Arusha bhana raha uizunguke na uijue ukipita tu bara bara kuu hamna kitu ,ingia huko ndani sasa dah unaweza zimia,Arusha ni mkoa ambao vijana wadogo wanamaisha kitu ambacho kinamuactivate kijana mwingine kupambana,sehemu nyingi Arusha nimefika but huwezi linganisha na sehemu yoyote yaan unaweza ingia porini ukakuta na investment za hatari mfano Dolly estate dah dah dah kile ni kijiji kingine maana nature imehifadhiwa kama ilivyo kisha kukawekwa tu maisha ya wanadamu ,na u appreciate sana mji wa Arusha. Kero ya Arusha ni maisha tu yako juu sana yaani kuingiza laki kwa siku kawaida na kuimaliza kwa siku kawaida tena sio kwa matumiz ya anasa ni hela unaingia nayo sokoni inaisha ,nyumba nzima kuna sehemu unapanga kwa laki moja Arusha nyumba zinapangishwa mpaka interms of dollers na uswahilini unapata nyumba nzima room tatu tu kwa laki 2 na nusu .
Arusha ni sehemu pekee wazazi ni lazima kuwatafutia watoto elimu na maisha yaani mtoto anasomeshwa na kama mzazi ni masikini basi anampa mtoto kiwanja anamwambia jenga ,kama wazazi wanakipato kidogo mtoto anakabidhiwa nyumba na mashamba aendeshe maisha yake maana ni mwiko MAJOGOO MAWILI KUKAA NYUMBA MOJA,huwezi vaa kitaulo chako kwenye nyumba ya baba it looks funny but ndio sababu maendeleo yapo sio kama mikoa mingine mtoto upate kwa shida zako mwenyewe na ukipata ujengee wazazi kisha ndio wewe ujenge kwako(si lalamiki kuhudumia wazazi msinielewe vibaya nawapenda sana wazazi ila naiangalia kwenye fact ya maisha ya sasa ,kujenga nyumba ni ngumu sasa fikilia unatakiwa ujenge nyumba mbili yaani ya wazazi wako na ya kwako hapo hakuna ya biashara hata moja,kwanini umasikini usiendelee),Arusha kila utakachofanya ni pesa hata kulima we lima Arusha muda wote soko liko mazao hayawezi ozea shambani yaani utapata shida ya bei tu ila si kukosa pa kuuza na ukiwekeza zaidi mfamo kujenga green house hali ya hewa ya Arusha ni nzuri mno ndio maana world best flowers companies ziko kwenye ardhi ya Arusha,nadhani wa mikoa mingine tujifunze toka kila mkoa kama Arusha upande wa utafutaji wa maisha .God bless TANZANIA