uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. J

    Nape: Uchaguzi ukiisha wakubwa tunakaa na kumalizana ila wapambe ndio hutaka kutoana roho

    Aliyekuwa mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ameandika katika akaunti yake ya twitter kuwa uchaguzi ukiisha wakubwa hukaa na kumalizana ila kazi inabaki kwa wapambe ambao hupiga mikelele kiasi cha kutaka kutoana roho. Nape anasema " Kuna maisha baada ya Siasa hivyo tupende na kuchukia kwa kiasi"...
  2. J

    GE2020 Je, Uchaguzi utakuwa huru na wa haki hata kama vyombo vya habari vitaendelea na katazo la kutangaza habari kampeni za vyama mbadala?

    Vyombo vya habari kutangaza kwa usawa kampeni za vyama vya siasa ni moja ya vigezo vya uchaguzi ulio huru na wa haki. Siyo sawa hata kidogo kwa CCM kuvikataza vyombo vya habari kutangaza kampeni za vyama vingine vya siasa. Tume ya Uchaguzi inapaswa kuingilia kati suala hili.
  3. Determinantor

    Tathmini: Miezi tisa baada ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 2019

    Wadau, Ni almost miezi Tisa tangu Tanzania ifanye uchaguzi wa serikali za mitaa. Kama mtakumbuka, uchaguzi huu uligubikwa na kila aina ya hila na vituko. Matukio kabla ya Uchaguzi Miongoni mwa matukio ya makubwa ilikua ni pamoja na kuenguliwa kwa Wagombea wa upinzani kwa kigezo cha kukosea...
  4. zeebaba

    Nafasi za kusimamia vituo vya kupigia kura uchaguzi mkuu 2020 zinaombwaje?

    Kuna yoyote ana idea lini nafasi za kusimamia vituo vya uchaguzi zinatoka na je unatuma wapi maombi?
  5. funaku

    Wananchi masikini wapewe kipaumbele kuset agenda za uchaguzi 2020

    Wasalamu! Tumeingia kwenye awamu nyingine ya kusaka viongozi wetu wa awamu ya tano/sita katika ngazi ya Urais,Ubunge na Udiwani. Naipongeza Serikali chini ya Rais Shupavu John Pombe Magufuli kwa kitufikisha hatua hii kwa amani,usalama na Siha njema.Hili halikuwezekana hivi hivi bali kwa...
  6. S

    GE2020 Watanzania wengi sasa wanamiliki smartphone ili kupashana habari za uchaguzi hasa zinazohusu wapinzani

    Kwa wake wanaodhani kuwa kudhibiti vyombo vya habari kuripoti habari za wapinzani kutawasaidia, wajue tu wanajidanganya kwani hivi sasa watanzania wengi wanamiliki smartphone hasa maeneo ya mijini, hivyo watazitumia kupashana habari za uchaguzi zikiwemo habari za wapinzani. Lissu kasema...
  7. K

    GE2020 Mbowe itampa wakati mgumu sana kumnadi Lissu

    Ndugu zangu, Napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa siku ya leo. Katika uchaguzi ambao niliufuatilia kwa karibu kubwa sana tangia nianze kufuatilia siasa na wanasiasa, basi ulikuwa ule wa 2015. Ulikuwa uchaguzi wa kipekee sana kuwahi kutokea hapa nchini, na ulikuwa uchaguzi mgumu sana kwa Chama...
  8. The Palm Tree

    TANGAZO LA AJIRA 12,000 ZA UALIMU TAMISEMI: Ni la kweli au ni magumashi ya CCM na siasa za uchaguzi mkuu tu?

    Takribani wiki NNE au TATU zilizopita waziri wa OR - TAMISEMI Ndg Selemani Jaffo alizungumza na waandishi wa habari... Kati ya mambo mengi aliyozungumza, aliutangazia umma pia kuwa, serikali imeshatangaza AJIRA MPYA ZA UALIMU 12,000 kwa shule za Msingi & Sekondari... Ukiingia katika website ya...
  9. President of China

    Kutoka uwanja wa Uhuru: Tamasha la CCM linalojumuisha wasanii Tanzania

    Nitakuwa nakupatia update. Wasanii wote Tanzania kwa moyo wa upendo walitunga nyimbo kuhusu serikali ya CCM. Wapo katika kufanya mazoezi ya nyimbo zitakazotumika kwenye kampeni ya chama kikubwa barani Afrika CCM.
  10. Relief Mirzska

    Kuelekea uchaguzi mkuu 2020: Je, masheikh wa Uamsho ndio karata ya turufu Zanzibar?

    Habari wadau, Kama ijulikanavyo, Zanzibar waislam ni 99% ya watu wote. Ni nchi yenye idadi ya watu inayokaribia 2M kwa sasa. Kikawaida kwa waislam, wao huwa ni waislam kabla ya mengine yote yaani kama ni utaifa basi wao ni waislam kabla kuwa Wazanzibari, kama ni mambo ya mipira , basi wao ni...
  11. J

    GE2020 Nakuonya Tundu Lissu kuelekea uchaguzi mkuu 2020

    Katika kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu imekuwa kama desturi kwa maadhi ya vyama vya siasa kikiwemo CHADEMA kuendeleza siasa zenye mrengo wa vurungu na uvunjifu wa amani. Ni muhimu sana kama taifa kukumbushana baadhi ya vitu tunapoelekea katika uchaguzi huu maana mchakato upo mwanzoni lakini...
  12. C

    GE2020 Uchaguzi mkuu 2020 na hatma ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

    Kwa hali inavyoendelea na mapokezi aliyopata Maalim Seif Zanzibar uchanguzi kwa upande wa Zanzibar unaonekana utakuwa mugumu kwa CCM na Hussein Mwinyi. Kwa siasa za Zanzibar Kuna uwezekano mkubwa ACT wakashida. Hapa ndo penye shida je CCM wako tayari kukabidhi Zanzibar kwa ACT ? Je, hatma ya...
  13. waterproof

    Nyimbo za wanaharakakati kama kina roma zina mchango gani msimu huu wa uchaguzi?

    Vipi wadau me naona Roma ashushe moja ya kiwanaharakati tumemisi hivyo vitu sana maana sabufa zina vumbi mno
  14. kali linux

    GE2020 Wagombea uchaguzi huu hasa nafasi ya Rais njooni na suluhiso la ajira nchini, leteni sera za kuinua wawekezaji wa ndani

    Hello bosses, Niende moja kwa moja kwenye mada. Ni aibu kuona wanavyuo wengi wanahitimu wakati bado wengine wengi wako mitaani bila kazi au wanafanya kazi za chini sana ambazo hata hawakutegemea(kama vile ulinzi, vibarua, etc....) Ni muda sasa wagombea wetu mje na sera za kutatua tatizo la...
  15. S

    Tundu Lissu alionya kuwa mwaka huu issue si uchaguzi huru na wa haki kwani hilo halipo, bali ni kama tutaendelea kuwa hai na salama baada ya uchaguzi

    Siku moja au mbili kabila ya kurejea nchini,Lissu alihojiwa na chombo kimoja cha habari kuhusu swala zima la uchaguzi na iwapo uchaguzi itakuwa huru na wa haki. Nakumbuka Lissu alijibu kwa kusema:Issue sio uchaguzi huru na wa haki, kwani hilo halitaraji, bali issue ni je,tutaendelea na maisha...
  16. E

    Harakati za kusaka wadhamini zinakiuka sheria ya uchaguzi chapter 343

    Kitendo cha kukodi gari la matangazo kupita mitaani kuhamasisha watu, kuandaa jukwaa na kuhutubia kwa zaidi ya saa nzima huku ukijitapa namna serikali yako itakavyokuwa na kujaribu kukosoa serikali iliyopo madarakani kwangu hiyo ni kampeni, unaposema serikali yangu mtakayoichagua wakati ukijua...
  17. MAHANJU

    GE2020 CCM hatuupendi ukweli, tusione ajabu mgombea wetu akashindwa vibaya uchaguzi huu

    Mara nyingi nimekua nikisema kuwa sisi wana CCM tumekua waoga sana wa kuusema ukweli, ipo siku tutakua kwa aibu maana tukiendelea kutegemea Polisi kama alivyowahi kutuambia Rais mstaafu awamu ya 4 Dr JK. Hivi vyombo kuna wakati vitaamua kusimamia sheria ya nchi bila kuonea mtu, siku wakichoka...
  18. G Sam

    Kumbe uchaguzi wa kwanza kabisa wa Tanganyika mwaka 1960 Mwl. Nyerere alipoteza jimbo moja tu ambalo ni la Karatu, Lissu ameeleza leo

    Picha: Lissu akihutubia Karatu muda huu Leo Tundu Lissu anasema kuwa katika uchaguzi wa kwanza kabisa Tanganyika mwaka 1960, Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere alipoteza jimbo moja tu la Karatu kwa mtu anayeitwa Sarwatt kisha baadaye akaja kuwa mkulima maarufu aliyekamata ndege ya Tanzania...
  19. Noel france

    Watu wasiojulikana ndiyo msingi wa CCM kupoteza uchaguzi huu

    Habari wanajukwaa! Kiukweli uchaguzi wa mwaka huu ni wenye ushindani mkubwa sana, kwa pande zote. Kwa upande wa chama tawala, turufu yao kuu ni ununuaji wa ndege, ujenzi wa miundombinu mbalimbali, pia kuleta mabadiliko ya kiuongozi ndani ya taasisi za serikali. Kwa mfano: Katika baadhi ya...
  20. J

    GE2020 Tume imekataza Viongozi wa Dini kuwa waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2020. Chaguzi zote tangu 1995 viongozi wa Dini walishirikishwa

    Jamani habari ya mjini ndiyo hiyo. Tangu uchaguzi wa 1995 viongozi wa Dini wamekuwa waangalizi wa uchaguzi mkuu. Lakini uchaguzi wa mwaka huu Tume imeamua viongozi wa Dini wasishirikishwe. Nilitegemea kwamba ili malalamiko yasiwepo basi waangalizi walipaswa kuwa wengi. Waswahili tena msemo...
Back
Top Bottom