Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
kwamba uongozi wa nchi umekushinda? Kwanini kupambana na ufisadi kuwaathiri Watanzania walio wengi ambao si mafisadi?

Kama ufisadi mbona nawe unaufanya!? Hujasema lolote kuhusu rushwa ya milioni 10 kwa kila mbunge wa MACCM iliyotolewa October 25, 2016 pale lumumba?

Mbona unaendeleza ubadhirifu kwa kuchota trillions kutoka hazina bila idhini ya Bunge?

Kujenga chato Airport ni ubadhirifu mwingine unaofanya. Hivyo achana na uongo wako sema kweli tu uongozi wako wa nchi umeshindwa na utaendelea kushindwa kutokana na sera MUFILISI, kukurupuka na kuendesha nchi kama vile una hati miliki.

"Licha ya ukweli kutokana na hatua tunazozichukua za kuwabana mafisadi na wabadhirifu wa mali za umma, wapo wananchi wa kawaida ambao si wezi wala mafisadi wanaoathirika, hili ninalifahamu, lakini kama kweli tunataka kupambana na wizi na ubadhirifu pamoja na kuleta maendeleo kwa nchi yetu, athari hizi hatuwezi kuzikwepa, mabadiliko ya aina yoyote ile lazima yana athari kama hizi, lakini jambo la kututia moyo ni kwamba athari hizi mara nyingi ni za kipinzdi kifupi", amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba..."Mabadiliko ni magumu mwanzoni, yatakuwa machungu yanapofikia katikati, lakini mwishoni matokeo yake ni mazuri au ni matamu, hivyo nawaomba wananchi na watanzania tuvumile katika kipindi hichi cha mpito, baada ya muda mfupi mambo yatakuwa mazuri, lakini hata kama hayatakuwa mazuri hivi karibuni, watoto na wajukuu zetu watanufaika, na huo ndio uzalendo".
Pointless
 
Naongeza na hii pia!sababu ya kutopandisha mshahara Kwa watumishi wa umma ni ?jamaa Hana mzigoo Baba

Ova
 
kwamba uongozi wa nchi umekushinda? Kwanini kupambana na ufisadi kuwaathiri Watanzania walio wengi ambao si mafisadi?

Kama ufisadi mbona nawe unaufanya!? Hujasema lolote kuhusu rushwa ya milioni 10 kwa kila mbunge wa MACCM iliyotolewa October 25, 2016 pale lumumba?

Mbona unaendeleza ubadhirifu kwa kuchota trillions kutoka hazina bila idhini ya Bunge?

Kujenga chato Airport ni ubadhirifu mwingine unaofanya. Hivyo achana na uongo wako sema kweli tu uongozi wako wa nchi umeshindwa na utaendelea kushindwa kutokana na sera MUFILISI, kukurupuka na kuendesha nchi kama vile una hati miliki.

"Licha ya ukweli kutokana na hatua tunazozichukua za kuwabana mafisadi na wabadhirifu wa mali za umma, wapo wananchi wa kawaida ambao si wezi wala mafisadi wanaoathirika, hili ninalifahamu, lakini kama kweli tunataka kupambana na wizi na ubadhirifu pamoja na kuleta maendeleo kwa nchi yetu, athari hizi hatuwezi kuzikwepa, mabadiliko ya aina yoyote ile lazima yana athari kama hizi, lakini jambo la kututia moyo ni kwamba athari hizi mara nyingi ni za kipinzdi kifupi", amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba..."Mabadiliko ni magumu mwanzoni, yatakuwa machungu yanapofikia katikati, lakini mwishoni matokeo yake ni mazuri au ni matamu, hivyo nawaomba wananchi na watanzania tuvumile katika kipindi hichi cha mpito, baada ya muda mfupi mambo yatakuwa mazuri, lakini hata kama hayatakuwa mazuri hivi karibuni, watoto na wajukuu zetu watanufaika, na huo ndio uzalendo".

Wakati tunaongea kuhusu ubadhirifu bada tunajiandaa kulipia Mabehewa hewa matrioni ya shilingi.

Tulikula za Kivuko cha 1948 na sasa tunapiga tena za vichwa vya train kwa kumlipa ASIYEJULIKANA
 
"Humanity is a very important quality you must have as a leader. If you are humble, if you let people realise that you are not a threat to them, those people will listen to you, those people will embrace you." R.I.P Nelson Mandela.
Fact
 
mimi nina imani sana na raisi wetu, tatizo hii nchi ilikuwa imeoza sana, sasa ndio anainyoosha, lazima muone tofauti, ila kwa tunaetazama mbele zaidi tunaona mwanga, tanzania ijayo itamkumbuka huyu mtu kwa jinsi atakailetea maendeleo,,,, viva magufuli, endelea kukaza
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa?

Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Mara paaah! Game linaanza," Michango ya wahanga wa tetemeko la ardhi Kagera inatumiwa kwa shughuli za serikali, hapo ndipo nliona hata kijiko kinaweza kusonga ugali
 
Tunaelekea kupunguza mafisadi wengi ili tubaki mafisadi wachache tunaoaminiana na kuchanjiwa. Tazama wizara nyeti utagundua
 
mimi nina imani sana na raisi wetu, tatizo hii nchi ilikuwa imeoza sana, sasa ndio anainyoosha, lazima muone tofauti, ila kwa tunaetazama mbele zaidi tunaona mwanga, tanzania ijayo itamkumbuka huyu mtu kwa jinsi atakailetea maendeleo,,,, viva magufuli, endelea kukaza
Nyie ndo wale watu ambao akili zao zimekwamia enzi za ujima
 
Hatujui kwamba ataanza kuboresha kwanza umeme ndo afwate viwanda..

Au aanze viwanda kwanza ndo afwate umeme...
hii ndo Bongoland
Nikuulize tu! alivyokuwa anaomba kura alikuwa anaomba kura za nini? za kwenda kupumzika na mkewe Ikulu kwa miaka 5? unajua wajibu wa Taasisi ya urais na majukumu ya serikali kwa ujumla? umekula maharage ya wapi wewe? nakushauri wahi kwa tabibu wa afya ya akili haraka, hujachelewa!!
 
Hiv kuna mtu anategemea kitu kwa huyu Bwana???
Wapo. Unadhani wale wafaidika wa moja kwa moja wa utawala huu wanamchukia? Wanaomchukia ni wafanyakazi ambao kagoma kuwala nyongeza na wafanyabiashara ambao mzunguko wao umepunguzwa kwa kodi kandamizi
 
Najiuliza hii awamu inajenga au inabomoa nchi? Kila siku nyumba zinabomolewa watu wanabaki bila makazi, watu wanafukuzwa/wanaachishwa, watu wanashindwa kulipa mikopo nyumba zinauzwa, biashara zinafungwa.....
 
Yaaani ni kilio na kusaga meno saiz mungu tuongoze vyema tuifikie 2020 na utupe machaguzi bora sio kama tulivo Kosea awamu hii
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom