KIJANA INUKA
1
Umekaliwa kitako,
Kukwepa tamaa yako,
Wewe na jamaa zako,
Wahisi maisha mwiko,
Ujana ni mlipuko,
Kijana nyosha kiwiko.
Kitamu huwa ukoko,
Kula bila chokochoko,
Unaporemba mwandiko,
Utaukosa mwaliko,
Ujana ni mlipuko,
Kijana nyosha kiwiko.
2
Leo haujahusika,
Kuendana na masika...