"A man should provide for his wife. PERIOD"

"A man should provide for his wife. PERIOD"

Unadhani anyesema hiyo nani? shoga ake mke wangu...kumbe nikichacha huwa wanaambizana......ujue pia kuoa wa dar sometimes kasheshe...
Oh nlidhani anakusimanga live!! Ila huyo shogake mke wako we anakwambiaje hayo mambo???
 
Mwenzenu najisikia kuburudika tu leo............... hii ni special kwa MwanajamiiOne



LOL Ballerina mpenzi mwe aksante sana yaani umenikuna kumoyo........huyu mdada ninavyomzimiaga na huo wimbo wallah leo ntamfurahisha zaidi Mr kwa hisani yako mpendwa lol
 
Last edited by a moderator:
Maisha ya sasa ni magumu ni wanaume wachache sana wanaweza kuwa sole providers na familia ikaridhika kabisa. Na inategemea tunaongelea kuprovide nini. Ndio maana hata masaki wamama wanafuga kuku wakati waume zao wengine ni mawaziri ili siku ya siku wasiumbuke. Na ninawajua wanaume wengi ambao nimeshawasikia wakitamba wake zao wana kazi nzuri unadhani ni kwa nini? Wanajua wamepata unafuu wa maisha. Nani anataka kutegemewa 100%.

Ni sawa unapokuwa single parent unakuwa na wasiwasi kuwa mtoto/watoto wataishije ukifukuzwa kazi. Mume anayetegemewa 100% lazima atakuwa na roho ya wasiwasi kwani ni mkono mmoja na yaweza hata kumsababishia hata pressure maana kuna ambao hata hawawezi sema kuwa wife leo sina pesa.

nyumba kubwa yaani mie huwa nasema namwuomba sana MUNGU anipe ufahamu pamoja na maarifa basi! maisha ya ndoa peke yako kwa kujifanya wajua ni magumu. Shangazi yangu mie alikuwa wa hivyo, nyumba ya shirika, watoto wawili wanasoma, kodi za umeme, maji n.k alikuwa hata hajui ni kiasi gani hulipwa........akiulizwa anasema mume wangu injinia......... (Utafikiri ni injinia pekee Tanzania!) mama mwisho wa mwezi ye anazungumzia akanunue Bazee la bei gani, lesi material ya aina gani maghorofani wamtambue! mama haya kushauri ....baba tufungue kigrosari basi mume wangu ah....ila kila jioni anatoka anakaa kwenye glosari ya shoga yake anampigia simu mjomba atamkuta hapo.....shughuli inaanza kunywa hadi sita usiku. Wanarudi............... wanakujatahamaki maghorofa yameuzwa, shirika limefilisika, injinia yuko juu ya mawe anabangaiza na kazi za wahindi,....kiwanja kilinunuliwa kisukulu enzi hizo mama akasema ni mbali sana, nani akae porini kikauzwa! .........................sasa wamepanga na mama anazikumbuka pesa za Bazee na Lace material.
 
Kwa sie wenye dini ,Toka mwanzo huo ndio ulikuwa mpango wa Mungu.Ila wanadamu huwa tunakuwa na akili hadi tunapitiliza mipango ya Mungu(hivi sasa tunataka ndoa za jinsia moja???).Na mwanamke alipewa kazi ya kuzaa ambayo ni nzito sana.kwa sasa wanawake wanafanya kazi kubwa kuliko wanaume katika familia.
 
Maisha ya sasa ni magumu ni wanaume wachache sana wanaweza kuwa sole providers na familia ikaridhika kabisa. Na inategemea tunaongelea kuprovide nini. Ndio maana hata masaki wamama wanafuga kuku wakati waume zao wengine ni mawaziri ili siku ya siku wasiumbuke. Na ninawajua wanaume wengi ambao nimeshawasikia wakitamba wake zao wana kazi nzuri unadhani ni kwa nini? Wanajua wamepata unafuu wa maisha. Nani anataka kutegemewa 100%.

Ni sawa unapokuwa single parent unakuwa na wasiwasi kuwa mtoto/watoto wataishije ukifukuzwa kazi. Mume anayetegemewa 100% lazima atakuwa na roho ya wasiwasi kwani ni mkono mmoja na yaweza hata kumsababishia hata pressure maana kuna ambao hata hawawezi sema kuwa wife leo sina pesa.


kinachotakiwa ni kwamba hata kama mkeo atafanya biashara
usishindane nae kwa pesa za matumizi ya familia
halafu tukisema ku provide ni mpaka hiyo mitaji ya kufuga kuku
au kumsomesha afanye kazi nzuri ya kipato,but still mume kama una uwezo
provide kila kitu,bila kushindana
 
Baba ndie kichwa cha nyumba awe ana kipato au asiwe nacho nafasi yake haibadiliki.Kama amemzidi mkewe kipato anatakiwa ahudumie nyumba yake lakini hili halimzuii mama kuchangia vitu vidogo vidogo,na pia haipendezi mama kumwomba baba fedha ya c**pi za watoto au kuomba kununulia nguo ilhali wewe ni mfanyakazi.
 
...nasikia 'manukato' ya Ubwana na Utwana hapo, hhhe heh!


Old Skool kind of a wife. Kate, Big Up sana,...nadra sana kupata wanawake wa namna yako
kwa maisha ya kisasa. Ubarikiwe na kujaaliwa kila lililo na heri kwako.
Wakwepa majukumu utawajua tu, hahahaaaaahaaaa
 
kinachotakiwa ni kwamba hata kama mkeo atafanya biashara
usishindane nae kwa pesa za matumizi ya familia
halafu tukisema ku provide ni mpaka hiyo mitaji ya kufuga kuku
au kumsomesha afanye kazi nzuri ya kipato,but still mume kama una uwezo
provide kila kitu,bila kushindana
The boss huu utandawazi umewashika sana baadhi ya watu, mie naangalia tu, mwisho wa siku kila mtu yupo kwake na anaishi anavyotaka yeye
 
Aksante Mzee DC (I hope this time nimepatia LOL) Yaani uko sawa kabisa maana wakati naisoma huyu bwana kakazania kusema kama mwanaume anajijua si mzuri kwa bed basi ajitutumue kuprovide (na hapa ndo linapokuja swali la The Boss je kama hajiwezi kote?) au kama u mzuri sana kwa Bed usiprovide??

Hapo kwenye zawadi Mzee uko sawa kabisa na pia tunachokisahau wanawake wengi ni kuwa tusisubiri tu kuletewa zawadi (kwa wale wenye bahati zao); nasi siku moja moja tumshower na zawadi wajameni. ... itabidi Shantel utupe kitchen party bi dada maana yako mswano!!.
Kwa kweli bibie tufundishane wote tu, nachojua mimi ,wewe hujui na hivohivo wewe unachojua mie sijui, ila kwa kutunzwa tu!mie sisemi sitaki kuumiza watu roho humu, na unaposema unatunzwa sio kwamba ndio umekaa tu kama tunavosema kuna vitu unasaidia, vingine viko indirect sana
 
Kuna dada ni mtu wangu wa karibu, aliolewa na mwanaume baada ya mwaka na nusu karudi kwao na mtoto wake. Kaulizwa kulikoni anamwambia baba yake hawezi kuishi na mume asiye na pesa. Dada babake alikuwa na cheo kikubwa sana though most of the kids walikataa shule including the lady. Kibaya zaidi alikuja na lori amesomba mpaka makochi kisa ni zawadi alipewa siku ya harusi. Babake kamwambia rudisha hivyo vitu haraka sana. Yani mwanaume pesa imeisha na yeye penzi likakata. Mwisho wa siku kapata kibosile ambaye ni mjane na ninavyoandika jamaa kisha dead. Kuna watu wanaamini kuwa mmwanamke lazima utunzwe no matter what.
 
Kuna mdada mmoja aliolewa na jamaa mmoja handsome ana kazi yake na mkewe ana kazi yake, ila mkewe anapata mshahara mkubwa zaidi ya mkewe, dada wa watu alikuwa anajitahidi kuhudumia family including him, kwa kila kitu, jamaa akabweteka kabisa, mwisho wa siku akaanza kutembea na msichana wa jirani yao yaani alikuwa anakaa kwao, basi yule kaka akatafuta chumba na sebule akamweka yule dada, jamani mngemwona huyo dada wa nje alivo mbaya, mngeshangaa,mkewe mzuri maskini, yule mwanaume si akaanza kulala huko kwa mwanamke mara siku moja mara mbili, mpaka navyoandika hapa huyo mke bado anapata tabu na dhiki ya uke wenza, ila kipato anacho, sasa ukimwona hata huwezi jua kama ana pesa, kakonda kwa mawazo,kwa mimi ninavyowaza, mwanaume akikosa pa kuzitumia pesa zake anaweza fanya mambo ya ajabu sana, kama haya pia.hii ni story nayoijua na ni ya kweli.kwa hiyo wadada wenzangu kuweni makini sana na mambo kama haya
 
Kuna mdada mmoja aliolewa na jamaa mmoja handsome ana kazi yake na mkewe ana kazi yake, ila mkewe anapata mshahara mkubwa zaidi ya mkewe, dada wa watu alikuwa anajitahidi kuhudumia family including him, kwa kila kitu, jamaa akabweteka kabisa, mwisho wa siku akaanza kutembea na msichana wa jirani yao yaani alikuwa anakaa kwao, basi yule kaka akatafuta chumba na sebule akamweka yule dada, jamani mngemwona huyo dada wa nje alivo mbaya, mngeshangaa,mkewe mzuri maskini, yule mwanaume si akaanza kulala huko kwa mwanamke mara siku moja mara mbili, mpaka navyoandika hapa huyo mke bado anapata tabu na dhiki ya uke wenza, ila kipato anacho, sasa ukimwona hata huwezi jua kama ana pesa, kakonda kwa mawazo,kwa mimi ninavyowaza, mwanaume akikosa pa kuzitumia pesa zake anaweza fanya mambo ya ajabu sana, kama haya pia.hii ni story nayoijua na ni ya kweli.kwa hiyo wadada wenzangu kuweni makini sana na mambo kama haya

....................Something is wrong somewhere mydia..... either huyo mkaka ana matatizo ya akili au huyu dada unayesema mzuri na mwenye pesa ana matatizo. Lakini kama kila kitu ni sawa ndani sidhani kama mwanaume huyo angethubutu kula na kipofu huku akimvuta (maana huku si kushika) mkono. Yaani ajue kuwa kuna kisima cha pesa sehemu afu akang'ang'anie maji ya bomba!! hapana mwe!!

Inawezakuwa mwanaume huyo anasimangwa na mkewe, au kwa sababu ya pesa basi mwanadada ndo hata huduma nyingine muhimu kwa bwana hatoi au kupata hizo pesa zake inambidi awe buzy kiasi cha kushindwa hata kuwa karibu na mumewe na kuyajua madhila yake. Lakini kwa ishu kama hii mh hatujui huyo tumwonaye mbaya anampa nini pengine ni ile hali ya kumheshimu na kumnyenyekea ambayo inamfanya mwanaume yule ajisikie ni mwanaume ndo ilomfanya aka'fika' bei kwa mtoto wa jirani!.

Masikini pesa sio msingi wa ndoa ingawa ni muhimu kwa kiasi flani!
 
...hivi wewe Babu!, ....hiyo fee uliyoiainisha hapo maana yake ada? mahari? mchango? au?....
halafu,....nikishatoa mahari, makazi, malazi, chakula, mavazi, na matakataka mengine,...kisha huyu mjukuu wako
aka 'laaziz chokileti wa moyoni mwangu' anambie eti watoto tisa wanatosha, pataeleweka kweli?

Itabidi anizalie timu nzima mahari yangu na gharama zirudi!

Aiseee.... hii moskwito ina macho sijapata kuona..... khaa!

Ndo maana japokuwa malaria haikubaliki lakini bado ipo ipo tu............!
 
Ngoja nikonkludi hii sredi ya Mjukuu mtiifu kama ifuatavyo:

A husband should not provide for his wife..... Married couples should provide for themselves......... Hii dhana ya "kuwa mwili mmoja" isiwe kwenye viapo tu bali pia katika utekelezaji.....

Yes: Boyfriends should provide for their girlfriends....PERIOD!

If it is a must for a man to provide for his wife then:
1. Hakuna haja ya kupeleka watoto wa kike shule........ si ataolewa na mwanaume atakaye provide kwake
2. Kina mama hakuna kufanya kazi za kuwaingizia vipato...... wakae nyumbani kutuzalia na kulea watoto wakati sie twahangaikia kuwaprovaidia kila kitu
3. Ile mambo yao ya Beijing ipigwe vita na marufuku. Inakuwaje mnataka usawa wa kila kitu lakini kwenye familia "baba" ndo awe mchunikaji mkuu?

Nimejifunza mengi kwenye hii sredi: Napaswa kumshukuru Mungu kwa kuniozesha malaika. Haka kabibi kenu tunashea 50 fifty. Kipato changu na chake viko hadharani. Anakamata ATM yangu nami nakamata ya kwake. Nadraw kwenye akaunti yake kama yeye anavyofanya kwenye yangu... Tunatumia tutakavyo bila kuhojiana maswali....Haki ya Mungu hakuna raha kama hii......

Leo nikirudi nyumbani, ntampigia makofi matatu ya upendo.
Ngoja nikajipumzishe kitandani.
 
Ngoja nikonkludi hii sredi ya Mbu kama ifuatavyo:

A husband should not provide for his wife..... Married couples should provide for themselves......... Hii dhana ya "kuwa mwili mmoja" isiwe kwenye viapo tu bali pia katika utekelezaji.....

Yes: Boyfriends should provide for their girlfriends....PERIOD!

If it is a must for a man to provide for his wife then:
1. Hakuna haja ya kupeleka watoto wa kike shule........ si ataolewa na mwanaume atakaye provide kwake
2. Kina mama hakuna kufanya kazi za kuwaingizia vipato...... wakae nyumbani kutuzalia na kulea watoto wakati sie twahangaikia kuwaprovaidia kila kitu
3. Ile mambo yao ya Beijing ipigwe vita na marufuku. Inakuwaje mnataka usawa wa kila kitu lakini kwenye familia "baba" ndo awe mchunikaji mkuu?

Nimejifunza mengi kwenye hii sredi: Napaswa kumshukuru Mungu kwa kunioza kwa malaika. Haka kabibi kenu tunashea 50 fifty. Kipato changu na chake viko hadharani. Anakamata ATM yangu nami nakamata ya kwake. Nadraw kwenye akaunti yake kama yeye anavyofanya kwenye yangu... Tunatumia tutakavyo bila kuhojiana maswali....Haki ya Mungu hakuna raha kama hii......

Leo nikirudi nyumbani, ntampigia makofi matatu ya upendo.
Ngoja nikajipumzishe kitandani.

Ukimaliza uende na kwenye ile ya Mwj1 ya Fainali Uzeeni ukakonkludi!
 
Ukimaliza uende na kwenye ile ya Mwj1 ya Fainali Uzeeni ukakonkludi!
Khaaaa!.......... Leo nimeamkia kushoto naona..... kama wewe ulivyoamkia kushoto VoiceOfReason akaitwa babu DC.

naende Edit kabla sijang'atwa na mbu wa malaria.
 
Ngoja nikonkludi hii sredi ya Mjukuu mtiifu kama ifuatavyo:

A husband should not provide for his wife..... Married couples should provide for themselves......... Hii dhana ya "kuwa mwili mmoja" isiwe kwenye viapo tu bali pia katika utekelezaji.....

Yes: Boyfriends should provide for their girlfriends....PERIOD!

If it is a must for a man to provide for his wife then:
1. Hakuna haja ya kupeleka watoto wa kike shule........ si ataolewa na mwanaume atakaye provide kwake
2. Kina mama hakuna kufanya kazi za kuwaingizia vipato...... wakae nyumbani kutuzalia na kulea watoto wakati sie twahangaikia kuwaprovaidia kila kitu
3. Ile mambo yao ya Beijing ipigwe vita na marufuku. Inakuwaje mnataka usawa wa kila kitu lakini kwenye familia "baba" ndo awe mchunikaji mkuu?

Nimejifunza mengi kwenye hii sredi: Napaswa kumshukuru Mungu kwa kuniozesha malaika. Haka kabibi kenu tunashea 50 fifty. Kipato changu na chake viko hadharani. Anakamata ATM yangu nami nakamata ya kwake. Nadraw kwenye akaunti yake kama yeye anavyofanya kwenye yangu... Tunatumia tutakavyo bila kuhojiana maswali....Haki ya Mungu hakuna raha kama hii......

Leo nikirudi nyumbani, ntampigia makofi matatu ya upendo.
Ngoja nikajipumzishe kitandani.

Umerekebisha eh!!

Yaani hapa umefunga mjadala kabisa ila omba nyumba kubwa na Kate wasiingie humu bila kumsahau Mbu......watajakuchopoa huko huko kitandani mwako.

Babu ningekuwa sikufahamu vema na ungekuwa si Babu yangu, hapo kwenye habari ya Bibi ningesema unajipigia pande. PIG UP KWA SANA.
 
Umerekebisha eh!!

Yaani hapa umefunga mjadala kabisa ila omba nyumba kubwa na Kate wasiingie humu bila kumsahau Mbu......watajakuchopoa huko huko kitandani mwako.

Babu ningekuwa sikufahamu vema na ungekuwa si Babu yangu, hapo kwenye habari ya Bibi ningesema unajipigia pande. PIG UP KWA SANA.
Hahahaha.... na hiyo red hapo ndo nani huyo? LOL......... Afu kitimoto kinaletwaje huku kwenye kuprovaidiana?
 
Back
Top Bottom