Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Kwa maoni yangu na namna ninavyomtathmini Rais Magufuli ni wazi upepo wa URAIS umemkataa kabisa.

Tathimini hii nimeifanya kwa kujaribu kulinganisha mwenendo wake kama Rais kwa miaka miwili na nusu na mienendo anayotakiwa kuwa nayo kiongozi ngazi ya Rais.

Ni wazi kwamba kiongozi huwezi kuwa kamili na kuwezi kuridhisha kila mtu lakini Magufuli kazidi. Yapo mambo kadhaa anayafanya ya kawaida sana japo yeye anayachukuliwa kama mambo yasiyo ya kawaida na kutaka kulazimisha apongezwe. Mbaya zaidi Rais Magufuli yeye binafsi anajiona ni rais bora na wa kipekee na anataka watu wamchukulie hivyo japo kiukweli anajidanganya.

Ukiweka vigezo vya Rais bora kulinganisha na mwenendo wa Rais wetu ni wazi hawezi fika hata asilimia 10 ya vigezo hivyo. Rais Magufuli ameshindwa kuifanya nchi itulie angalau iwe na uelekeo fulani,kila kukicha ni vurugu na matukio ambayo yanafanya nchi kukosa mwelekeo.

Kibaya kingine ni yeye kuvuruga mfumo badala ya kuipeleka nchi kwenye taasisi imara zenye uwezo wa kujisimamia yeye amejilimbikizia kila kitu. Matokeo yake mambo hayaendi au yanaenda kusiko uelekeo sahihi. Jambo hatari ambalo amekuwa nalo Rais ni ubabe wa kujigeuza mmiliki wa nchi badala ya kiongozi. Amekuwa sio mtu wa kutafuta muafaka,mfano mdogo ni ugomvi wake na vyama vya upinzani na maaskofu. Ugomvi huu kila mtu anajua hauna afya kwa nchi.

Rais anaona kukaa meza moja na wapinzani ni aibu kwake kwamba ataonekana dhaifu. Hii ni kama sawa na mtu anayenuka majasho badala ya kuoga anahipaka marashi kutoa harufu,huwezi kutoboa.

Mambo kama haya ndio huzaa madikteta wa kung'ang'ania madaraka. Ni dhahiri rais inakuwa ngumu kutoka madarakani kwa sababu ya uadui aliojitengenezea kwa wananchi. Anajishtukia kuwa anaweza kufanyiwa kitu mbaya akiwa sio Rais.

Sina mengi namtakia busara sana Rais wetu Mungu ampe hekima
 
Ni nyie wavuta BHANGI wa ufipa mlio kwenye kaproject maalumu ka kuandika upuuzi humu ndio MNACHUKI NAE Nna ndio maana waaandikaji wa UPUUZI NI WALE WALE KILA SIKU.....
Ila ukweli ni kwamba MAGUFULI NI RAIS BORA KUWAHI KUTOKEA KWENYE NCHI HII......kuthibitisha hili subiri uo upuuzi wenu unaopangwa HAPO UFIPA kupitia KIMAMBI KAMA UTAFANIKIWA unless otherwise mlete hapo VIJANA WA REDBRIDGADE MLIO WAFICHA KULETA VURUGU
 
Albert Einstein
Ni MTU aliyepata bahati ya kupewa urais Bila kupigiwa kula lakin alikataa alipoulizwa kwa nini
Alisema."Siasa Ngumu kuliko Physics"
Sasa huyu mkemia aka investor wa Acid ataweza kweli??
Kula=Kura
 
Ni nyie wavuta BHANGI wa ufipa mlio kwenye kaproject maalumu ka kuandika upuuzi humu ndio MNACHUKI NAE Nna ndio maana waaandikaji wa UPUUZI NI WALE WALE KILA SIKU.....
Ila ukweli ni kwamba MAGUFULI NI RAIS BORA KUWAHI KUTOKEA KWENYE NCHI HII......
Hebu sema ubora wake upo wap
Leta hoja
 
Wako wapi kina JINGALAO? Njooni mlitetee jiwe lenu. LIZABONI alihangaika Sana humu usiku na mchana kumtetea, siku hizi sijui Yuko wapi!
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Wanakemia waacheni wafanye kazi labaratory. Ikulu waachieni waliosomea utawala. Tatizo tunafikiri kuwa ikulu kila mtu anaweza kwenda fanya kazi kama Rais kama vile katiba inavyoeleza.

Ukweli si hivyo, na ndio maana wadau tofauti wameshaanza kuwatahadharisha watanzania kuwa chaguzi za mbele wachague mtu na sio chama.

Hii inamaanisha kwamba kama chama unachokipenda kimeteua mwendawazimu asiyefaa unachotakiwa si kujali mapenzi yako ya chama bali angalia mtu. Kama ni mbaya/hana uwezo/mwendawazimu basi mtose mgombea huyo na chama chake.

Hii itasaidia sana siku za mbele kwa kamati kuu za vyama kujitathimini juu ya mgombea wataomchagua/teua.
 
Kwa maoni yangu na namna ninavyomtathmini Rais Magufuli ni wazi upepo wa URAIS umemkataa kabisa.

Tathimini hii nimeifanya kwa kujaribu kulinganisha mwenendo wake kama Rais kwa miaka miwili na nusu na mienendo anayotakiwa kuwa nayo kiongozi ngazi ya Rais.

Ni wazi kwamba kiongozi huwezi kuwa kamili na kuwezi kuridhisha kila mtu lakini Magufuli kazidi. Yapo mambo kadhaa anayafanya ya kawaida sana japo yeye anayachukuliwa kama mambo yasiyo ya kawaida na kutaka kulazimisha apongezwe. Mbaya zaidi Rais Magufuli yeye binafsi anajiona ni rais bora na wa kipekee na anataka watu wamchukulie hivyo japo kiukweli anajidanganya.

Ukiweka vigezo vya Rais bora kulinganisha na mwenendo wa Rais wetu ni wazi hawezi fika hata asilimia 10 ya vigezo hivyo. Rais Magufuli ameshindwa kuifanya nchi itulie angalau iwe na uelekeo fulani,kila kukicha ni vurugu na matukio ambayo yanafanya nchi kukosa mwelekeo.

Kibaya kingine ni yeye kuvuruga mfumo badala ya kuipeleka nchi kwenye taasisi imara zenye uwezo wa kujisimamia yeye amejilimbikizia kila kitu. Matokeo yake mambo hayaendi au yanaenda kusiko uelekeo sahihi. Jambo hatari ambalo amekuwa nalo Rais ni ubabe wa kujigeuza mmiliki wa nchi badala ya kiongozi. Amekuwa sio mtu wa kutafuta muafaka,mfano mdogo ni ugomvi wake na vyama vya upinzani na maaskofu. Ugomvi huu kila mtu anajua hauna afya kwa nchi.

Rais anaona kukaa meza moja na wapinzani ni aibu kwake kwamba ataonekana dhaifu. Hii ni kama sawa na mtu anayenuka majasho badala ya kuoga anahipaka marashi kutoa harufu,huwezi kutoboa.

Mambo kama haya ndio huzaa madikteta wa kung'ang'ania madaraka. Ni dhahiri rais inakuwa ngumu kutoka madarakani kwa sababu ya uadui aliojitengenezea kwa wananchi. Anajishtukia kuwa anaweza kufanyiwa kitu mbaya akiwa sio Rais.

Sina mengi namtakia busara sana Rais wetu Mungu ampe hekima
Jambo jema umesema ni maoni yako, bahati nzuri Mungu aliumba kila binadamu na kichwa na ubongo wa kumtosha yeye
 
Mara aseme Urais amesakiziwa......

Mara aseme ameenda yeye mwenyewe kuchukua fomu za Urais

Yaani ni Rais mwenye vituko hajawahi tokea hapa TZ!
Yaani sijui ilikuwaje hata haya yote yakatokea... Badala ya keki watanzania tukajikuta tumeshikilia Jiwe hadi miaka 5 ipite kama si 10.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom