Avatar ipi mnaipenda?

Avatar ipi mnaipenda?

Ni Avatar gani Mwanakijiji aitumie?

  • Napenda ya mzee mwenye Jembe (ya zamani)

    Votes: 52 59.1%
  • Napenda ya mzee mwenye mkwaju (mpya)

    Votes: 35 39.8%
  • Asitumie Avatar yoyote

    Votes: 1 1.1%

  • Total voters
    88
ile ya zamani imekee kiukweli kabisa...hi sijaipenda kabisa halaf ile ukiingalia kwa makini inashabihiana na mzee mwanakijiji kiukweli lkn hii walaaa
 
Mzee Mwanakijiji Mimi naipenda ile ya Zamani ile ambayo ulikuwa unasokota sijui Bangi au Tumbaku nataka niianzishie Thread Kushinikiza uiweke japo kwa siku moja

Naipenda ile kuliko hizi Mbili

umenikumbusha ile ya original yenyewe!!
 
Ya ZAMANI inaendana na Busara zinazooneka kwenye mada zako mbali mbali. tafadhali rudisha AVATAR ya zamani
 
aahh, isiwe ishu, mi kuanzia kesho nitakua naitumia ile avata ya zamani.
ALINIUZIA NIMESHAINUNUA.
 
Mi nafikiri ile ya zamani yafaa zaidi. Hii mpya huyu Mzee hajakaa kiTz Tz! I might be wrong lakini yupo kama wa kutoka SA hivi
 
Kusema ukweli, ile ya zamani (ya jembe) huwa inanifanya nipende kusoma si tu makala unazo bandika humu jamvini ila hata unazobandika kwenye vyombo mbalimbali vya habari hususani magazeti. Kwangu ni kama nembo inayonisukuma kuangalia nini kilicho ndani yake zaidi. Tafadhali irudishe!
 
Naipenda ya zamani kwa sababu huwa inanitia uchungu sana kwani ni ukweli pamoja na utajiri wote wa nchi yetu bado asilimia 80 ya wanakijiji wantumia jembe techn.ya 18century.
 
mie ile ya kwanza sijaiona... lakini hii sasa ni safi kabisa
 
Pendekezo langu, naomba urudishe ile ya zamani na tayari nimeipigia kura irudi...
Hii ya sasa hivi inaonyesha ni mzee maskini asiyejua kujishughulisha kazi yake ni kuzurura tu vibarazani na bakora yake.

Ya zamani ina vutia sana inaonyesha ni Mzee Mwanakijiji wa ukweli ambaye ni mjasiria mali anajua kilimo ni uti wa mgongo wa Mtanzania alisi Kilimo kwanza fimbo baadae!
 
acha hii bana

yaani niikona naimajini ulivyo!

lile jembe halina dili mbolea ya ruzuku si ndo hii wameiba yote,
 
Naipenda ile ya zamani, ulionekana mzee mchapa kazi sana na busara tele...
hii pia iko poa kiasi chake labda with time tutaizoea
but I have voted for the other one though, I love it.
Inanipa tafsiri mbali mbali niki-compare na mabandiko yako!!!
 
Mzee wa Zamani, hii avatar ya sasa imekaa uzuri sana, inaonekana mzee makini, it is a representation ya posts zako.
Ile ya zamani yes ni nzuri lakini inaonyesha mzee mnyonge mnyonge hivi.

I like the new one. Keep it old chap.

Without a possibility of change in meanings human communication could not perform its present functions.
 
Hii mpya hunaonekana mwanakijiji ambaye maisha yamekunyookea miongoni mwa walalahoi unaweza hata kukunua kofia, unavaa smart, ndevu umepiga "wese jingi zinang'ara,umetengeneza mpaka "ooo" ", unapiga "bring bring"sikioni na shingoni..., huko miguuni hatuoni, yawezekana ukawa umepiga "mokasin" kali kama sio ya "Berluti Reprisés"....sina shaka pia mkononi ukawa na saa ya "ChronoSwiss kama si Omega " kiunoni una mkanda mkali wa ngozi ya mamba au chatu unashikilia suluali ya "hacoupian" (very expensive amongst few!)...

Kwa hii Avatar kama hutakuwa unaishi mjini kwa wanao, basi umepata mafao yako ya kustaafu hivi punde, basi kwa huko kijijini heshima ipo juu sana na pengine utakuwa fisadi miongoni mwa wanakijiji wenzio, we ulimi bali unalimisha watu...

Rudisha ile ya zamani bana kama hujaiuza/kuikodisha au kuibinafisha!

attachment.php
 
Huyu babu mbona ana onekana kama matonya?Jamani kwa wale mnayemjua yule omba omba maarufu aliyekuwa Dar es salaam sasa hivi yupo Morogoro wamefanana sana!
 

Attachments

  • MZEE_ANTHON_MATONYA_PIX_NO_1.JPG
    MZEE_ANTHON_MATONYA_PIX_NO_1.JPG
    19.7 KB · Views: 74
Ile ya zamani ndo nzuri!
Imeshazoelekea maana mpaka kwenye magazeti imetumika, sasa endapo utaamua kubadilisha;
know one thing for sure, perception yako kwa watu itabadilika ina both ways (+ve & -ve)
Kwa sisi ambao tunauelewa flani wa mambo ya masoko, tunakushauri usibadili
Endelea kutumia ile ya zamani huku ukiwazoesha watu taratibu hii mpya kwa kuichanganya na ile ya zamani,
kwa kufanya hvyo utaweza kukusanya opinions zao na kujua wanajamii wanaichukuliaje
before you decide which is which
Ni hayo tu!
 
Avatar ya zamani ni nzuri sana na naipenda.

Hii ya sasa siipendi tu!
 
Avatar ya zamani ni nzuri sana na naipenda.

Hii ya sasa siipendi tu!
hahahaaaa,
nakubaliana na wewe mpwa,
OLD IS GOLD, mkuu mwanakijiji nadhani utakubali hili.
IRUDISHE ya zamani ASAP
 
Back
Top Bottom