IGP Wambura afanya mabadiliko ya Makamanda wa Polisi wa mikoa, Agosti 12, 2022

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,986
FZ93nsWXwAAuqPx.jpg
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Camillus Wambura amefanya mabadiliko madogo kwa baadhi ya makamanda wa Polisi wa mikoa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Agosti 12,2022 na Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime imeeleza kuwa katika mabadiliko hayo, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Pili Omary Mande aliyekuwa Afisa Mnadhimu namba moja mkoa wa Ruvuma anakuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi.

Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Marco Chillya ambaye alikuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi amehamishiwa mkoa wa Ruvuma akichukua nafasi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Joseph Konyo ambaye amestaafu.

Aidha aliyekuwa Mkuu wa Operesheni Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Gaudianus Kamugisha amehamishiwa kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Unguja, akichukua nafasi ya Kamishna Msaidizi wa wa Polisi (ACP) Abdallah Haji Seti aliyehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.
 
RPC Morogoro kashindwa kuzuia madawa ya kulevya maeneo ya msamvu, zinavutwa waziwazi
 
Wambura bado amelala.
Akitaka kupata ufanisi apige chini ma RPC wote na RTO wote chini au abadili vituo vya kazi.
Kawa hali iliyopo atafeli sana
 
huyo naye sijaona alichofanya tangu aapishwe hata kitu kimoja tangible hakuna, suala la kupunguza waomba hela za kubrashi viatu barabarani wala sio lake ni la Kinana, yaani jamaa mweupe sana kuliko hata Zirro mtangulizi wake
 
Back
Top Bottom