Arusha halisi ilivyo na watu wake

Arusha halisi ilivyo na watu wake

Arusha miaka ya 1950 mikoa mingine hata supermarket hawajaota.......

b00598-p04645.jpg


b00598-p04646.jpg


b00598-p04653.jpg


b00598-p04652.jpg

Alafu kuna vichaa wanasema Arusha imependelewa na CCM eti kwa kupewa mawaziri wakuu wengi ambao walipendelea Arusha
 
Wee ni muongo sana ,unasifia kwenu mpaka unapitiliza na vya wenzenu unafanya vya kwenu hapo namba 4 umeitaja mbuga ya serengeti kwamba ipo Arusha ni uongo, Serengeti haipo Arusha, Serengeti ipo mkoa wa Mara,sema tu watalii wengi hupenda kuanzia safari ya kwenda huko kwa kutokea Arusha.
Soma vizur mkuu serengeti ipo karibu na Arusha
 
Habari zenu wadau.

Kwanza naomba niseme huu uzi hauna lengo la kuilinganisha Arusha na mkoa wowote Tanzania pia nataka huu uzi utumike kama reference kwa threads zote zitakazouongelea mji wa Arusha.

Dhumuni la kuuanzisha uzi huu ni kutokana na wimbi kubwa la members huku kuusema mji wa Arusha kwa namana tofauti ambazo pengine kutokana na kuwa sio wakazi wa Arusha wanaweza wasiwe sahihi sana.

MAMBO YA KIPEKEE KUHUSU MKOA WA ARUSHA.

1. Hati rasmi za uhuru wa Tanzania zilitiwa sahihi hapa na Uingereza mwaka 1961.

2. Azimio la Arusha la kujitegemea lilipitshwa mjini hapa karibu na maeneo ya mnara wa saa.

3. Makubaliano ya Arusha accords ya kusitisha vita nchini Rwanda yalipitishwa mjini Arusha mwaka 1993.

4. Una mbuga nyingi barani Africa, Hali ya hewa ni nzuri sana. Mbuga ya wanyama ya Serengeti na Ngorongoro, Ziwa Manyara, Olduvai Gorge, Arusha National Park,Tarangire na mlima Kilimanjaro zipo ndani\karibu na mji huu.

5. Arusha imechezwa movie ya Hollywood maarufu kama HATARI mwaka 1962.....Hatari! (pronounced [hɑtɑri], Swahili for "Danger!") is a 1962 Americanaction/adventure romantic drama film directed by Howard Hawks and starringJohn Wayne. It portrays a group of professional wildlife catchers in Africa.[2]The film includes dramatic wildlife chases and the scenic backdrop of Mount Meru, Arusha a dormant volcano.

6. Wakati mikoa yote inahangaika na madawati likiwemo jiji kuu la Dar, Arusha haikuwahi kuwa na upungufu wa dawati hata moja na kila secondary school inayo maabara hata kabla ya agizo la Rais. (shule nyingi za serikali za Arusha zina computer labs)

7. Arusha ndio mkoa wenye matumizi makubwa ya Internet kuliko Mkoa wowote Tanzania and East Africa.

8. Arusha ni mkoa wa kwanza kwa Social Development Index (Huduma Bora za Kijamii kama maji, life expetancy, Health services, Education) By UNDP

9. Arusha ndio mkoa unaofatia ukitoka Dar kwa wingi wa viwanda na kuchangia katika pato la Taifa.

10. Arusha ndio mkoa wenye gharama za juu za maisha kuliko mkoa wowote Tanzania, kama unataka kuanzia maisha Arusha na una uhakika hauna kipato cha kujitosheleza nakushauri ujaribu Mwanza.

CHANGAMOTO ZA JIJI LA ARUSHA

1. Roads Roads Roads, Barabara Arusha zipo nyingi ila ni nyembamba kutokana na mji huu kuwa na masterplan ambayo ni ya muda mrefu, Maeneo ambayo yanatakiwa kuwekewa mkazo ni pamoja na Olasiti, Olasiver, Englesheraton, USARiver, Moshono, Kisongo, Ngaramtoni ambapo ndipo mji unaelekea.

Mimi kama kama mzaliwa Arusha na nimetembea mikoa yote sio kupita kwa bus wala kukaa siku 2 bali nimeishi mikoa mingi kwa kweli, nimekuja koconclude Arusha ni ya kipekee sana kuanzia tabia za watu wa Arusha ni tofauti 100% na watanzania wote, Maisha ya watu wa Arusha ni tofauti na mikoa mingine na hata wa mikoani wakija Arusha wanakiri maisha ya Arusha na watu wake ni wa tofauti.

#Arusha #GenevaOfAfrica #SafariCity #UN #A-Town #Machalii #Mamong'oo #Arachugga #Mabillionare #Meli #Mafogo #MjiWaMabilionea #HalfLondon #TheOnly #MjiWaWajanja #Tanzanite #HeadQuaters #EastAfricaCommunity #Zurich #TanzaniteInTheSky #Wakakamavu #ChaliAraa #Jombii #Ungalelo #Matejoo #Ungalimii #Arifu #Makamanda #USARiver #Watengwa #Weusi #Nako2Nako
Hizi mada za kuisifia arusha sijui zina lengo gani.
Ninyi vijana wa arusha hao wakenya wamewalemaza mawazo huko kijijini kwenu arusha mnaanza kuwaiga tabia zao za kibaguzi.
Hivi nikuulize mleta uzi hiyo mada itawasaidia nini watanzania wa mikoa mingine.
Mkumbuke kwamba mnavyozidi kujitekenya humu JF na kisha mnacheka wenyewe mjue watanzania wenye uelewa wanazidi kuwadharau.
Kuna msemo unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza huko kujitembeza kwenu mitandaoni kuisifia arusha ni kama mnautafutia bwana mkoa wa arusha.
Tulieni watu watakuja huko arusha na watawasifia hapa JF.
Nitarudi badae
 
Hizi mada za kuisifia arusha sijui zina lengo gani.
Ninyi vijana wa arusha hao wakenya wamewalemaza mawazo huko kijijini kwenu arusha mnaanza kuwaiga tabia zao za kibaguzi.
Hivi nikuulize mleta uzi hiyo mada itawasaidia nini watanzania wa mikoa mingine.
Mkumbuke kwamba mnavyozidi kujitekenya humu JF na kisha mnacheka wenyewe mjue watanzania wenye uelewa wanazidi kuwadharau.
Kuna msemo unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza huko kujitembeza kwenu mitandaoni kuisifia arusha ni kama mnautafutia bwana mkoa wa arusha.
Tulieni watu watakuja huko arusha na watawasifia hapa JF.
Nitarudi badae

Kwani katiba inakataza mtu kujivunia kwake??
 
Hatutaki ligi soma uelewe...amesema zipo ndani ama karibu na mji wa arusha sasa Serengeti inaangukia upande wa karibu na mji wa arusha
Serengeti haipo Arusha,na mleta mada hoja yake kuu anauzungumzia mkoa wa Arusha,sasa suala la kuzungumzia vitu vilivyo karibu mkoa wako na kuvifanya ndio advantage ya mkoa wako hiyo ni irrelevant na hoja yenyewe na yeye mwenyewe mwanzo kabisa amesema hana lengo la kuulinganisha mkoa wa Arusha na mkoa mwingine,so alichopaswa kuzungumzia yeye ni mkoa wa Arusha tu,kama kuwa karibu na Serengeti basi mwanza wako karibu zaidi kuliko Arusha,yeye alipaswa kuzungumzia ni vile vilivyomo Arusha na uzuri wa Arusha tu na maeneo yake kama vile karatu,kwa mrombo,oljoro ,ikidinga, maji ya chai,usa river,ngulelo,ngaramtoni.kisongo,monduli,muriet,majengo,mbauda ,njiro,moshono,kijenge,tengeru,na kwingineko
 
Kitu cha kweli nachojua mimi swala la kipato kingi taifa linavuna ni Dar na Mwanza ikifuatiwa na Mbeya,hiyo ni tosha kuonyesha Arusha imekalia wapi na siyo misifa tu bila la maana,all in all hii ni Tanzania yetu sote,ila mkileta ubaguzi nakuapieni Arusha hamuifati Mwanza,maana hilo ndo hua linawaumiza,sema hamuwezi kuamini kwa sababu jamii ya Mwanza ni ya kistaarabu haina majivuno,kuleta maneno ya kusifia majengo,mala keepleft ndani ya mji kama napoona hapo juu ndugu mmoja kapiga picha na kupost hapa ni utoto tu au kutokuelewa maana maeneo yenu hayo tunayajua na muonekano wa picha siku zote utaona kama kitu kinatisha kumbe ni bla bla.fanyeni mkoa uwe na kipato kizuri kitaifa ndo mjisifie
 
Serengeti haipo Arusha,na mleta mada hoja yake kuu anauzungumzia mkoa wa Arusha,sasa suala lakuzungumzia vitu vilivyo karibu na kuvifanya ni vyako hiyo ni irrelevant na hoja yenyewe na yeye mwenyewe mwanzo kabisa amesema hana lengo la kuulinganisha mkoa wa Arusha na mkoa mwingine,so alichopaswakuzungumzia yeye ni mkoa wa Arusha tu,kamakuwa karibu na Serengeti basi mwanza wako karibu zaidi kuliko Arusha,yeye alipaswa kuzungumzia ni karatu,kwa mrombo,oljoro ,ikidinga, maji ya chai,usa river,ngulelo,ngaramtoni.kisongo,monduli,muriet,majengo,mbauda ,njiro,moshono,kijenge,tengeru,na kwingineko

Wewe umeona Serengeti pekee?? Kwani Kilimanjaro upo Arusha?? Alichosema ni zipo au zipo karibu.. Serengeti watalii wote wanaoenda huko wanapitia Arusha.. Kampuni zote za kitalii zinazopeleka watalii Serengeti ni za Arusha.. Ebu niambie wewe ni watalii wangapi wanapitia Mwanza?? Ni kampuni gani ya tours inapeleka watalii Serengeti ambayo HQ zake ni Mwanza au huko Mara?? Purposefully anayefaidika na Serengeti zaidi ni Arusha kuliko hata huyo Mara na Mwanza..
 
Soma vizur mkuu serengeti ipo karibu na Arusha
Mleta mada kajichanganya ,hakupaswa kuhusisha vitu vilivyo karibu na Mkoa wa Arusha kwa msingi wa hoja yake anauzungumzia mkoa wa Arusha sasa kuzungumzia eti Mkoa waArusha upo karibu na mkoa mwingine hapo si sawa,angalia sifa nyingi alizoziorodhesha ni za mkoa wa Arusha tu sasa kama alikua anataka kuuzungumzia mkoa wa Arusha hakupaswa kukodi majeshi na kufanya kama ndio sifa ya mkoa wa Arusha
 
Kitu cha kweli nachojua mimi swala la kipato kingi taifa linavuna ni Dar na Mwanza ikifuatiwa na Mbeya,hiyo ni tosha kuonyesha Arusha imekalia wapi na siyo misifa tu bila la maana,all in all hii ni Tanzania yetu sote,ila mkileta ubaguzi nakuapieni Arusha hamuifati Mwanza,maana hilo ndo hua linawaumiza,sema hamuwezi kuamini kwa sababu jamii ya Mwanza ni ya kistaarabu haina majivuno,kuleta maneno ya kusifia majengo,mala keepleft ndani ya mji kama napoona hapo juu ndugu mmoja kapiga picha na kupost hapa ni utoto tu au kutokuelewa maana maeneo yenu hayo tunayajua na muonekano wa picha siku zote utaona kama kitu kinatisha kumbe ni bla bla.fanyeni mkoa uwe na kipato kizuri kitaifa ndo mjisifie

Kipato kipi mkuu?? Kodi inayokusanywa na TRA Arusha ni zaidi ya kodi yote inayokusanywa Mwanza, Kagera na Shinyanga.. GDP per capita ya Arusha ni 2.1 M wakati ya Mwanza ni 1.7 M.. Hizi ni takwimu za kitaalamu si blah blah
 
Back
Top Bottom