisi juu ya baadhi ya mawazo yake dhidi ya tamko liitwalo "Fiducia Supplicans."

Lengo ni kuhuisha fikra za Kikatoliki kuhusu ujinsia wa binadamu kama unavyofahamika leo katika milenia ya tatu.

II. Muhtasari wa salamu za Askofu NiweMugizi

Naitwa Severine NiweMugizi, kwa neema ya Mungu tu, Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara. Naomba nikuletee salam na ujumbe wa Krismasi ya 2023....

Mpendwa msikilizaji tunaalikwa kumkubali mtoto Yesu azaliwe mioyoni mwetu. Aiguse mioyo yetu ibadilike kuwa mioyo safi. Atuguse tuwajibike inavyopasa....

Tumuombe atuguse tuache dhambi, uhasama, visasi, uvivu, uzembe, utapeli wa aina mbalimbali...

Tunaadhimisha Krismas hii pia baada ya Baba Mtakatifu, Fransis, kuridhia waraka uitwao "Fiducia Supplicans" yaani "Supplicating Trust."

Hili ni tamko kuhusu fundisho la Kikatoliki lililochapishwa mwezi huu, Desemba, na Dikasteri au Idara inayohusika na mafundisho ya imani ya Kikatoliki. Ujumbe wa Waraka umezua taharuki ndani na nje ya Kanisa Katoliki.


Sababu ni maagizo ya Papa yasemayo kwamba maaskofu na mapadre wanalo jukumu la kubariki watu walio katika miungano isiyo ndoa halali ikiwa ni pamoja na miungano ya wale watu wa jinsia moja, yaani mashoga na wasagaji.

Hasa dhamira za watu zimejeruhika kwa sababu ya tamko hilo na kumekuwepo na mlipuko wa mijadala kuhusu hilo...

Msimamo wa Kanisa katika mafundisho ya msingi ya imani na maadili hauwezi kubadilishwa na mtu mmoja. Papa peke yake hana mamlaka ya kubadilisha mafundisho hayo, kama hayuko katika ushirika kamili na maaskofu wenzake.

Ufunuo wa maandiko matakatifu unaweka wazi kwamba ndoa ni muungano kati ya mwanamume na mwanamke. Na Yesu amesema wazi hasa ukisoma enjili ya Mathayo sura ya kumi na tisa... Nanukuu:


"Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa sababu yoyote? Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mwanamume na mwanamke akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?... Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni." (Mathayo 19:3-6, 12).

Hapa ieleweke kuwa mtu yule anayetajwa hapa ni mwanaume... Mwanamke na mwanamke au mwanamume na mwanamume hawawezi kufunga ndoa iliyo halali....

Nitaje hapa, kama mchungaji wa Kanisa, Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara, baraka ziombwazo na watu wa jinsia moja wanaokuja pamoja na wanafahamika kuwa mashoga au wasagaji ni marufuku kwa mapadre kuzitoa jimboni Rulenge Ngara.

Amri hii inatolewa kwa sababu kwa sura ya nje baraka hiyo inaweza kutafsirika kuwa ni kuwathibitisha na kuwaombea waendelee na wastawi katika muungano huo ambao ni dhambi.

Hali hii itakuwa kinyume na Kristo na kikwazo kwa jamii ya waamini na hasa ukifanyika hadharani.

Nirudie tena kusema, kama waraka ulivyotambua wale watu wa jinsia moja wanaokuja kanisani hawawezi kufukuzwa. Ni wana wa Mungu kwa vyovyote. Na hao wakija kuomba kufanya kitubio watabarikiwa ili waungame na kuacha muungano ulio dhambi. Huo ndio msimamo halisi.

Baadhi ya maelezo yaliyo katika waraka yanaonekana yana mtego fulani, kwa sababu baada ya kutolewa kwa huo waraka tayari watu walianza kufurika kwa mapadre kwenda kuomba baraka na wakiwa wameshikana mikono. Hali hii inaleta kikwazo fulani.

Hivyo, tutulie na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania muda si mrefu litatoa pia tamko au msimamo kuhusiana na waraka huu....


III. Maswali yanayoibuliwa na salamu za Askofu NiweMugizi

Kwa sehemu kubwa salamu za NiweMugizi hazina tatizo. Anasisitiza kuwa Tamko la Papa halijatengua mafundisho rasmi ya Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni kitu gani na sio kitu gani. Sawa.

Tatizo liko kwenye sehemu moja tu ambapo anakaidi agizo la Papa Francis ambaye ametoa agizo kwamba maaskofu na mapadre wanalo jukumu la kubariki watu walio katika miungano isiyo ndoa halali ikiwa ni pamoja na miungano ya wale watu wa jinsia moja, yaani mashoga na wasagaji, pale Watu hawa watakapoomba baraka hizo.

Askofu NiweMugizi amekaidi hadharani agizo la Papa kwa kutumia hoja kwamba ni agizo haramu kwa mujibu wa maandiko matakatifu. Ukaidi huu unaambatana na changamoto kadhaa kama zinavyojadiliwa hapa chini.

Tatizo la kusahau kutofautisha maneno "fiducia" na "fides"

Wanateolojia na wanafalasafa ya lugha wanatofautisha kati ya "Fiducia" na "fides." Wakati "fiducia" linamaanisha "affective faith" neno "fides" linamaanisha "rational faith."

Kuhusu tofauti hii Chia na Juanda (2020), katika makala yao "Understanding the Relationship Between Faith and Knowledge," iliyochapishwa kwenye Jarida liitwalo Didaskalia (Volume 3, issue Number 1), ukurasa wa 2-3, wanasema yafuatayo:

"Faith is employed both as an epistemological and as a non-epistemological term. The words fides and fiducia provide conveniently self explanatory labels for the two uses.
"We speak, on the one hand, of faith (fides) that there is a God and that such and such propositions about him are true. Here ‘faith’ is used cognitively, referring to a state, act, or procedure which may be compared with standard instances of knowing and believing.
"On the other hand, we speak of faith (fiducia) as a trust, maintained sometimes despite contrary indications, that the divine purpose toward us is wholly good andloving.5 Hick, thus, defines faith not only in area of cognitive but also feeling."
"Speaking theologically, faith has passive and active meaning. Passively, faith is God’s work in us that changes us and gives new birth from God (John 1:13). Actively, on the other hand, it means believing, obeying, trusting, hoping, and being faithful in Christ and Holy Scripture. Therefore, faith is two-sided coin. On one hand, it has a beginning, in the past, but it does not stop but it is ‘on going’ activity such as obeying and being faithful."

Ni katika mazingira haya Papa anataja maana tofauti za neno "baraka." Hivyo, naona kuwa, kwa kuzigatia maana hizo tofauti, Askofu NiweMugizi alipaswa kutaja maandiko mataktifu yanayokataza "baraka" maalum kwa miungano ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Hakufanya hivyo.

Kimsingi, ukiangalia Tamko la Papa, na ukazingatia tofauti za maneno "Fiducia" na "fides" ambazo Askofu NiweMugizi anazofahamu vizuri kuliko mimi, "hazina ya imani" kwa maana ya "fides" bado iko salama.

Tamko la Papa ni ufafanuzi unaowataka makasisi kuondokana na dhana kwamba homosexuals, transgenders, intersexuals na eunuchs ni "uchafu" kama alivyokuwa anaamini na kushikilia Papa Yohane Paul wa pili.

Na bado Papa Yohanne Paul II anao wafuasi wake leo wenye kufikiri namna hii. Askofu Flavian Cassala ni mmoj wao. Lkini zama za sayansi zimepindua mtazamo huo.

Askofu NiweMugizi ni mtalam wa sheria za Kanisa. Anajua vema kwamba sheria za Kanisa zinatofautisha kati ya mawazo yafuatayo: "ratification," "consumation," "blessing," "marital act," na mawazo baki kama haya.

Katika mipaka ya misamiati hii Tamko la Papa Francis halijakiuka sheria za Kanisa. Ni agizo halali, na ukaidi wa Askofu NiweMugizi ni haramu inayistahili adhabu ya kiutawala.

Baraka anazoziongelea Papa Francis hazina tofauti na zile zinazotolewa kwa wezi wakubwa waliothibitika kwamba wameiba, na hawajarudisha walichokiiba. Mpaka leo tunawaona Kanisani wakipokea baraka.

Hivyo, ufafanuzi wa Askofu NiweMugizi unaibua maswali yafuatayo: Kasisi anaweza kuogopa kutekeleza majukumu yake kwa sababu tu ya hofu kwamba watu wanaweza kutafsiri matendo yake isivyo? Kama jawabu ni ndiyo, kwa nini kuna undumilakuweili kuhusu baraka kwa wezi wanaofahamika kwa jamii na wazinzi wa jinsia moja?

Tatizo la kisemantiki

Lakini pia, kuna tatizo la kisemantiki na kiepistemolojia. Kanisa Katoliki linamaanisha nini linapotumia neno "ushoga"? Na linatumia utaratibu gani kuwatambua mashoga na wasagaji?

Kuna matukio kadhaa yanaonyesha kwamba, ndani ya Kanisa Katoliki, neno "ushoga" linatumika kihuni kama silaha ya kipropaganda kwa ajili ya kuwanyamazisha wakosoaji wa baadhi ya misimamo tata ya kanisa katoliki tena wakati mwingine dhidi ya watu wasio na hatia. Mifano ipo.

Kifo cha Rodney Mutie Mengi mwaka 2005 kilizua mvutano kati ya baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki na Reginald Mengi, mzazi wa Rodney.

Mengi aliweka bayana kwamba mwanaye alikufa kwa UKIMWI, hivyo akahimiza watu kuwa waaminifu au kuwa waangalifu kwa kujikinga kwa kutumia kondomu.

Miongoni mwa watu walio mjibu tena kwa maandishi kupitia magazeti ni Askofu NiweMugizi.

Baadaye kidogo, gazeti la Kiongozi likaunga mkono pilika hizi kwa kuchapisha habari isemayo kuwa "Serikali Ikemee Ushoga."

Kisha Askofu KIlaini akawaita Maparoko wote wa Dar na kuwapa orodha ya watu ambao anaona kuwa ama ni manabii wa "ushoga" au mashoga kabisa, kwa sababu tu kwamba wanaandika kuhimiza matumizi ya kondomu kama kingamagonjwa na/au kingamimba.

Maparoko wakasukuma taarifa hizi kwa walei, na walei wakazisambaza mitaani na serikalini.

Mie taarifa hizi zilinifikia kupitia mjumbe was baraza la walei parokia ya kimara.

"Paroko amesema kuwa Askofu KIlaini amekutaja kwenye orodha ya mashoga. Pia wamo Mashanga na Priva," mtoa taarifa alisema.

Nikamshukuru kwa taarifa na kuingia kazini.

Nilikuwa najua kuwa Professional Janet Smith ameandika kitabu kizuri just ya mada ya "contraception" kikiitwa "He manage Vitae: A generation Later."

Nikatinga Cathedral Bookshop na kuweka oder. Mpaka kesho naisubiri order hiyo. "Baba Askofu KIlaini amesitisha order yako," wahudumu was duka la vitabu walinijuza.

Sikuchoka. Nikitumia mifereji baking ya maarifa kukielimisha. Sasa Nina weledi wa masumbwi ya hoja kwa kiwango Cha kumtoa kwa knock out Askofu KIlaini katika raundi ya Kwanza.

Kwa ujumla, picha kubwa niliyoibaini hapa ni kwamba , kina KIlaini wanaamini kuwa mapenzi ya jenitalia kwa jenitalia yanayofanyika kwa kutumia kingamimba kama vile kondomu ni tendo la kishoga.

Yaani, huu ni mtazamo kwamba watu wawili wa jinsia tofauti, na hivyo ambao sio mashoga, wanaweza kufanya tendon la kishoga.

Lakini ukweli ni kwamba, pasipo "homo-affective condition" hakuwezi kuwepo na "homosexual acts."

Na inaonekana kwamba, haya ndiyo mafundisho wanayopewa vijana wetu huko seminarini. Wanafunzwa teolojia ya ushoga inayowafanya mbele ya jamii waonekane Kama Watu wenye kuumwa ugonjwa wa umachuaveli wa kiteolojia (theological machiavellism)

Ni mafundisho mabovu yanayoliweka Kanisa Katoliki karibu na mafundisho ya kishirikina na kuliweka mbali na mafundisho ya kisayansi kuhusu ujijsia was binadamu.

Lakini, bado kuna shida kubwa zaidi katika eneo hili la kisemantiki.

Maelezo mengi ya makasisi wetu, akiwemo Askofu Ruwaichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, hayatofautishi kati ya "homo-affective condition" na "homosexual acts."

Utafiti unaonyesha kwamba, mkanganyiko huu umeenezwa mpaka ngazi ya ndoa kupitia mafundisho kwa wanandoa kabla ya kufunga ndoa.

Wakati wa mafundishi haya ya wanandoa, maparoko wengi wanawambia "wanafunzi wao" kwamba "ni mwiko kwa wanandoa kufanya ushoga," yaani ulawiti, utadhani kwamba mashoga wote wanafanya ulawiti.

Wanachofanya maparoko hawa ni sawa na kufanya uenjilishaji wa kufundisha amri za Mungu kwa kuwambia waumini kwamba: usiue kama wanavyofanya Wanyakyusa, usizini kama wanavyofanya wahaya, usiibe kama wanavyofanya wachaga, usiseme uwongo kama wanavyofanya wazaramo, usitamani mke wa jirani yako kama wanavyofanya wangoni, na orodha inaendelea.

Lakini, sio Wanyakyusa wote ni wauaji, sio Wahaya wote ni wazinzi, sio wachaga wote ni wezi, na kadhalika, Kwa hiyo, uenjilishaji wa aina hii ni matumizi ya mbinu haramu kwa ajili ya kufanikisha lengo zuri, yaani "umachiaveli."

Basi, kwa njia hii maparoko wanawavisha miwani ya kishoga wanandoa na wao kuanza kuitazama dunia kwa kutumia miwani hiyo. Miwani hii ni tatizo la kijamii maana inawaonyesha "ushoga" hewa.

Tatizo hapa ni kwamba, maparoko husika wanasahau kuwa sio kila ulawiti ni tendo la kishoga na kwamba tendo la ulawiti kati ya mwanamke na mwanamume sio, na haliwezi kuwa, tendo la kishoga.

Kimsingi, kuna janga la kisemantiki ndani na nje ya Kanisa Katoliki kuhusu maana ya neno "ushoga." Napenda kufahamu Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu tatizo hili.

Tatizo la kiepistemolojia

Kiepistemolojia pia kuna tatizo kubwa. Kuna waseminari kadhaa huko seminari kuu wamekuwa wakiachishwa masomo kwa sababu ya madai kwamba wana "vidole vya kishoga," ambavyo ni dalili ya ushoga.

Yaani wakuu wa seminari wanatumia "second to fourth digit ratio (2D:4D ratio)," mbinu ambayo haikubaliki kisayansi. Nimewashuhudia Padre Kaombe, hayati Profesa Kanywanyi, na watu baki wakitumia mbinu hii pia.

Kuna makruta waliwahi kufukuzwa kwenye mafunzo kwa kutumia kigezo hiki pia. Kuna dalili kwamba "mafundisho tata ya Kikatoliki kuhusu namna ya kuutambua ushoga" yalikuwa na mchango hapa pia. Hili ni janga la kiepistemolojia katika jamii. Napenda kufahamu Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu tatizo hili.

Tatizo la "tuhuma hewa" za kumomonyolewa kwa "hazina ya imani " Katoliki

Kuna madai yasiyo kweli kwamba Tamko la Papa limemomonyoa "hazina ya imani" Katoliki. Propaganda hii inaenezwa sana na mabaraza ya Maaskofu sehemu nyingi duniani. Inafika mahali ninatilia shaka weledi wao juu ya kile wanachokiongelea.

Kwa ufupi, hoja ya "Fiducia Suplicans" (Suplicating Trust) inaweza kufupishwa katika sentensi tatu kama ifuatavyo:
  1. Liturgical blessings, such as marital ratification, are exclusively reserved for individuals and heterosexual couples who are living in regular situations, meaning that, their lifestyles are compatible with God's will.
  2. Non-liturgical blessings can be administered to individuals and couples who are living in either regular situations or in irregular situations, meaning that, even individuals and couples whose lifestyles are incompatible with God's will, can receive them.
  3. Thus, couples in irregular situations such as a cohabitating couple, a contracepting couple, a polygamous couple, a couple in civil marriage, a pedicating heterosexual couple, and a pedicating homosexual couple can receive non-liturgical blessings, as a means toward conversion to perfection.
Naye Dr. Christopher J. Malloy(2023), Professor wa Theolojia katika Chuo Kikuu cha Dallas, katika posti yake moja mtandaoni amefafanua waraka huu kama ifuatavyo:

"The document Fiducia supplicans (FS) of the Dicastery for the Doctrine of the Faith (DDF) claims that priests may, in certain circumstances, give blessings to “couples in irregular situations and same-sex couples” (Víctor Manuel Cardinal Fernández, “Presentation”; FS 31). The qualifying circumstances include the following factors: scandal must be avoided (FS 30, 39), the blessing is to be informal and not performed in a liturgical setting (FS 9-11, 23-24, 31-39), and the blessing must neither lead to confusion (FS 5) nor signal a change in the Church’s moral teaching (Fernández, “Presentation,”; FS 3, 4)...
"FS includes a helpful set of reflections on the various kinds and parts of blessings (a descending gift from God, an ascending prayer of praise or thanksgiving to God, and an extending of blessing towards another). In this essay, I focus on the descending aspect. A blessing is chiefly (as a descending reality) a gift of divine assistance in the present for the ultimate good of the recipient. As such, a blessing is a means to an end. The ultimate end of any blessing is of course eternal salvation, but the proximate end is some present good suitable for the journey to heaven. A blessing targets the recipient either simply as a person—called to be a son or daughter of God—or according to some special aspect, activity, or purpose in life. If the blessing targets a special activity, it gives wings, so to speak, to the person in that activity, approving it and assisting it...
"In its climactic paragraph, it states, 'Within the horizon outlined here appears the possibility of blessings for couples in irregular situations and for couples of the same sex' (FS 31). Clearly, FS is here treating persons as partners. Thus, it is treating them under a special aspect, namely, as being partners in various kinds of non-marital sexual relationship: unmarried, adulterous, and homosexual...

Pia Dkt. Erick Ybara(2023) kwenye post yako moja mtandaoni anaongeza ufafanuzi ufuatao kuhusu waraka huu:

"Liturgical blessings require the object to conform to God’s will. Enduring and maintaining a SS union does not conform to God’s will. Therefore, SS unions cannot be the object of a liturgical blessing.
"However, blessings are not to be reduced to liturgical blessings (only), since, there are blessings such as the one given by God to mankind by sending His Son to be our Lord and Saviour. Just that blessing on its own had as object the unworthy, sinful, and fallen world of man. Such a blessing surely had no preconditions nor did it require us to do anything. It was all a move of God’s free and undeserved mercy, love, and grace.
"From this consideration, a pastoral option opens for the Church to use the power of the priesthood to administer blessings towards SS unions without requiring the couples to quit their sin...
"The blessing should fall upon the couple in such a way that the persons, as objects, have enriched everything that is 'good, true, and humanly valid' in their lives. So the blessing is for the enrichment of whatever is good, true, and beautiful in their life. Not only that, but it says that the blessing might enrich all that is good, true, and humanly valid in their lives “and in their relationships"...

Kwa kuzingatia ukweli huu, nimesikiliza maelezo ya Askofu NiweMugizi ili niweze kubaini wapi Tamko la Papa linasigina "hazina ya imani" ("deposit of faith") kwa kiwango ambacho kinahalalisha ukadi wa hadharani kama alivyofanya. Pia nimepitia maoni ya "Maaskofu Waasi" sehemu mbalimbali duniani kwenye andiko "List of opponents of Fiducia supplicans" lililoko Wikipedia.

Nilitaka kujua wapi Papa amekosea. Kuna maelezo ya jumla kwamba Papa amekiuka mafundisho Katoliki kuhusu ndoa ni kitu gani na sio kitu gani. Lakini nikisoma tamko la Papa sioni jambo hilo. Nataka kuonyesha ukweli huu kwa kuanzia mwaka 1968. Tuanzie hapa:

"Marriage … is … the wise and provident institution … whose purpose …[is] to effect in man …[a] loving design ... as a consequence [of which], husband and wife, through that mutual gift of themselves, which is specific and exclusive to them alone, develop that union of two persons in which they perfect one another … in the generation and rearing of new lives." (Pope Paul VI (1968), Humanae Vitae, para 8).
"This particular doctrine [that each and every marital act must of necessity retain its intrinsic relationship to the procreation of human life], often expounded by the magisterium of the Church, is based on the inseparable connection, established by God, which man on his own initiative may not break, between the unitive significance and the procreative significance which are both inherent to the marriage act." (Pope Paul VI (1968), Humanae Vitae, para 12).
"Therefore ... excluded is any action which either before, at the moment of, or after sexual intercourse [between two fertile heterosexual persons], is specifically intended to prevent procreation [using a condom, swallowing contraceptive pill, vasectomy, tubal ligation, using a cervical barrier, norplants, withdrawal, fellatio, manual sex, thigh sex, interbreast sex, armpit sex, heterosexual pedication or homosexual pedication]." (Pope Paul VI (1968), Humanae Vitae, para 14).

Hivyo, kihistoria, kwenye mipaka ya Waraka wa Humanae Vitae, fasili ya ndoa ifuatayo inahusika:

"Heterosexual marriage is a union between a man and a woman which is ratified in public under an oath to live together for their entire common life to the exclusion of all others, as husband and wife, after it has been consummated by sexual acts which simultaneously entail unitive significance and procreative significance, and which are then regularly used to actualize it, regardless of whether they are procreative in effect or otherwise." (My synthesis from Humanae Vitae 1968, para 8, 11, 12).

Kwa kuzingatia mafundisho haya, mwaka 1983 sheria ya Kanisa Katoliki, iliyoandaliwa na Papa Yohanne Paul II akiwa kama mtunga sheria mkuu wa Kanisa, chini ya kifungu cha 1055(1), ilitoa fasili ifuatayo kuhusu ndoa:

"Marriage is a covenant , by which a man and a woman establish between themselves a partnership of their whole life, and which of its very nature is ordered to the wellbeing of the spouses and to the procreation and upbringing of children."

KIfungu cha cha 1057(2), kinafafanua kwamba:

"Matrimonial consent is an act of the will by which a man and a woman mutually give and accept each other through an irrevocable covenant in order to establish marriage."

Hatimaye, kifungu cha 1061(1) kinatofaitisha kati ya kubariki ndoa (ratification) na kuthibitisha ndoa kitandani (consumation) kama ifuatavyo:

"A valid marriage between the baptized is called ratum tantum (ratified) if it has not been consummated; it is called ratum et consummatum (consumated) if the spouses have performed between themselves in a human fashion (humano modo) a conjugal act which is suitable in itself for the procreation of offspring, to which marriage is ordered by its nature and by which the spouses become one flesh."

Chini ya vifungu hivi, kuna pointi mbili muhimu za kisheria. Pointi ya kwanza ni kwamba watu wanaohusika na utoaji wa ridhaa ya kufunga ndoa ("the subject of matrimonial consent”) ni mwanamume na mwanamke ("man and a woman)."

Na pointi ya pili ni kwamba, tendo la ngono linarodhiwa na wanandoa ("the object of matrimonial consent”) ni "a conjugal act which is suitable in itself for the procreation of offspring...by which the spouses become one flesh," yaani "tendo la ngono linaloweza kusababsha mimba ... ambalo huwafanya mwanamke na mwanamume kugeuka mwili mmoja".

Kwa kuzingatia ushahidi wa kisayansi tulio nao leo, pointi hizi mbili zikitazamwa kwa kutumia miwani ya kimantiki zinatualika kuuliza na kujibu maswali yafuatayo:
  • "Is canonical marriage involving homosexual couples possible?
  • "Is canonical marriage involving intersexual couples possible?
  • "Is canonical marriage involving transgender couples possible?
  • Is canonical marriage involving infertile couples possible?
Tayari hapo juu tumeona kwamba, kwa mujibu wa sheria za Kanisa Katoliki, mtazamo wa kisheria ni kwamba, "the subject of matrimonial consent” ni "mwanamume na mwanamke," na kwamba, "the object of matrimonial consent” ni "tendo la ngono linaweza kusababisha mimba" Hivyo, tunapata jawabu la "hapana: kwa maswali yote manne hapo juu. Yaani:
  • canonical marriage for homosexual couples is impossible since they are closed to new life.
  • canonical marriage for intersexual couples is impossible since they are closed to new life
  • canonical marriage for transgender couples is impossible since they are closed to new life
  • canonical marriage for infertile couples is impossible since they are closed to new life
Kutokana na majawabu haya, maswali mapya mawili yanaibuka:
  • Kama jawabu kwa maswali haya yote manne ni "hapana" kwa sababu ile ile ya "ugumba" nini hatima ya makundi haya ndani ya Kanisa Katoliki?
  • Kama jawabu kwa maswali haya yote manne ni "hapana" kwa sababu ile ile ya "ugumba" kwa nini jozi ya mwanamke na mwanamume ambayo inahusisha angalau mgumba mmoja wanaruhusiwa kufunga ndoa Kanisani?
Wanazuoni Katoliki wanatoa majibu tofauti kwa maswali haya. Kuhusu swali la kwanza, baadhi wanasema kwamba sheria za Kanisa zibadilishwe kwa kulegeza masharti juu ya "the subject of matrimonial consent” pamoja na "the object of matrimonial consent.”

Lakini wako wanazuoni wanaopinga pendekezo hili kwa hoja kwamba maneno "mwanamke na mwanamume" yanatokana na mafundisho ya Biblia yasiyoweza kubadilishwa na binadamu.

Na kuhusu swali la pili, baadhi wansema kwamba, kwa kuwa ndoa ya wagumba hufanya mapenzi katika namna ambayo inatekeleza hatua ya kwanza ambayo ndoa ya wazazi hutekeleza, basi wanayo sifa ya kisheria ya kuwaruhusu kufunga ndoa kwa mujibu wa sheria za Kanisa.

Lakini, wanasayansi na wanafalsafa wanaozingatia ukweli kwamba pale ambapo yamkini ya "final cause" kutokea ni ziro, basi, tendo la ngono ya wagumba haliwezi kuwa na hadhi sawa na tendo la ngono ya watu ambao sio wagumba.


Kwa ufupi, maswali yote sita hapo juu yanahitaji mijadala ya kiufundi katika ngazi ya kisayansi, kiteolojia na kifalsafa. Mijadala hiyo lazima itoe majawabu makini kwa maswali matatu yafuatayo:
  • What is a man and who counts as one?
  • What is a woman and who counts as one?
  • What is marital consumation, how should it be conclusively effected, and why?
Kisayansi, utata husika tayari uko bayana. Kuna kesi nyingi na hukumu zake zenye kuonyesha vizuri utata huu. Mfano, katika uamuzi wa kesi moja udadacuzi ulikuwa hivi:

The question then becomes… what is meant by the word ‘woman’ in the context of marriage, for I am not concerned to determine the ‘legal sex’ of the respondent at large. Having regards to the essentially heterosexual character of the relationship which is called marriage, the criteria must in my judgment be biological, for even the most extreme degree of transsexualism in a male, or the most severe hormones which can exist in a person with male chromosomes, male gonads and male genitalia cannot reproduce a person who is naturally capable of performing the essential role of a woman in marriage. In other words, law should adopt, in the first place, the first three doctor’s criteria, i.e. the chromosomal, gonadal and genital tests, and if all three are congruent, determine the sex for the purpose of marriage accordingly, and ignore any operative intervention. The real difficulties, of course, will occur if these three criteria are not congruent. The question does not arise in the present case and I must not anticipate, but it would seem to me to follow from what I have said that the greater weight would probably be given to the genital criteria than to the other two…. My conclusion, therefore, is that the Respondent is not a woman for the purpose of marriage but is a biological male and has been so since birth. It follows that the so-called marriage of 10 September 1963 is void.(Corbett v Corbett (1970) 2 WLR 1306, 2 All ER 33; www.pfc.org.uk/caselaw/Corbett%20v%20Corbett.pdf).

Lakini uamuzi wa kesi hii ulipinduliwa katika mahakama ya juu, kwa sababu ya hoja kwamba kuna tofauti kati ya jinsi na jinsia. Udadavuzi ulikuwa hivi:

"Our departure from the Corbett thesis is not a matter of semantics. It stems from a fundamentally different understanding of what is meant by ‘sex’ for marital purposes. The English court apparently felt that sex and gender were disparate phenomena. In a given case there may, of course, be such a difference. A preoperative transsexual is an example of that kind of disharmony, and most experts would be satisfied that the individual should be classified according to biological criteria…. The English court believed, we feel incorrectly, that an anatomical change of genitalia in the case of a transsexual cannot ‘affect her true sex’. Its conclusion was rooted in the premise that ‘true sex’ was required to be ascertained even for marital purposes by biological criteria. In the case of a transsexual following surgery, however, according to the expert testimony presented here, the dual test of anatomy and gender are more significant. On this evidential demonstration, therefore, we are impelled to the conclusion that for marital purposes if the anatomical or genital features of a genuine transsexual are made to conform to the person’s gender, psyche or psychological sex, then identity by sex must be governed by the congruence of these standards." (M.T. vs J.T (1976) 355 A. 2d. 204, 140 NJ Super 77; www.leagle.com/decision/1976217140NJSuper77_1209.xml/M.T.%20v.%20J.T)

Mijadala ya aina hii bado inaendelea ndani na nje ya mahakama. Lakini, Papa Francis anasema kuwa wakati mijadala hiyo ikiendelea, Kanisa halipaswi kuacha mtu yeyote nyuma.

Hivyo Papa aliamua kubuni wazo la "synod on synodality" iliyosindikizwa na tamko la "Fiducia Supplicans."

Kwa ajili ya kufanikisha mikakati hii anahimiza "paradigm shift" miongoni mwa wasaidizi wake. Lakini bado naona anayo kazi kubwa. Bado ukale, mapokeo, umuhimu wa "hazina ya imani" na mambo kama hayo vinatawala.

Lakini, nionavyo mimi, kukumbatia "hazina ya imani" katika namna ambayo inajeruhi maisha ya baadhi ya wanadamu ni kosa kimadili.

Yaani, "promoting a deposit of faith that harms by conceptual and practical exclusion is a machiavellistic and an un-Christian strategy."

Tatizo la kuinua maadili ya ngono na kusahau maadili ya uchumi

Kwa miaka 55 sasa Kanisa katoliki limewekeza sana katika kutafiti na kujadili maadili ya ujinsia wa binadamu na kuwekeza kidogo sana kwenye maadili ya uchumi na siasa. Wenzetu Waislamu wanawekeza sana kwenye uchumi wakati huu. Mfano, ukienda kituo chochote cha mabasi na magari ya masafa marefu kuvuka mikoa ni mali za waislamu, maduka makubwa ni mali ya waislamu.

Aidha, wakati tunamaliza mwaka tayari Waarabu kupitia Kampuni ya Blue Carbon walikuwa wameweka mapatano ya kutwaa asilimia nane ya misitu ya Tanzania. Lakini uvamizi huu hauko Tanzania pekee. Gazeti moj la Kiingereza limeripoti yafuatayo majuzi:

The four MOUs that Blue Carbon has so far signed in Africa cover 20% of Zimbabwe (18 million acres), roughly a tenth of Liberia (2.5 million acres) and Zambia (20 million acres respectively), and 8 percent of Tanzania (20 million acres). The company has also approached another well-forested African country, Angola.

Aidha, tayari Waingereza kupitia kampuni ya Carbon UK (T) Ltd wamefunga mikataba ya kutwaa misitu iliyo katika mbuga sita. Bandari ya Dar imetwaliwa na Shekhe wa Dubai, na kadhalika.

Pia ukosefu wa Katiba ya nchi inayoakisi matakwa ya umma, na inayoiweka Ikulu chini ya Bunge, sasa umeruhusu nchi yetu kuwa koloni la Waarabu wa Dubai. Kuna haja ya kupigania Katiba mpya kwa nguvu zote, muda wote.

Matukio haya yanahitaji uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa akili za watu ili wajue namna ya kuchambua na kupinga unyonyaji unaoendelea.

Mfano, ni Watanzania wachache sana wanaweza kujadili dhana ya "Treaty" na kuonyesha kwanini IGA kati ya Tanzania na Dubai ni tatizo la kimataifa. Lakini bado Makuhani wetu wanaelekeza nguvu kwenye maadili ya jenitalia. Hiki sio kipaumbele sahihi kwa sasa katika Afrika, na SECAM wanapaswa kuamka.

Maswali kwa Askofu NiweMugizi

Kwa ujumla ninajiuliza maswali yafuatayo:
  1. Kuhani anaweza kuogopa kutekeleza majukumu yake kwa sababu tu ya hofu kwamba watu wanaweza kutafsiri matendo yake isivyo? Kama jawabu ni ndiyo, kwa nini kuna undumilakuweili kuhusu baraka kwa wezi wanaofahamika kwa jamii na wazinzi wa jinsia moja?
  2. Kwa nini viongozi wenfi wa Kanisa Katoliki linapenda kufanya uenjilishaji kwa kutumia "mental reservation", kwa maana ya "equivocation" inayohusiana na neno "ushoga", wakati wanajua fika kwamba utaratibu huo unawapotosha waumini kwa kuwafanya wafikirie zaidi juu ya "ulawiti" hata mahali ambapo wanapaswa kuwa wanafikiria juu ya "hali ya kimaumbilie" yaani homosexual condition?
  3. Hizi "irregular situations" zinazowakumba Wakristo na na kuwaweka kwenye "moral dilemmas" ziko Ulaya pekee na hapa Afrika hakuna kwa vile Afrika inayo chanjo dhidi yake?
  4. Ni kifungu gani cha Biblia kinaruhusu baraka kwa "pedicating heterosexual couples" lakini kinakataza baraka kwa "pedicating homosexual couples"?
  5. Sio "utapeli wa kidini" kuwafundisha watu kwamba kitendo cha mwanamke na mwanamume kutumia kingamimba ni tendo la kishoga?
  6. Sio tabia ya "umachiaveli wa kidini" kuwavisha joho la ushoga wakosoaji wa mafundisho tata ya kanisa, tena wakiwa wanafanya hivyo kwa kutumia hoja ambazo zingeweza kujibiwa kwa ushahidi bila kumshambulia mleta hoja?
  7. Sio "ushirikina wa kiteolojia" kuwafundisha watu kwamba kila tendo la ngono inayofanyika kwa kuingiza uume katika uke, kati ya mwanamke na mwanamume ambapo angalau mmoja wao ni mgumba, ni tendo la ngono ambalo ni alama ya uzazi?
  8. Bado fundisho kwamba: "each and every marital act (efficient cause) must of necessity retain its intrinsic relationship to the procreation of human life (final cause)," linabaki na uhalali pale ambapo kuna uhakika wa asilimia zote kwamba yamkini ya kutokea kwa "final cause" inayotjwa ni zero?"
  9. Na je, kwa nini Biblia na Yesu wanaongelea wanawake, wanaume na matowashi lakini ninyi Makuhani mnaongea kana kwamba hawa matowashi hawapo kabisa?
  10. Kwa nini uongozi wa Kanisa Katoliki unapenda sana kuwekeza zaidi kwenye maadili ya jenitalia badala ya kuwekeza zaidi kwenye maadili ya siasa na uchumi?
NIngependa kujua Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu maswali haya. Yeye huwa ni mtu mwenye utayari kujichanganya huku mitandaoni na kwenye jamii pana.

IV. Hitimisho

Kwa ufupi, ni maoni yangu kwamba, tamko la Papa limekuja wakati ambapo baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki mahalia halijajipanga kimtazamo ili kuweza kulitendea haki.

Bado wanaishi kwenye boma la ukale wa teolojia na mapokeo yaliyoasisiwa na Papa Yohane Paul II tangu miaka ya 1968 akiwa bado ni Kardinali wa Krakow, huko Poland. Alifuta upadre na ubatizo wa Padre Gross Sally kwa sababu kwamba alikuwa hunta (intersexual).

Lakini, tayari Papa Francis anaongelea "paradigm shift" ambayo inahitajika katika namna ya kufikiri, kuhukumu na kutenda ndani na nje ya Kanisa Katoliki, kwa kusoma alama za nyakati tukiwa tumevaa miwani ya sayansi, tekinolojia, teolojia na falsafa bila kubagua nyenzo yoyote kati ya hizi.

Kwenye sekta ya elimu tunasema kwamba "if one wants to teach a donkey anything, one must be more knowledgeable than the donkey." Wanafaksafa wanasema "out of nothing comes nothing," kwa maana kwamba, "we can not give what we do not have."

Katika suala la sasa, busara hizi maana yake ni kwamba kuhani aliye mtumwa ndani ya boma la ukale wa teolojia na mapokeo hawezi kutakatifuza ulimwengu wa wanasayansi mamboleo kwa ufanisi. Sababu ni kwamba "ombwe huzaa ombwe" na "mtu hawezi kutoa kitu asicho nacho."

Hivyo "paradigm shift" ndani na nje ya Kanisa Katoliki ni lazima, ikiwa inaambatana na "reparation" kwa wale wote ambao baadhi ya viongozi wa Kanisa wamewajeruhi kwa kutumia mbinu za kimachiaveli pasipo uhalali wowote, hata kama waathirika wameshakufa.

Bila hivyo kuna sababu ya kutangaza ugomvi wa kudumu dhidi ya makuhani wote ambao ni wafuasi wa Nicollo Machiavelli, kwa sababu ya wao kufikiri kuwa inawezekana kuwanyamazisha watu wote, siku zote na sehemu zote kwa kutumia mbinu haramu kama vilr kuwavisha joho la ushoga bila kujali kwamba ni mashoga au hapana.

Itikadi hii haikubaliki kwa Yesu, kwa Mtume Paulo na kwa Wakristo makini.

V. Pendekezo

Ni muhimu hapa kuweka bayana kwamba, swali juu ya ndoa ya mke na mume ni kitu gani na ndoa ya mke na mume sio kitu gani linahitaji kujibiwa kirazini zaidi kuliko kunukuu misahafu, maana hii ni taasisi inayovuka mipaka ya kidini.

Tangu enzi za Fr. Gregor Mendel maneno "mwanamume" na "mwanamke" yamepata maana pana zaidi kuliko ilivyokuwa enzi za Biblia. Na sasa kisheria maneno "legal sex" yamepata fasili mpya inayohitaji maelezo ya kisayansi yasiyo kwenye Biblia.

Nguvu kubwa ya kifkra inapaswa kuelekezwa huku. Hii tabia ya baadhi ya Maaskofu kupewa air-time katika luninga ya Taifa (TBC) na kisha kutumia nafasi hiyo kuhubiri chuki badala ya upendo unaoambatana na kutoa elimu makini hapana. Mungu hapendi uinjilishaji unaotumia mbinu za kimachiaveli.

VI. Kanusho/Disclaimer

Napenda ifahamike kuwa sitafuti maslahi binafsi katika andiko hili. Yaani sitafuti kuombewa kwa sababu mbili. Mosi, mie sina tatizo la uhomofilia. Pili, hata kama ningekuwa nalo, nafahamu kuwa baraka ni sala, na siamini katika miujiza itokanayo na sala. Hivyo, bado nisingelikuwa na sababu ya kutaka yeyote aniombee kwa sababu hii.

Badala yake naandika haya kwa kusukumwa na mambo mawili. Mosi, ninaamini katika jamii inayoheshimu usawaziko wa haki (a just society), bila kujali vigezo vya kinasibu vinavyotamkwa na watawala, bila kuzingatia misingi ya kimaumbile.

Matowashi, mashoga, mashosti, watu wenye jinsi-pindu (intersexuals/mahunta) na watu wenye jinsia-pindu (transgenders) ni binadamu wenye haki ya kuishi kama binadamu baki kwa mujibu wa maumbile yao kama binadamu.

Na pili, ni dhamira yangu ya kukuza na kuhami tunu ya urazini ndani na nje ya Kanisa Katoliki. Kuna juhudi za kuwaburuza waumini zinafanyika kwa kutumia kigezo cha "Baba Askofu Kasema" hata pale anaposema "kauli zenye ukakasi na zisizo na ushahidi," kama vile kauli kwamba "baadhi ya binadamu ni uchafu katika jamii," na hivyo kuchochea chuki dhidi yao, jambo ambalo ni kosa la jinai.

Adolf Htler alikuwa mwansiasa aliyekuwa na jeuri ya aina hii. Na sasa tunashuhudia jeuri kuu, inayotokana na ulevi wa madaraka ya kdini, na isiyokubaliana na kanuni ya hadhi ya utu.

Lazima waumini makini kupaza sauti za kupinga uhuni huu, na hasa unapofanyika kwenye altare ya ibada takatifu tena kwa kutumia luninga ya Taifa (TBC).

Kwa kuzingatia mantiki hii, Maaskofu na makasisi wote wenye fikra za kufanya uinjilishaji kwa kutumia matusi, uwongo na mbinu baki za kimachiaveli, ni wahuni wanaojificha kwenye majoho ya kikuhani.

Hawana tofauti yoyote na panya-road wanaovaa suti. KImsingi, kuhani anayehubiri kwamba mashoga, mahunta na matowoashi ni "uchafu" katika jamii ni panya-road wa daraja la juu, maana yeye anavalia joho la kikuhani badala ya koti la kawaida. Ni afadhali ya Hitler aliyekuwa mhuni anayevaa magwanda ya kijeshi.

MWISHO.

Uchambuzi huu umeandaliwa na:

Mama Amon,
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu,
Dawati la Utafiti la Mama Amoni (DUMA),
SLP P/Bag
"Sumbawanga"
Tanzania.
 
Baadhi ya maelezo yaliyo katika waraka yanaonekana yana mtego fulani, kwa sababu baada ya kutolewa kwa huo waraka tayari watu walianza kufurika kwa mapadre kwenda kuomba baraka na wakiwa wameshikana mikono. Hali hii inaleta kikwazo fulani.

Hivyo, tutulie na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania muda si mrefu litatoa pia tamko au msimamo kuhusiana na waraka huu....
Maaskofu muwe wapole tu, anzeni kubariki mashoga. Hakunaga mpango wa mzungu unapanguliwa na mwafrika.

Chanjo ya korona wananchi na rais wa nchi waliapa kwamba hakuna chanjo itakanyaga hapa. Lkn mwisho wa siku chanjo ya mzungu ikafika.

Hata mashoga ni suala la muda tu. Watafunga ndoa na kubarikiwa kabisa kanisa katoliki na makanisa mengine.

TEC wakijichanganya tu kwenye tamko lao maaskofu wote watafutwa kazi. Ikumbukwe kuwa kanisa katoliki duniani kote linatii amri toka Roma. Ndiyo maana ya msemo "Roma lucuta causa finito"
 
Bado wanaendelea kutupigia kelele wakati wanajua fikra Hilo agizo watakuja litimiza taka wasitake waache kutuchora hawa Binadamu wenzetu wanaojiona watakatifu!!
 
Bado wanaendelea kutupigia kelele wakati wanajua fikra Hilo agizo watakuja litimiza taka wasitake waache kutuchora hawa Binadamu wenzetu wanaojiona watakatifu!!
Mm nashangaa. Ushoga wafanye wengine halafu kelele wao. Cha msingi watoe ubarikio watu waendelee kusagana.

Mbona yule afande wa Zanzibar hawakumkemea? Au huyo afande Dometira aliyekodi majambazi yaue mumewe ili aendelee kusagana. Mbona hawajamkemea
 
Africa imegomea uchafu huo.

Mpasuko ni muhimu sana Kwa wakati huu Ili Kondoo na mbuzi watambulike.

Amen
 
Mm nashangaa. Ushoga wafanye wengine halafu kelele wao. Cha msingi watoe ubarikio watu waendelee kusagana.

Mbona yule afande wa Zanzibar hawakumkemea? Au huyo afande Dometira aliyekodi majambazi yaue mumewe ili aendelee kusagana. Mbona hawajamkemea
Ni swala la MDA tuu Hilo waliloagizwa lazima walitimize tena wanavyolizungumza kila wakati ndio wanalipa nguvu na promo ya kutosha na kitu kikishazoeleka kusikika mara Kwa mara masikioni Mwa watu kwenye kutenda huwaga ni rahisi mnoo,,litakujaonekana ni swala la kawaida tuu na hawa ndio wanaotumiwa kulizoesha masikioni Mwa Watu kwa kulisema sema kila wakati na ndio watakao kuja kuwa wa Kwanza kulifanyia kazi ni kheri wangekaa kimya,,na naamini walishakubaliana kabla sasa wanajaribu kucheki upepo uko Vipi katika mapokeo ya wafuasi wao.
 
Africa imegomea uchafu huo.

Mpasuko ni muhimu sana Kwa wakati huu Ili Kondoo na mbuzi watambulike.

Amen
Mkijitenga mtatengeneza makanisa mawili makubwa:- Katoliki ya waafrika na Katoliki ya wazungu..

Katoliki ya waafrika itakufa kwa kuendelea kugawanyika mpk kutakuwa na Katoliki ya mtu binafsi. Hii ni kwasabb waafrika ni wabinafsi sana.
 
Mkijitenga mtatengeneza makanisa mawili makubwa:- Katoliki ya waafrika na Katoliki ya wazungu..

Katoliki ya waafrika itakufa kwa kuendelea kugawanyika mpk mtakauwa na Katoliki ya mtu binafsi. Hii ni kwasabb waafrika ni wabinafsi sana.
Hata Katoliki ikifa IMANI ITAENDELEA kuwepo.

Yesu: Nijapo nitaikuta IMANI?

Afrika imegoma kuhalalisha Abomination!!

Mungu ibariki Afrika. Amen
 
Hata Katoliki ikifa IMANI ITAENDELEA kuwepo.

Yesu: Nijapo nitaikuta IMANI?

Afrika imegoma kuhalalisha Abomination!!

Mungu ibariki Afrika. Amen
Afrika ipi hiyo. Hii yenye kila aina ya uovu? Ubinafsi, uzandiki, ufisadi, mauaji na uporaji?
 
Afrika ipi hiyo. Hii yenye kila aina ya uovu? Ubinafsi, uzandiki, ufisadi, mauaji na uporaji?
Hiyo hiyo.

Saa mbovu Huwa inasema Kweli sometimes.

Afrika ni makimbilio Kwa mataifa yote Kwa Kila kitu, utajili, USALAMA, chakula nk nk.

Watakuja kujifunza kuwa NDOA ni kati Ya Mwanaume na Mwanamke pekee.

Amen
 
View attachment 2860422
View attachment 2860423
I. Utangulizi

Askofu Severine NiweMugizi ni miongoni mwa Maaskofu wa Kanisa Katoliki machachari sana. Hataki kulala na dukuduku moyoni mwake hata siku moja.

Hivyo, salamu zake za Krismas ya 2023 ziliambatana na maoni yake binafsi kuhusu tamko liitwalo "Fiducia Supplicans" lililotolewa na Papa Francis, hapo 18 Desemba 2023.

Hapa chini nafupisha salama za Askofu NiweMugizi kwa ujumla na kisha kufupisha mawazo yake kuhusu tamko hili. Kuna maswali na tafakari inafuata.

II. Muhtasari wa salamu za Askofu NiweMugizi

Naitwa Severine NiweMugizi, kwa neema ya Mungu tu, Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara. Naomba nikuletee salam na ujumbe wa Krismasi ya 2023....

Mpendwa msikilizaji tunaalikwa kumkubali mtoto Yesu azaliwe mioyoni mwetu. Aiguse mioyo yetu ibadilike kuwa mioyo safi. Atuguse tuwajibike inavyopasa....

Tumuombe atuguse tuache dhambi, uhasama, visasi, uvivu, uzembe, utapeli wa aina mbalimbali...

Tunaadhimisha Krismas hii pia baada ya Baba Mtakatifu, Fransis, kuridhia waraka uitwao "Fiducia Supplicans" yaani "Supplicating Trust."

Hili ni tamko kuhusu fundisho la Kikatoliki lililochapishwa mwezi huu, Desemba, na Dikasteri au Idara inayohusika na mafundisho ya imani ya Kikatoliki. Ujumbe wa Waraka umezua taharuki ndani na nje ya Kanisa Katoliki.

Sababu ni maagizo ya Papa yasemayo kwamba maaskofu na mapadre wanalo jukumu la kubariki watu walio katika miungano isiyo ndoa halali ikiwa ni pamoja na miungano ya wale watu wa jinsia moja, yaani mashoga na wasagaji.

Hasa dhamira za watu zimejeruhika kwa sababu ya tamko hilo na kumekuwepo na mlipuko wa mijadala kuhusu hilo...

Msimamo wa Kanisa katika mafundisho ya msingi ya imani na maadili hauwezi kubadilishwa na mtu mmoja. Papa peke yake hana mamlaka ya kubadilisha mafundisho hayo, kama hayuko katika ushirika kamili na maaskofu wenzake.

Ufunuo wa maandiko matakatifu unaweka wazi kwamba ndoa ni muungano kati ya mwanamume na mwanamke. Na Yesu amesema wazi hasa ukisoma enjili ya Mathayo sura ya 19...

Nitaje hapa, kama mchungaji wa Kanisa, Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara, baraka ziombwazo na watu wa jinsia moja wanaokuja pamoja na wanafahamika kuwa mashoga au wasagaji ni marufuku kwa mapadre kuzitoa jimboni Rulenge Ngara.

Amri hii inatolewa kwa sababu kwa sura ya nje baraka hiyo inaweza kutafsirika kuwa ni kuwathibitisha na kuwaombea waendelee na wastawi katika muungano huo ambao ni dhambi.

Hali hii itakuwa kinyume na Kristo na kikwazo kwa jamii ya waamini na hasa ukifanyika hadharani.

Nirudie tena kusema, kama waraka ulivyotambua wale watu wa jinsia moja wanaokuja kanisani hawawezi kufukuzwa. Ni wana wa Mungu kwa vyovyote. Na hao wakija kuomba kufanya kitubio watabarikiwa ili waungame na kuacha muungano ulio dhambi. Huo ndio msimamo halisi.

Baadhi ya maelezo yaliyo katika waraka yanaonekana yana mtego fulani, kwa sababu baada ya kutolewa kwa huo waraka tayari watu walianza kufurika kwa mapadre kwenda kuomba baraka na wakiwa wameshikana mikono. Hali hii inaleta kikwazo fulani.

Hivyo, tutulie na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania muda si mrefu litatoa pia tamko au msimamo kuhusiana na waraka huu....


III. Maswali yanayoibuka kutokana na salamu hizi

Kwa sehemu kubwa salamu hizi hazina tatizo. Tamko la Papa halijatengua mafundisho rasmi ya Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni kitu gani na sio kitu gani.

Tatizo liko kwenye agizo la Papa Francis kwamba maaskofu na mapadre wanalo jukumu la kubariki watu walio katika miungano isiyo ndoa halali ikiwa ni pamoja na miungano ya wale watu wa jinsia moja, yaani mashoga na wasagaji.

Askofu NiweMugizi amekaidi agizo la Papa kwa hoja kwamba ni agizo haramu kwa mujibu wa maandiko matakatifu. Askofu NiweMugizi ni mtalam wa sheria za Kanisa.

Anajua vema kwamba sheria za Kanisa zinatofautisha kati ya mawazo yafuatayo: "ratification," "consumation," "blessing," "marital act," na mawazo baki kama haya.

Katika mipaka ya misamiati hii Tamko la Papa Francis halijakiuka sheria za Kanisa. Ni agizo halali, na ukaidi wa Askofu NiweMugizi ni haramu inayistahili adhabu ya kiutawala.

Baraka anazoziongelea Papa Francis hazina tofauti na zile zinazotolewa kwa wezi waliokiri hadharani kwamba wameiba, na hawajarudisha walichokiiba. Wanufaika wa ESCROW ni mfano hai. Mpaka leo tunawaona Kanisani wakipokea baraka.

Hivyo, ufafanuzi wa Askofu NiweMugizi unaibua maswali yafuatayo: Kasisi anaweza kuogopa kutekeleza majukumu yake kwa sababu tu ya hofu kwamba watu wanaweza kutafsiri matendo yake isivyo? Kama jawabu ni ndiyo, kwa nini kuna undumilakuweili kuhusu baraka kwa wezi wanaofahamika kwa jamii na wazinzi wa jinsia moja?

Lakini pia, kuna tatizo la kisemantiki na kiepistemolojia. Kanisa Katoliki linamaanisha nini linapotumia neno "ushoga"? Na linatumia utaratibu gani kuwatambua mashoga na wasagaji?

Kuna matukio kadhaa yanaonyesha kwamba, ndani ya Kanisa Katoliki, neno "ushoga" linatumika kama silaha ya propaganda dhidi ya wakosoaji wa baadhi ya misimamo tata ya kanisa tena wakati mwingine dhidi ya watu wasio na hatia. Mifano ipo.

Kifo cha Rodney Mutie Mengi mwaka 2005 kilizua mvutano kati ya Kanisa Katoliki na Reginald Mengi, mzazi wa Rodney.

Mengi aliweka bayana kwamba mwanaye alikufa kwa UKIMWI, hivyo akahimiza watu kuwa waaminifu au kuwa waangalifu kwa kujikinga kwa kutumia kondomu. Miongoni mwa watu walio mjibu tena kwa maandishi kupitia gazeti la Rai, kama sikosei, ni Askofu NiweMugizi.

Gazeti la Kiongozi likaunga mkono pilika kwa kuchapisha bahari "Serikali Ikemee Ushoga." Askofu KIlaini akawaita Maparoko wote wa Dar na kuwapa orodha ya watu ambao anaona kuwa ama ni manabii wa "ushoga" au mashoga kabisa, kwa sababu tu kwamba wanaandika kuhusu matumizi ya kondomu kama kingamagonjwa na/au kingamimba.

Picha kubwa inayozaliwa hapa ni kwamba mapenzi ya jenitalia kwa jenitalia yanayofanyika kwa kutumia kingamimba kama vile kondomu ni tendo la kishoga. Watu ambao sio mashoga wanaweza kufanya tendo la kishoga kweli? Hapana!

Lakini shida kubwa zaidi ni kwamba, maelezo mengi ya makasisi wetu, akiwemo Askofu Ruwaichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, hayatofautishi kati ya "homo-affective condition" na "homosexual acts."

Mkanganyiko huu umeenezwa mpaka ngazi ya ndoa kupitia mafundisho ya ndoa. Wakati wa mafundishi ya wanandoa, maparoko wengi wanawambia "wanafunzi wao" kwamba "ni mwiko kwa wanandoa kufanya tendo la kishoga," yaani ulawiti, utadhani kwamba mashoga wote wanafanya ulawiti.

Kwa njia hii wanawavisha miwani ya kishoga na wao kuanza kuitazama dunia kwa kutumia miwani hiyo. Miwani hii ni tatizo la kijamii maana inawaonyesha "ushoga" hewa.

Sababu ni kwamba, maparoko hawa wanasahau kuwa sio kila ulawiti ni tendo la kishoga na kwamba tendo la ulawiti kati ya mwanamke na mwanamume sio, na haliwezi kuwa, tendo la kishoga.

Kuna janga la kisemantiki ndani na nje ya Kanisa Katoliki. Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu tatizo hili?

Kiepistemolojia pia kuna tatizo kubwa. Kuna waseminari kadhaa huko seminari kuu wamekuwa wakiachishwa masomo kwa sababu ya madai kwamba wana "vidole vya kishoga."

Yaani wanatumia "second to fourth digit ratio (2D:4D ratio)," mbinu ambayo haikubaliki kisayansi. Nimewashuhudia Padre Kaombe, hayati Profesa Kanywanyi, na wtu baki wakitumia mbinu hii pia.

Kuna makruta waliwahi kufukuzwa kwa kutumia kigezo hiki pia. Kuna dalili kwamba "mafundisho tata ya KIkatoliki kuhusu namna ya kuutambua ushoga" yalikuwa na mchango hapa pia. Hili ni janga la kiepistemolojia. Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu tatizo hili?

Kwa ujumla ninajiuliza: Sio "utapeli" wa kidini kuwaaminisha watu kwamba kutumia kingamimba ni tendo la kishoga? Sio umachiaveli kuwavisha joho la ushoga wakosoaji wa kanisa, tena kwa kutumia hoja ambazi zingeweza kujibiwa bila kumshambulia mleta hoja? NIngependa kujua Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu maswali haya.

IV. Hitimisho

Kwa ufupi, ni maoni yangu kwamba, tamko la Papa limekuja wakati ambapo Kanisa Katoliki mahalia halijajipanga kimtazamo ili kuweza kulitendea haki.

Papa anaongelea "paradigm shift" ambayo inahitajika katika namna ya kufikiri, kuhukumu na kutenda ndani na nje ya Kanisa Katoliki, kwa kusoma alama za nyakati tukiwa tumevaa miwani ya sayansi, teolojia na falsafa bila kubagua nyenzo yoyote kati ya hizi.

Kwenye sekta ya elimu tunasema kwamba "if one wants to teach a donkey, one must be more knowldheable than a donkey."

Katika suala la sasa, ni kwamba mtu aliye mtumwa ndani ya boma na maarifa ya sanaa na teolojia hawezi kutakatifuza ulimwengu wa sayansi kwa ufanisi.

Hivyo "paradigm shift" ndani na nje ya Kanisa Katoliki ni lazima, ikiwa inaambatana na "reconciliation" kwa wale wote ambao baadhi ya viongozi wa Kanisa wamewajeruhi kwa kutumia mbinu za kimachiaveli pasipo uhalali wowote.

Kuna sababu ya kutangaza ugomvi wa kudumu na watu kama Askofu Kilaini kwa sababu hii: Hwa ni maaskofu ambao ni wafuasi wa Nicollo Machiavelli, kwa sababu ya kufikiri kuwa inawezekana kuwanyamazisha watu wote, siku zote na sehemu zote kwa kutumia mbinu haramu ya kuwavisha joho la ushoga bila kujali kwamba ni mashoga au hapana. Haiwezekani.

V. Pendekezo

Ni muhimu hapa kuweka bayana kwamba, swali juu ya ndoa ya mke na mume ni kitu gani na ndoa ndoa ya mke na mume sio kitu gani linahitaji kujibiwa kirazini zaidi kuliko kunukuu misahafu, maana hii ni taasisi inayovuka mipaka ya kidini. Napendekeza kwamba fasili ifuatayo inakubalika kwa wengi na hivyo ifafanuliwe kila mara, kila wakati na kila mtu:

"Heterosexual marriage is a communion of persons which is ratified in public under an oath to live together alone for life, and then consummated and regularly actualized by sexual acts which are simultaneously unitive in significance and procreative in significance, regardless of whether they are procreative in effect or otherwise."

Fasili hii ikishakueleweka ndio hapo sasa tuanze kutenga muda wa kujadili "the impossibility of homosexual marriage" kwa kutumia fasili hii kama msingi wa majadiliano. Vinginevyo naona kwamba tunatapatapa.
Shoga huyo. Very articulate. Nit picking on technicalities, cutting corners, mincing words, essentially to confuse. Shoga huyo.
 
Shoga huyo. Very articulate. Nit picking on technicalities, cutting corners, mincing words, essentially to confuse. Shoga huyo.

Majibu "very articulate" kwa porojo za Askofu LGF: Umachiaveli hapana, utapeli wa kidini hapana, ukweli wa kisayansi sawa!

1704254894201.png

Padre Gregor Mendel mwasisi wa sayansi ya msimbonasaba (genetics)!

God, the author of truth, Pope Francis, the guardian of truth, and Padre Gregor Mendel, the father of truth about human genetics, are not happy with the rubbish-minded Catholic Bishop who has introduced himself as LGF because he defecates by passing stinking feces through both terminals of his alimentary canal, namely, through his mouth and through his anus.

Refuting Bishop LGF's lies artistically


Makengeza wapo wa kuzaliwa, mfano Suleimani Kova
Mashoto wapo wa kuzaliwa, mfano Baraka Obama
Mazeruzeru wapo wa kuzaliwa, Mfano Haji Manara
Matowashi wapo wa kuzaliwa, Mfano Paul Makonda
Mahunta wapo wa kuzaliwa, mfano Mwamba Nyanda

Mashoga wapo wa kuzaliwa, mfano James Delicious

Ushoga na Uanaume ni maumbile yasiyochaguliwa
Ulawiti na Ubakaji ni tabia za kujitakia
Ushoga sio ulawiti na ulawiti sio ushoga
Uanaume sio ubakaji na ubakaji sio uanaume
Maumbile huzaa tabia inayoweza kukataliwa na mhusika

Shoga mwizi anaadhibiwa kwa kosa la wizi pekee

Shoga jambazi anaadhibiwa kwa kosa la ujambazi pekee
Shoga mlawiti anaadhibiwa kwa kosa la ulawiti pekee
Ushoga sio wizi, sio ujambazi, sio ulawiti, sio tabia, sio dhambi, sio jinai
Ushoga ni maumbile ya kibayolojia.

Papa Yohanne Paul II aliupinga ukweli huu kwa sehemu kubwa!
Wafuasi wa teolojia ya kishirikina wanaupinga ukweli huu!
Makasisi mateka wa ungwini
wanaupinga ukweli huu!
Mateka wa Krepkian dogmatism wanaupinga ukweli huu!
Papa Francis anawapinga hawa wanaopinga ukweli huu!


Mateka wa umachiavelli hawa!
Wanafiki wakubwa hawa!
Waongo wakubwa hawa
II!
Matapeli wa kidini hawa!
Wazembe wa kutafsiri misahafu hawa!

Katiba na sheria za nchi hekalu la raia wote
Ni hekalu la raia maheterofilia (heterosexuals)
Ni hekalu la raia mahomofilia (homosexuals)
Ni hekalu la raia mahunta yaani watu wenye "jenitalia mseto" (intersexuals)

Ni hekalu la raia wenye "jinsia-pindu" (transgenders).


Maaskofu na makasisi wanasayansi hoyee!
Padre Gregor Mendel na wenzake hoyee!
Utafiti na ukweli wa kisayansi hoyee!

Papa Francis na ma-Jesuit wenzake hoyee!
Mwongozo wa Fiducia Suplicans hoyee!


Rebutting Bishop LGF's claims technically

Contrary to what Bishop LGF wrongly thinks, "nit picking on technicalities, cutting corners, mincing words," is the surest way, not "to confuse" the audience, but to bring about conceptual clarity, in a way that demarcates truth from falsehood.

Here is the philosophical reasoning that explains why: There are four areas of communicative activity in which argumentation plays a role.

First, we have private argumentation, taking place in everyday life among all sorts of people: we argue with our family and friends, but also on occasion with strangers we meet by chance or in the course of our daily activities, such as shopping, asking for directions, riding on public means of transport, and so on.

Then, we have public argumentation. This is the realm of democratic discussion, in canvassing, political meetings, or in the mass media or increasingly in the social media.

Further, we have
professional argumentation, done by lawyers in court or with a client, by physicians among themselves (e.g., in differential diagnosis or ‘doing the rounds’ in a hospital) or with a patient, by architects, engineers, administrators, managers, and so on in construction sites, business meetings, and whatnot.

Finally, we have
academic argumentation, that takes place in universities, colleges, research institutes, scientific conferences, laboratories, and so on.

The agenda of "Fiducia Supplicans" can and should be discussed intelligibly at an academic argumentation level and not otherwise.

A discussion on the issues surrounding the lives of couples living in irregular situations, as a result of disorders of sexual development (DSD), for example, is a discussion on heterosexuality and non-heterosexuality (homosexuality, intersexuality, and transgenderism) in relation to moral, civil and canon laws. These are technical issues.

And this is where nit picking on technicalities, cutting corners, and mincing words come in. No alternative, except if some one prefers vagueness as a strategy to confuse the audience.

Specifically, if my taxonomy of communicative activities is correct, then there is no real problem of "nit picking on technicalities, cutting corners, mincing words, essentially to confuse," at least insofar as the applied philosophy of argumentation I have studied is concerned.

Instead, there is a problem of avoiding "technicalities, cutting corners, mincing words" by using an evil strategy of "mental reservation," also known as “the doctrine of equivocation,” which allows one to knowingly mislead people, allegedly, “without being guilty of lying.”

This catholic principle distinguishes between the following two definitions of “lying”: On one hand, “to lie is to speak or act against the truth in order to lead someone into error.” Let us call this the first definition of lying.

And on the other hand, “to lie is to speak or act against the truth in order to lead into error someone who has the right to know the truth.” Let us call this the second definition of lying.

The general catholic teaching about “mental reservation” is that you are not permitted to tell a lie, as understood in terms of the second definition, but you are permitted to tell a lie, as understood in terms of the first definition.

To do this, you simply use an ambiguous expression realizing that the person who you are talking to will accept an untrue version of a statement, while foreseeing and permitting that to happen without directly intending it to happened, as the latter would be lying, as understood in terms of the second definition. For me, this is a typical case of machiavellism.

And generally, the third millennium in which we live now, and which is mainly guided by a scientific outlook, aided by modern information analysis and evaluation skills, does not have a room for such a machiavellistic strategy.

Specifically, according to the scientific outlook which emerged in the 18th century, the modern world is mainly governed by a philosophy according to which:

  1. Statements of facts, as opposed to statements of values, should be based on observation, not on unsupported and sectarian authority (argument from subjective authority);
  2. The inanimate world is a self-perpetuating system in which all changes conform to natural laws, as opposed to supernaturally revealed laws;
  3. The earth is not the center of the universe; and
  4. The concept of "teleological cause," as opposed to "efficient cause," is a concept which is scientifically useless.
Systematically framing the dark side of Bishop LGF

Bishop LGF is a typical primitive, naive, demented, foolish and ignorant devotee of Machiavellian ideology of anathematism, which is a coercive method of evangelization, akin to the scandal of the first century Islamisation by sword.

He publishes criminal false statements that are damaging to personal reputation, being defamatory written statements (libel) which reproduce his oral defamatory statements that he made ten years ago (slander), as he waged unwarranted wars against critical Catholic believers in Dar Es Salaam Arch-Diocese.

He is a criminogenic Bishop just as the late Bishop Balina was and Bishop Mtega has been, all of these now casting a serious doubt on the integrity and moral authority of the Tanzania Episcopal Conference (TEC).

Bishop Balina was an expert of organised theft, which targeted church property and finance, while Bishop Mtega is a womanizer who used to forcibly having sex with nuns as a precondition to their taking of perpetual vows, which he would later preside over as their Bishop and covert polygamist husband.

The Vatican forced Bishop Mtega to resign because of this sexual scandal after it was covertly recorded by one nun and sent to the Pope.

However, TEC protected and sided with Bishop Balina, the fact which forced Dr. Wilbrod Slaa, the then TEC Secretary General, to resign from office. Balina remained a part of TEC team until his death.


Bishop LGF strongly believes that a pursuit of good religious ends may justify the application of the evil means of Machiavellian stigmatization by anathematizing the other.

He is a very articulate and compulsive liar who deceptively dodges scientific and philosophical technical arguments, and machiavellistically attacks personalities instead of addressing their arguments.

He equivocates on the words "God's Will" without specifying "God's will for who and about what", essentially to mislead the incompetent audiences who do not know any distinction between rhetorical appeals and logical appeals.

He is a typical primitive, naive, ignorant and hooliganistic Bishop who scored an "F" at form four in life science and accidentally became the promoter of theological science, namely, the Gospel of life.

For this reason he does not comprehend the essential difference between "pre-fertilisation gametic life," and "post-fertilization somatic life."

For him, there is no any biological difference between a sperm and an embryo. He wrongly equates spermicide and abortion, whereas in fact, abortional "contra-life will" is direct "contra-life will" with respect to "somatic life" while contraceptive "contra-life will" is a direct "contra-life will" with respect to "gametic life," and an indirect "contra-life will" with respect to "somatic life."

From such equivocations poor Bishop LGF fails to distinguish between gametic life as an instrumental good and somatic life as a basic good, and hence, confusedly and illicitly concludes that contraception is contra-life, and therefore, intrinsically evil, meaning that it is morally wrong everywhere, every time and for every copulating pair.

No cognitive booster will assist poor bishop LGF to understand that contraception is a contra-fertilisation act and hence an indirect contra-life act with respect to somatic life. As such he does not see the truth that, the doctrine of double effect allows one to indirectly pursue contraceptive "contra-life will" without being morally blameworthy of pursuing abortional "contra-life will".

In short, he equivocates on the term "life" which means both pre-fertilization gametic life and post-fertilization somatic life. He cannot comprehend the biological steps entailed by fertilization, and the ontological transformation that they necessarily bring about.

He denies the following claims: that, in successful fertilization, also known as conception, various steps are involved, namely, the union of sperm and egg in one of the fallopian tubes to form a zygote; that, the zygote travels down the fallopian tube, where it becomes a morula; that, once it reaches the uterus, the morula becomes a blastocyst; and that, finally, the blastocyst then burrows into the uterine wall, a process called implantation.

He abhors the technical biological narrative according to which, during fertilization, also known as conception, the sperm and egg fuse to form a zygote, kick-starting the development of a new individual with a unique combination of genetic traits, where, this remarkable process marks the beginning of new concrete human life in sexually reproducing organisms.

He hates the claim that, fertilization, also known as conception, is the process which occurs in the fallopian tube, where, for successful fertilization, various steps are involved, including the acrosomal reaction, cortical reaction, sperm entry, karyogamy, and activation of eggs.

So, for him it is a wastage of time to talk about the following technical biological processes: acrosomal reaction, cortical reaction, sperm Entry, karyogamy, and eggs activation.

He trembles when he hears about "acrosomal Reaction," a process where, the acrosome, a cap-like structure in the sperm, releases enzymes upon contact with the egg's zona pellucida, to help the sperm penetrate the protective layer surrounding the egg;

He quivers when he hears about "cortical Reaction," a process whereupon, after sperm penetration, the egg's cortical granules release enzymes that harden the zona pellucida, preventing other sperm from entering, to ensure only one sperm fertilizes the egg, avoiding genetic complications;

He tremors when he hears about "sperm Entry," a process whereby, once the sperm fuses with the egg, it sheds its tail and other unnecessary parts while the sperm's genetic material combines with the egg's genetic material, forming a single-cell zygote;

He shakes when he hears about "Karyogamy," a process where, the pronuclei from the sperm and egg merge, resulting in the complete genetic blueprint of the new individual, so that, the zygote is now ready for cell division and further development; and

And he palpitates when he hears about "eggs activation ," a process whereby, various metabolic changes are triggered in the egg, preparing it for embryonic growth, such that, the egg starts the process of mitosis and cellular differentiation, ultimately leading to the formation of an embryo.

Worse still, he embraces fallacious reasoning every now and then. His mind is driven by an axiom according to which plausibility necessarily implies validity, which is a philosophy that underpins the Machiavellian ideology of social constructionism.

He wrongly believes that his priestly ordination bestowed on him an ontological transformation that allowed him to attain omni-competence that makes him capable of miraculously transcending the natural cognitive closure which characterizes the cognitive limits of social scientists, as opposed to natural scientists, in light of their respective professional training in their relevant academic disciplines.

For all these reasons, he is now a demented, ignorant, foolish expert of sanitizing church history which is bloated with blood and bones of witches and non-heterosexuals who were burnt alive during the inquisition as ordered by the then foolish Pope, all these being crimes against humanity.

The Catholic Bishop LGF is a national prophet and coordinator of the crime of "organised ignorance" against innocent African children who are enrolled by him and subjected to coercive cathechetical classes, which are full of contradictory doctrines, and which are thus necessarily false, meaning that he denigrates their human dignity, simply because these African kids can neither say no nor distinguish between truth and falsehood.

He forcibly wants the kids to swallow "the modalism paradoxes," which state that, each of the following set of contradictory claims must be accepted as true: "The Father is God; The Son is God; Thus, the Father is the Son; and The Father is not the Son"; and "The Father is God; The the Holy Spirit God; Thus, the Father is the Holy Spirit, The Father is not the Holy Spirit."

He coercively wants the kids to swallow "the tri-theism paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "The Father is God and the Son is God and the Holy Spirit is God; Each of the persons is distinct from the other persons; Thus, there are three Gods; There is exactly one God."

He violently wants the kids to swallow "the tetratheism paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "The Trinity is God, the Father is God, the Son is God and the Holy Spirit is God; The Trinity and each of the persons is distinct from the others; Thus, there are four Gods; There is exactly one God."

He oppressively wants the kids to swallow "the subordination paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "The Father is the source of the Son; The Father is always older than the Son; Thus, the Father is not identical to the Son; The three persons in the Trinity are identical."

He brutally wants the kids to swallow "the procession paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "God is not begotten; The Son is God; Thus, the Son is not begotten; The Son is begotten."

He harshly wants the kids to swallow "the Self-creation paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "The Father is God; The Son is God; The Father is the source of the Son; Thus, God creates God."

He tyrannically wants the kids to swallow "the divine triunity paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "God is triune; The Son is not triune; Thus, the son is not God; The Son is God" and "God is triune; The Father is not triune; Thus, The Father is not God; The Son is God" and "God is triune; The Holy Spirit is not triune; Thus, The Holy Spirit is not God; The Son is God."

And he superstitiously wants the African kids to swallow "the transubstantiation paradox," which state that, each of the following sets of contradictory claims must be accepted as true: "A body is anything which has weight and exclusively occupies space by reason of its property of impenetrability; According to the property of impenetrability no to bodies can occupy the same space at the same time; At incarnation Jesus assumed a human body which he possesses until now; During the holy mass the process of consecration allows the body of Jesus to occupy the same space which is simultaneously occupied by bread and wine in the alter cups."

Only sheep-minded Christian parents can allow their innocent children to be followers of this Machiavellian, demented, ignorant, foolish Catholic Bishop, who defecates by passing stinking feces through both terminals of his alimentary canal, namely, through his mouth and through his anus.


Pictorially framing the dark side of Bishop LGF

Pictures below say more about the discoveries based on this outlook, so as to remind some of our Bishops that Africa is neither immune from genetic disorders of sexual development (DSD) nor free from lifestyles engulfed in persistent moral dilemmas.


Mr. Gross Sally, Padre Mkatoliki wa Afrika Kusini mwenye sura ya kike (intersex/hunta)


1704254701152.png


Mwamba Nyanda wa Morogoro, Tanzania, ni hunta
1704616427380.png

Mwanariadha Casta Semanya, Afrika Kusini, ni hunta

1704616584547.png

Mama Mwafrika na watoto wake mmoja akiwa zeruzeru
1704254736927.png

Mama Mwafrika mwenye makengeza

1704254847293.png

Mwafrika mwenye Mashoto akiwa anaandika kwa kalamu

1704279273412.png

Mtoto wa kiafrika aliyezaliwa na mdomo wa sungura

1704279379202.png

Tatizo la baadhi ya mafundisho ya dini dhidi ya uhuru wa mwafrika
1712647314230.png


Asemavyo Nyrere kuhusu tofauti kati ya ujinga na upumbavu wa Askofu LGF


 
kubariki shoga papa amekubali na amekataa kubariki mahusiano ya kishoga, maana yake ni kuwa tunao ndugu mashoga kwenye jamii tunaishi nao maofisini,makanisani nk lakini tunakataa ushoga wao, ila tunanunua kwenye maduka yao,ni madaktari,wachungaji, wafiraji,nk falsafa hii ikoje tufanyeje kutenganisha ushoga na shoga na mahusiano ya ushoga msitari iko wapi kwenye utoaji baraka.
 
View attachment 2860422
View attachment 2860423
I. Utangulizi

Askofu Severine NiweMugizi ni miongoni mwa Maaskofu wa Kanisa Katoliki machachari sana. Hataki kulala na dukuduku moyoni mwake hata siku moja.

Hivyo, salamu zake za Krismas ya 2023 ziliambatana na maoni yake binafsi kuhusu tamko liitwalo "Fiducia Supplicans" lililotolewa na Papa Francis, hapo 18 Desemba 2023, na baadaye kufafanuliwa na Vatican siku chache baadaye.

Hapa chini nafupisha salama za Askofu NiweMugizi kwa ujumla na kisha kufupisha mawazo yake kuhusu tamko hili. Kuna maswali na tafakari inafuata.

II. Muhtasari wa salamu za Askofu NiweMugizi

Naitwa Severine NiweMugizi, kwa neema ya Mungu tu, Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara. Naomba nikuletee salam na ujumbe wa Krismasi ya 2023....

Mpendwa msikilizaji tunaalikwa kumkubali mtoto Yesu azaliwe mioyoni mwetu. Aiguse mioyo yetu ibadilike kuwa mioyo safi. Atuguse tuwajibike inavyopasa....

Tumuombe atuguse tuache dhambi, uhasama, visasi, uvivu, uzembe, utapeli wa aina mbalimbali...

Tunaadhimisha Krismas hii pia baada ya Baba Mtakatifu, Fransis, kuridhia waraka uitwao "Fiducia Supplicans" yaani "Supplicating Trust."

Hili ni tamko kuhusu fundisho la Kikatoliki lililochapishwa mwezi huu, Desemba, na Dikasteri au Idara inayohusika na mafundisho ya imani ya Kikatoliki. Ujumbe wa Waraka umezua taharuki ndani na nje ya Kanisa Katoliki.


Sababu ni maagizo ya Papa yasemayo kwamba maaskofu na mapadre wanalo jukumu la kubariki watu walio katika miungano isiyo ndoa halali ikiwa ni pamoja na miungano ya wale watu wa jinsia moja, yaani mashoga na wasagaji.

Hasa dhamira za watu zimejeruhika kwa sababu ya tamko hilo na kumekuwepo na mlipuko wa mijadala kuhusu hilo...

Msimamo wa Kanisa katika mafundisho ya msingi ya imani na maadili hauwezi kubadilishwa na mtu mmoja. Papa peke yake hana mamlaka ya kubadilisha mafundisho hayo, kama hayuko katika ushirika kamili na maaskofu wenzake.

Ufunuo wa maandiko matakatifu unaweka wazi kwamba ndoa ni muungano kati ya mwanamume na mwanamke. Na Yesu amesema wazi hasa ukisoma enjili ya Mathayo sura ya 19...

Nitaje hapa, kama mchungaji wa Kanisa, Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara, baraka ziombwazo na watu wa jinsia moja wanaokuja pamoja na wanafahamika kuwa mashoga au wasagaji ni marufuku kwa mapadre kuzitoa jimboni Rulenge Ngara.

Amri hii inatolewa kwa sababu kwa sura ya nje baraka hiyo inaweza kutafsirika kuwa ni kuwathibitisha na kuwaombea waendelee na wastawi katika muungano huo ambao ni dhambi.

Hali hii itakuwa kinyume na Kristo na kikwazo kwa jamii ya waamini na hasa ukifanyika hadharani.

Nirudie tena kusema, kama waraka ulivyotambua wale watu wa jinsia moja wanaokuja kanisani hawawezi kufukuzwa. Ni wana wa Mungu kwa vyovyote. Na hao wakija kuomba kufanya kitubio watabarikiwa ili waungame na kuacha muungano ulio dhambi. Huo ndio msimamo halisi.

Baadhi ya maelezo yaliyo katika waraka yanaonekana yana mtego fulani, kwa sababu baada ya kutolewa kwa huo waraka tayari watu walianza kufurika kwa mapadre kwenda kuomba baraka na wakiwa wameshikana mikono. Hali hii inaleta kikwazo fulani.

Hivyo, tutulie na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania muda si mrefu litatoa pia tamko au msimamo kuhusiana na waraka huu....


III. Maswali yanayoibuka kutokana na salamu hizi

Kwa sehemu kubwa salamu hizi hazina tatizo. Tamko la Papa halijatengua mafundisho rasmi ya Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni kitu gani na sio kitu gani.

Tatizo liko kwenye agizo la Papa Francis kwamba maaskofu na mapadre wanalo jukumu la kubariki watu walio katika miungano isiyo ndoa halali ikiwa ni pamoja na miungano ya wale watu wa jinsia moja, yaani mashoga na wasagaji.

Askofu NiweMugizi amekaidi agizo la Papa kwa hoja kwamba ni agizo haramu kwa mujibu wa maandiko matakatifu. Hajarejea ufafanuzi wa Vatican uliotolewa kulifafanua tamko.

Ni ufafanuzi unaowataka makasisi kuondokana na dhana kwamba homosexuals, intersexuals na eunuchs ni "uchafu" kama alivyokuwa anaamini na kushikilia Papa Yohane Paul wa pili.

Na bado Papa Yohanne Paul II anao wafuasi wake leo wenye kufikiri namna hii. Askofu Flavian Cassala ni mmoj wao. Lkini zama za sayansi zimepindua mtazamo huo.

Askofu NiweMugizi ni mtalam wa sheria za Kanisa. Anajua vema kwamba sheria za Kanisa zinatofautisha kati ya mawazo yafuatayo: "ratification," "consumation," "blessing," "marital act," na mawazo baki kama haya.

Katika mipaka ya misamiati hii Tamko la Papa Francis halijakiuka sheria za Kanisa. Ni agizo halali, na ukaidi wa Askofu NiweMugizi ni haramu inayistahili adhabu ya kiutawala.

Baraka anazoziongelea Papa Francis hazina tofauti na zile zinazotolewa kwa wezi waliokiri hadharani kwamba wameiba, na hawajarudisha walichokiiba. Wanufaika wa ESCROW ni mfano hai. Mpaka leo tunawaona Kanisani wakipokea baraka.

Hivyo, ufafanuzi wa Askofu NiweMugizi unaibua maswali yafuatayo: Kasisi anaweza kuogopa kutekeleza majukumu yake kwa sababu tu ya hofu kwamba watu wanaweza kutafsiri matendo yake isivyo? Kama jawabu ni ndiyo, kwa nini kuna undumilakuweili kuhusu baraka kwa wezi wanaofahamika kwa jamii na wazinzi wa jinsia moja?

Lakini pia, kuna tatizo la kisemantiki na kiepistemolojia. Kanisa Katoliki linamaanisha nini linapotumia neno "ushoga"? Na linatumia utaratibu gani kuwatambua mashoga na wasagaji?

Kuna matukio kadhaa yanaonyesha kwamba, ndani ya Kanisa Katoliki, neno "ushoga" linatumika kama silaha ya propaganda dhidi ya wakosoaji wa baadhi ya misimamo tata ya kanisa tena wakati mwingine dhidi ya watu wasio na hatia. Mifano ipo.

Kifo cha Rodney Mutie Mengi mwaka 2005 kilizua mvutano kati ya Kanisa Katoliki na Reginald Mengi, mzazi wa Rodney.

Mengi aliweka bayana kwamba mwanaye alikufa kwa UKIMWI, hivyo akahimiza watu kuwa waaminifu au kuwa waangalifu kwa kujikinga kwa kutumia kondomu. Miongoni mwa watu walio mjibu tena kwa maandishi kupitia gazeti la Rai, kama sikosei, ni Askofu NiweMugizi.

Gazeti la Kiongozi likaunga mkono pilika kwa kuchapisha bahari "Serikali Ikemee Ushoga." Askofu KIlaini akawaita Maparoko wote wa Dar na kuwapa orodha ya watu ambao anaona kuwa ama ni manabii wa "ushoga" au mashoga kabisa, kwa sababu tu kwamba wanaandika kuhusu matumizi ya kondomu kama kingamagonjwa na/au kingamimba.

Picha kubwa inayozaliwa hapa ni kwamba mapenzi ya jenitalia kwa jenitalia yanayofanyika kwa kutumia kingamimba kama vile kondomu ni tendo la kishoga. Watu ambao sio mashoga wanaweza kufanya tendo la kishoga kweli? Hapana!

Lakini shida kubwa zaidi ni kwamba, maelezo mengi ya makasisi wetu, akiwemo Askofu Ruwaichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, hayatofautishi kati ya "homo-affective condition" na "homosexual acts."

Mkanganyiko huu umeenezwa mpaka ngazi ya ndoa kupitia mafundisho ya ndoa. Wakati wa mafundishi ya wanandoa, maparoko wengi wanawambia "wanafunzi wao" kwamba "ni mwiko kwa wanandoa kufanya tendo la kishoga," yaani ulawiti, utadhani kwamba mashoga wote wanafanya ulawiti.

Kwa njia hii wanawavisha miwani ya kishoga na wao kuanza kuitazama dunia kwa kutumia miwani hiyo. Miwani hii ni tatizo la kijamii maana inawaonyesha "ushoga" hewa.

Sababu ni kwamba, maparoko hawa wanasahau kuwa sio kila ulawiti ni tendo la kishoga na kwamba tendo la ulawiti kati ya mwanamke na mwanamume sio, na haliwezi kuwa, tendo la kishoga.

Kuna janga la kisemantiki ndani na nje ya Kanisa Katoliki. Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu tatizo hili?

Kiepistemolojia pia kuna tatizo kubwa. Kuna waseminari kadhaa huko seminari kuu wamekuwa wakiachishwa masomo kwa sababu ya madai kwamba wana "vidole vya kishoga."

Yaani wanatumia "second to fourth digit ratio (2D:4D ratio)," mbinu ambayo haikubaliki kisayansi. Nimewashuhudia Padre Kaombe, hayati Profesa Kanywanyi, na wtu baki wakitumia mbinu hii pia.

Kuna makruta waliwahi kufukuzwa kwa kutumia kigezo hiki pia. Kuna dalili kwamba "mafundisho tata ya KIkatoliki kuhusu namna ya kuutambua ushoga" yalikuwa na mchango hapa pia. Hili ni janga la kiepistemolojia. Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu tatizo hili?

Kwa ujumla ninajiuliza: Sio "utapeli" wa kidini kuwaaminisha watu kwamba kutumia kingamimba ni tendo la kishoga? Sio umachiaveli kuwavisha joho la ushoga wakosoaji wa kanisa, tena kwa kutumia hoja ambazi zingeweza kujibiwa bila kumshambulia mleta hoja? NIngependa kujua Askofu NiweMugizi anayo maoni gani kuhusu maswali haya.

IV. Hitimisho

Kwa ufupi, ni maoni yangu kwamba, tamko la Papa limekuja wakati ambapo Kanisa Katoliki mahalia halijajipanga kimtazamo ili kuweza kulitendea haki.

Papa anaongelea "paradigm shift" ambayo inahitajika katika namna ya kufikiri, kuhukumu na kutenda ndani na nje ya Kanisa Katoliki, kwa kusoma alama za nyakati tukiwa tumevaa miwani ya sayansi, teolojia na falsafa bila kubagua nyenzo yoyote kati ya hizi.

Kwenye sekta ya elimu tunasema kwamba "if one wants to teach a donkey, one must be more knowldheable than a donkey."

Katika suala la sasa, ni kwamba mtu aliye mtumwa ndani ya boma na maarifa ya sanaa na teolojia hawezi kutakatifuza ulimwengu wa sayansi kwa ufanisi.

Hivyo "paradigm shift" ndani na nje ya Kanisa Katoliki ni lazima, ikiwa inaambatana na "reconciliation" kwa wale wote ambao baadhi ya viongozi wa Kanisa wamewajeruhi kwa kutumia mbinu za kimachiaveli pasipo uhalali wowote.

Kuna sababu ya kutangaza ugomvi wa kudumu na watu kama Askofu Kilaini kwa sababu hii: Hwa ni maaskofu ambao ni wafuasi wa Nicollo Machiavelli, kwa sababu ya kufikiri kuwa inawezekana kuwanyamazisha watu wote, siku zote na sehemu zote kwa kutumia mbinu haramu ya kuwavisha joho la ushoga bila kujali kwamba ni mashoga au hapana. Haiwezekani.

V. Pendekezo

Ni muhimu hapa kuweka bayana kwamba, swali juu ya ndoa ya mke na mume ni kitu gani na ndoa ndoa ya mke na mume sio kitu gani linahitaji kujibiwa kirazini zaidi kuliko kunukuu misahafu, maana hii ni taasisi inayovuka mipaka ya kidini. Napendekeza kwamba fasili ifuatayo inakubalika kwa wengi na hivyo ifafanuliwe kila mara, kila wakati na kila mtu:

"Heterosexual marriage is a communion of persons which is ratified in public under an oath to live together alone for life, and then consummated and regularly actualized by sexual acts which are simultaneously unitive in significance and procreative in significance, regardless of whether they are procreative in effect or otherwise."

Fasili hii ikishakueleweka ndio hapo sasa tuanze kutenga muda wa kujadili "the impossibility of homosexual marriage" kwa kutumia fasili hii kama msingi wa majadiliano. Vinginevyo naona kwamba tunatapatapa.
Kimsingi Papa alikosea kutoa tamko la kitaalamu na lenye uwezekano wa kuleta mkanganyiko kwa walei.

Pope’s teachings and instructions must be succinct and free of ambiguity.

Kosa hili japo laweza kuonekana dogo, laweza kuwa chanzo cha mgawanyiko wa kimadhehebu ndani ya Kanisa Katoliki.
 
Simple: Tunapotoa baraka kwa kina Rugemalira wa ESCROW waliokiri hadharani kwamba walikwiba kutumia mahakama saa mbili za usiku mstari tunauchora wapi?
Mbona unamkomalia sana huyu Rugemalira! Alikiri wapi, tena hadharani kwamba aliiba hela za Escrow? Na kama alikiri, ilikuwaje akae ndani mpaka Magufuli alipofariki?

Halafu wewe hapo ulipo una ukamilifu gani wa kufikia hatua ya kuwanyooshea watu wengine kidole; kama siyo unafiki tu ndiyo unaokusumbua!
 
Back
Top Bottom