Kuna hii huduma ya ku trace simu hutolewa na polisi wapelelezi. Kama umepoteza simu au unamtafuta mtu fulani namba yake inakiwa traced kujua yupo wapi.
Utaratibu wa utoaji wa hii huduma umekaa kiwizi wizi sana. Hakuna utaratibu rasmi wa kiserikali. Ni kama mradi wa mtu binafsi au wa serikali...
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamtafuta mzazi anayefahamika kwa jina la Daniel Muga, Mnyaturu ambaye ni fundi ujenzi, mkazi wa Bombambili Ukonga Wilaya ya Ilala kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa miaka mitatu kwa kumpiga na kitu kizito kichwani.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum...
Jeshi la polisi KAZI mnayofanya Sasa hivi inatia kichefuchefu hasa Kwa mtu anayetambua ugumu wa maisha uliopo. Kukamata pikipiki na Bajaji Katika Hali hii ya ukata nikudhibiti Watu wasitafute riziki.
Mmewanyima vijana ajira ya pikipiki na Bajaji matokeo yake wizi umeshamiri Kwa Kasi kubwa Sana...
Wananchi mkoani Njombe wameshauriwa kufika na kutambua mali zilizokamatwa wakati wa doria kutokana na kuibwa nyakati za usiku yakiwemo magodoro, pikipiki, sufuria zinazotumiwa na mama lishe migahawani, mitungi ya gesi, jiko na vingine vingi.
Mali hizo nyingi zimekuwa zikiibwa wakati wa usiku...
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Simon Sirro, mapema leo amefanya ukaguzi wa ghafla kwenye Kituo vya Polisi cha Stakishari, Tabata na Kawe jijini Dar es Salaam.
IGP Sirro amebaini changamoto ya uhalifu wa uporaji kwa kutumia pikipiki pamoja na makosa ya uvunjaji.
“Nimekuwa nikipata...
Mhalifu hawi mhalifu hadi pale itakapothibitika!
Sakata la mfalme Zumaridi (Kiongozi wa kanisa la Zumaridi huko Mwanza) Linaacha midomo wazi kwa wapenda haki na utii wa sheria!
Sipo hapa kumtetea Mfalme Zumaridi, Bali nashangaa namna ya uharamu wa ukamtaji!
Taratibu za ukamataji kwa mujibu wa...
TUKIO LA WAANDISHI WA HABARI KUKAMATWA NA KUPEWA KESI YA MCHONGO ARUSHA.
Waandishi wa Habari wawili wa vyombo vya Habari tofauti mmoja Korumba Victor Moshi na Wa Global Tv na Alphonce Kusaga Wa Tripal A Redio wote wa Mkaoni Arusha walikamatwa na jeshi la polisi mkoani Arusha wakiwa wanafatilia...
Serikali yetu kwa sasa imewapa uhuru sana kitengo cha usalama mpaka imefikia wakati wanavuka mipaka na kushirikiana na wezi au na watu wengine watenda maovu. Polisi kama tunavyoelewa ni kulinda raia na mali zao lkn leo imegeuka imekuwa kuonea raia na kunyang'anya mali zao.
Imagine Polisi...
Kijijini Mjesani, Muheza.
Mzee mmoja alipotea juzi Jumatatu, wanakijiij wakaanza kumsaka.
Leo mchana mwili wake umekutwa shambani, umeharibika sana na umeng'atwa na wanyama.
Wanakijiii wametoa taarifa kwa Polisi wilayani, askari wamejibu watakwenda kesho.
Mwili bado upo shambani.
Habarini ndugu zangu,
Napendekeza tuanze utaratibu wa kuwatembelea askari wetu wa jeshi la Polisi katika vituo vyao vya kazi kwa ajili ya kuwaonyesha upendo, kuwajali na kuwatia moyo katika kazi zao.
Tunaweza kwenda na soda, au juice na kuwagawia kwa kunywa nao na kupiga story zenye tabasamu...
Mahakama Kuu Nchini Nigeria imedumisha uamuzi wa kikosi cha Polisi kumfuta kazi afisa wa polisi wa kike ambaye alipata ujauzito nje ya ndoa mwaka jana.
Jaji Inyang Ekwo amesema hakuona sababu ya kutosha kuvuruga nidhamu ya jeshi.
Kesi hiyo iliwasilishwa Mahakamanina Chama cha Wanasheria wa...
Hakika huyu kamanda Mponjoli ndiye aina ya mapolis wanao hitajika hapa nchini.
Hana cha kuogopa rangi za chama wala diwani wa chama anacho hitaji ni haki itendeke.
Kwa msimamo wa huyu kamanda sijui kama bado yupo au asha staafu.
Msikilizeni na mtupatie mrejesho yuko wapi kwa sasa.
Nchini Zambia madaktari wasio na ajira wameandamana kuelekea Ikulu ya Nchi hiyo ili kufikisha malalamiko yao kwa Rais Hichilema kwa lengo la kujua hatima yao .
Cha kushangaza ni hatua ya Polisi wa nchi hiyo kujitokeza na kuwasindikiza waandamanaji hao kuelekea Ikulu , katika nchi ambayo ni...
Mwanamke mmoja Mkazi wa Kijiji cha Kanyarakata Kata ya Mbuluma Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa, Albetina Mazwile (42) amefariki baada ya kupigwa fimbo katika sehemu mbalimbali za mwili wake na Mumewe na kupelekea kuvuja damu kwa ndani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, William Mwampaghale amesema...
Wakuu naomba muongozo kuhusu misafara binafsi kupewa escort!
Ni vigezo vipi inabidi uwe navyo ili kupewa escort?
Maana siku hizi kwenye foleni kuwekwa pembeni then hiyo misafara ipite ni jambo la kawaida sana!
Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Wakati mwili wa Jacob Elias (44) mkazi wa Milanzi Manispaa ya Tabora anayedaiwa kufariki dunia kutokana na kipigo alichokipata akiwa mahabusu ukizikwa jana Februari 16, 2022, Jeshi la Polisi limekana kuhusika na kifo hicho.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amekana kuhusika kwa...
Wanamgambo wa Al-Shabab wameshambulia vituo vya polisi na vituo vya ukaguzi katika Mji Mkuu wa Somalia, Mogadishu, mapema leo Jumatano Februari 16, 2022.
Imeelezwa kuwa watu kadhaa wamepoteza maisha na wengine 16 wamejeruhiwa. Televisheni ya taifa imeripoti kuwa watu watano wamefariki katika...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limekamata mtandao wa watu 9 ambao wametajwa kuhusika na tuhuma za mauaji pamoja na kuendesha biashara ya mauziano ya viungo mbalimbali vya sehemu ya mwili wa binadamu.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, ACP. RICHARD ABWAO amesema mtandao huo umekamatwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.