Avatar ipi mnaipenda?

Ni Avatar gani Mwanakijiji aitumie?

  • Napenda ya mzee mwenye Jembe (ya zamani)

    Votes: 52 59.1%
  • Napenda ya mzee mwenye mkwaju (mpya)

    Votes: 35 39.8%
  • Asitumie Avatar yoyote

    Votes: 1 1.1%

  • Total voters
    88
mimi zote sizipendi maana zinatoa tafsiri ya mtu ambae siyo vile alivyo, zote zinatudanganya tu, ya kwanza inaonyesha kuwa wewe ni mkulima na ya pili inaonyesha kuwe wewe ni mfugaji.
kwangu naona ni maigizo maana hazimuwakilishi mwanakijiji halisi kwa maana ya nafsi ingawa zinatoa ujumbe.
Ningefarijika kama ungeweka picha yako mwenyewe ama ungeacha wazi ili kila mtu atoe tafsiri yake kulingana na namna anavyosoma maandishi yako....kwangu huwa nakujengea taswira kupitia maandishi....hivi viAvatar naona kama vinasaidia utambulisho wa haraka kama hii ni post ya MM ama Ngoshwe ama Fidel80
 
duh.. inaonekana katika ratio ya 2:1 ..


Mwanakijiji;

Ina kazi sana.

Unanikumbusha hadithi za Watanzania; wanachagua viongozi for pupularity; halafu waliowachagua wakiingia madarakani wanaanza longo longo maendeleo ya kweli hakuna.

Think. Think Twice.

Huitaji kuangalia wengi wape, hao watakuja tu baadaye. Hata Nyerere alishatuonyesha njia, he went for 20% Minority to bring Changes.

Obama akafuatia, kuwa Minority Race can win the Ballot.

Kwa vigezo vyote hii mpya inakidhi haja. Ina-ipresent ile ya zamani na bado ina new touch kuendana na hoja zoote zilizotolewa na wadau.

Naomba kuwakilisha!
 
Naona kuupgrade avatar yangu kumewakwaza wengine kidogo; wapo wanapenda niendelee na ile ya jembe la mkulima (black and white) na wengine wanapenda hii mpya ya mkwaju (ya rangi). Sasa sijui wapiga kura mnasema niendelee na hii mpya watu wataizoea au nirudie ile ya zamani ambayo kama mmoja alivyosema ni "brand image"..

Labda ungetupa pia sababu za kuamua ku-upgrade. mimi nikitizama hizo picha pili napata sura mbili tofauti sana za 'Mzee Mwanakijiji'. Ile ya mwanzo ilikuwa inaonesha mtu mtulivu (na pengine aliyejaa busara!) lakini hii ya pili inaonesha mzee kama 'mshari' hivi!

Alternatively labda ungefikiria pia kuweka picha yako halisi:)!
 
Avatar ya kwanza naipenda zaidi kwani huwa kila napoiangalia inanikumbusha survey moja ya socio-economic niliyowahi kufanya ambapo nilikuwa nahoji maswali ikiwa ni pamoja na kazi wazifanyazo wanakijiji. Nilikutana na mzee mmoja kwenye kibanda chake kwanza ndio anarejea kutoka shambani (mri wake kama miaka 67-70), baada ya kumaliza utangulizi katika hojaji yangu nilimuliza:

Mimi: Sasa mzee wewe kazi yako nini?
Mzee: Sina Kazi
Mimi: Sasa wewe unajikimu vipi kimaisha kama huna kazi?
Mzee: Nahangaika na kuumia hivyo hivyo kama unavyoniona sasa ninavyorejea
Mimi: Naona una jembe, kwa maana hiyo unarejea kutoka shambani
Mzee: Ndio
Mimi: Kwa maana hiyo kazi yako ni mkulima
Mzee: Samahani kijana, kwani ukulima ni kazi?
Mimi: Ndio, kwani wewe unadhani sio kazi?
Mzee: Kwani ukifanya kosa na ukahukumiwa kwenda gerezani, shughuli utakayoikuta kule sio kilimo? Unaweza kwenda kuwa mhasibu au mwalimu
Mimi: Ndio sana sana utafanya kazi ya kulima kule. Sidhani kama unaweza kupata nafasi ya kufanya hizo kazi nyingine
Mzee: Je baada ya kutoka gerezani utapata kiinua mgongo, kama wewe unvyotegemea utakavyostaafu.
Mimi: Hapana huwezi kupata kiinua mgongo, kwani ile ni adhabu
Mzee: Je, hapa Tanzania, sisi wakulima tunapozeeka kwani tunapata kiinua mgongo au mafao ya uzeeni?
Mimi: Hapana
Mzee: Kwa maana hiyo, ukulima sio kazi ila ni ADHABU. Tofauti ni mazingira tu, lakini serikali inafurahia sana wananchi wanapokuwa wazalishaji yenyewe inauza mazao nje wala huwezi kujua thamani halisi ya mazao, na unapojichokea unaachwa kujifia mwenyewe kijijini. Lakini nyie wenzetu.

Hii sio habari ya kutunga.

Avatar ya pili:
Naiona kama ya mzee wa kifugaji kule loliondo na Hanany, ambao kwa asili wao kazi yao ni kukaa vijiweni na kunywa pombe, kwani sehemu kubwa ya uchungaji hufanywa na morani na kina mama (Wenetu hawa wanafanya kazi zao kwa rika). Kwa sasa inaonekana huyu mzee hana uhakika wa kupata maziwa na pombe yake ya kila siku kwani maeneo yao ya kuchungia mifugo yameuzwa (mfano Loliondo n.k). Hapo kama anatafakari, nini kitafuata baada ya hapa baada ya sisi kuonekana kutokuwa na thamani katika ardhi ya nchi yetu! (Hii ya pili nimeijengea mzingira wafugaji wetu wanayokabiliana nayo ambayo nayo ni halisi).

Hivyo kwangu mimi zote ni nzuri na zinamwakilisha Mtanzania nyonge asiyekuwa na haki ndani ya nchi yake. Kura yangu inaanguka kwa MZEE MWANAKIJIJI
 
Naona kuupgrade avatar yangu kumewakwaza wengine kidogo; wapo wanapenda niendelee na ile ya jembe la mkulima (black and white) na wengine wanapenda hii mpya ya mkwaju (ya rangi). Sasa sijui wapiga kura mnasema niendelee na hii mpya watu wataizoea au nirudie ile ya zamani ambayo kama mmoja alivyosema ni "brand image"..


Mkuu Mwkjj, sa huyu mzee atakua anafaidikaje na wewe kuitumia picha yake? Haki miliki ya hiyo pic umeipataje? je alikupa mwenyewe au?
Vp kama ni marehemu na wewe unaendelea kumdisplay pasipo concern ya ndugu zake?
 
Naona kuupgrade avatar yangu kumewakwaza wengine kidogo; wapo wanapenda niendelee na ile ya jembe la mkulima (black and white) na wengine wanapenda hii mpya ya mkwaju (ya rangi). Sasa sijui wapiga kura mnasema niendelee na hii mpya watu wataizoea au nirudie ile ya zamani ambayo kama mmoja alivyosema ni "brand image"..
ile ya mwanzo unaonekana mkulima umechooooka,ndio maana mafisadi wanaidharau hii kidogo inatia heshima maana wakidharau utawacharaza na bakora yako hiyo.
 
Usibadilishe brand yako please kwani mimi niona makala yoyote yenye picha ile ya mwazo popote pale najua ni mwanakijiji bila hata ya kuangalia mtunzi. Its your selling logo dont change it!
 
Mazoea yana taabu, baada ya kumzoea Mzee Mwanakijiji vile ilivyozoeleka, ilishafikia kiwango cha avatar yake kuwa iconic, hivyo mabadiliko yatachukua muda kuzoeleka na mpaka kukolea.

Japo hiyo ndio kuonyesha uliberali, mimi bado naunga mkono uconservative wa kubadili baadhi tuu ya mambo yanayokwenda na wakati wakati yale ya asili tukiyaconserve.

Bado nampenda zaidi Mwakijiji yule niliyemzoea kuliko Mwanakijiji huyu mpya.
 
Naona hii mzee Mwanakijiji ana bling kwenye sikio.....sijui ndo kwenda na wakati huko au vipi....
 
Wewe ni babu wa mabadiliko hivyo ni lazima ubadilike kutokana na wakati hivyo basi ni vizuri kubadili ID yako na siyo jina lako
 
Tumia ya awali mkuu, inadhhirisha kuwa mtanzania wa kijijini mtaji wa nguvu zake ni jembe la mkono, majority.
 
Mkuu Mwkjj, sa huyu mzee atakua anafaidikaje na wewe kuitumia picha yake? Haki miliki ya hiyo pic umeipataje? je alikupa mwenyewe au?
Vp kama ni marehemu na wewe unaendelea kumdisplay pasipo concern ya ndugu zake?

ni picha ya kuchora hiyo... special order. Ile avatar inayotumika kwenye magazeti sitaibadilisha kwa hiyo hilo lisiwe na shaka. Hii mpya ni kwa kutumia online hapa tu.. jamani mwanakijiji si anaweza kuwa na picha za zamani na mpya...
 
ni picha ya kuchora hiyo... special order. Ile avatar inayotumika kwenye magazeti sitaibadilisha kwa hiyo hilo lisiwe na shaka. Hii mpya ni kwa kutumia online hapa tu.. jamani mwanakijiji si anaweza kuwa na picha za zamani na mpya...

mzee, mtazamo huo si sahahi.

kumbuka marketing haiishii kwenye magazeti tu! nimekushauri utumie ya zamani, lakini kama umeamua kutumia mpya licha ya ushauri wa wengi (angalia poll) basi tumia kila mahali zinapopatikana habari zako, mtandaoni na magazetini. that is you brand image, labda kama una sababu mahsusi.

hata hivyo i am talking from marketing point of view.
 
..........Ya zamani ilikuwa poa labda kwa sababu tulikuzoea kukuona katika ile avatar.
Lakini hata hii tutazowea tu, nakuona umeamua kuonekana mzee wa 21 century umevaa na earring.
 
..........Ya zamani ilikuwa poa labda kwa sababu tulikuzoea kukuona katika ile avatar.
Lakini hata hii tutazowea tu, nakuona umeamua kuonekana mzee wa 21 century umevaa na earring.

hizo ni zile za jadi..
 
Back
Top Bottom