2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Usiseme kila kitu wakati unajua hana kombe la dunia wala tuzo ya mchezaji bora wa mashindano ya kombe la dunia
Kombe la dunia, wachezaji zaidi ya 500 wanalo.

Nioneshe mchezaji mmoja mwenye magoli 976
FB_IMG_1784728721092.jpg
 
Ronaldo alipendwa Sana Ila ukichunguza Hadi mashabiki wa Manchester na Madrid wamemgeuka kwasabab ya Ego
Njoo leo tujadili kwa upana hii mada kuhusu ego.

Twende kwa ushahidi kabisa halafu mwisho tulime nani mwenye ego na nani mwenye sifa za u-humble wa ku-pretend ilihali ana matukio mengi ya kipumbavu.
 
Umeanza kuchanganyikiwa sasa 🤣 kuchukua WC ni bonus??? Hilo kombe sio NBC ujue, sio UEFA.
Hilo kombe hata mchezaj akikaa benchi tu wakati wa michuano basi ataji feel proud.
Nikuambie tu 2030 Ronaldo atarudi kwenye haya mashindano akiwa kama coaching staff au technical bench au mhamasishaji ili tu aone kama ataweza kubeba kombe
Mbali na FIFA, tumejua ni nani aliyekuwa akiwabeba 2022.

Di Maria ndio aliyekuwa msaada na stats zinaeleza.

Fainali ya 2015 kwenye Copa America Di Maria alitolewa nje dakika ya 29 baada ya kupata majeraha.

Fainali hiyo iliisha kwa Argentina kutolewa.

Fainali ya Copa America 2016 Di Maria alikuwa ametoka kwenye majeraha na hiyo mechi alicheza dakika 50 tu na kutolewa kwasababu hakuwa fit.

Mechi iliisha kwa Argentina kufungwa na kombe likaenda Chile.

Baada ya hapo hakuna fainali yeyote ambayo Di Maria alicheza na Argentina ikapoteza kikombe.
 
Unatumia nguvu nyingi saña kuuaminisha umma kwamba "Ronaldo is the best".

Messi anajipambania umaarufu wake, matendo zaidi.
Ronaldo anapambaniwa umaarufu wake, matokeo kidogo.
Basi ulivyo jikausha, ni kama hakijatokea chochote.

Hivi hii mnaifanyaje mpaka inawezekana?
 
WC si kipimo cha mchezaji kuwa GOAT! bali mafanikio binafsi ya mchezaji na mchango wake katika football vinamfanya awe GOAT, CR7 anastahili kuwa GOAT hata kama hajachukua WC.
Ungewaonesha na hii
FB_IMG_1784364466248.jpg
 
Leo hii mmebadilika 😄😄😄

Wakati Messi Hana WC mlikuwa mnasema Messi Hana hadhi ya kuwa Goat , mwanaume akapambana mpaka wakatwaa WC but Leo hii baada ya kuona cr7 kafeli kupata WC now mmekuja na hivi visingizio Binaadamu bhana 🙌
FB_IMG_1784364466248.jpg
FB_IMG_1784364537589.jpg
FB_IMG_1784364517506.jpg
image.jpg
Screenshot_20260718-122634.png
 
Tujadili sasa stats za Anduje na Ronaldo kwenye mechi walizocheza dhidi ya Spaina.

Naanza na mimi, Ronaldo alikuwa na shot on target 2

Anduje alikuwa na nini?
Kwanza penaldo alikutana na Spain hatua gani?
 
Kwanza penaldo alikutana na Spain hatua gani?
Katika hatua zote Ronaldo amecheza na Spain

Kwenye hii World Cup wamekutana kwenye hatua ya mtoani 16 na Ronaldo aliondoka na shot on target 2 ndani ya dakika 90.

Lakini kwenye fainali pia wamekutana naye mwaka jana ambapo Ronaldo alifunga bao moja.

Na hii fainali ni Portugal ndio aliibuka mshindi.

Tupe na wewe takwimu za Joti.
 
Ukinionyesha mchezaji mwenye Ballon d'or zaidi ya 5, assists zaidi ya 400 na golden balls za kombe la dunia 2 nakuonyesha mchezaji mwenye hayo mabao 976
Ballon d'Or zishapoteza credibility, ni tuzo zinazotolewa kwa connection.

Ballon d'Or za Dwarf nyingi ni robbery mfano 2010 , 2021 na 2023 humo kafanya uporaji wa kiwango kilichoacha maumivu makali sana kwa wachezaji halali waliostahili.

Assist mpaka iitwe assist ni mpaka imfikie mtu ambaye ni bora kwenye ufungaji then afunge, watu 100 wanaweza kutoa pasi katika mazingira sawa ya mchezo ila ni 20 tu wataofanya hiyo pasi iwe goli.

Kwa wataofanikiwa kufunga kwa hiyo nafasi basi pasi hiyo itaitwa assist na kwa ambao watashindwa hiyo itakuwa ni shot on target/off target japo mazingira ni yale yale yanayofanana.

Kwa maana hiyo assist inaonesha ubora zaidi kwa mfungaji kuliko yule aliyetoa pasi.
 
Back
Top Bottom