Imekuwa kero kupita kwenda soko maziwa na kurudi mnadani Kigamboni kuvuka mpaka upandishe nguo juu wakinamama na wanaume maji yamejaa hayaendi ni shida hakuna wakututengenezea daraja hapo gari zinakwama kupita kwa miguu nayo shida na kipindu pindu hiki hivi wakubwa hamuoni hapo kweli?
Napenda nifahamu sheria zenu mwanafunzi anapokuja kujifunza kwenu mwaka 1 katoka chuo akajifunza kipindi cha miezi 6 akafanya kosa, inawezekana kufukuzwa bila kutaarifiwa wazazi wake?
Kama kafanya kosa mara ya kwanza, mnapiga simu kwa mzazi kuhusu mtoto wake kafanya kosa hili anajaribu...
naomba kuuliza wanaojua nina bima ya afya nimekata march 2023 sh 980000/ sijaitumia mpaka hivi leo mwezi huu wa 9 unaingia.
Nimeenda hospital ya CCBRT kumuona daktari wa mifupa na bima yangu wamenikatalia kumuona mpaka nilete referral namba nawaambia mimi sina hiyo referall namba nataka...
Mimi nina nyumba Chanika jirani yangu anasema nimeingia kwake upana wa nyumba yangu 45 mt lakini nikipima ni 42 mt bado anasema nimejenga kwake. Je, utaratibu upoje wa kupata watu wa ardhi waje wapime watuwekee becon kila mmoja ajue mipaka yake na gharama ngapi? Mwenye kujua naomba anafafanulie.
Naomba kuuliza kwa mtu anaejua kitengo cha moyo Jakaya Muhimbili kuna kijana katoka chuo kasomea mambo ya moyo anataka kufanya intership pale kaambiwa akikubaliwa kwa wiki alipe 1,50000 laki moja unusu kwa wiki.
Je, kuna yeyote anaejua zaidi akatueleza, maana ni pesa nyingi sana mtoto wa...
Tunaomba kujua maji huwa yanatoka saa ngapi jiji la Dar? Tupo Ilala lakini wiki moja sasa sijaona maji yakitoka. Tupeni ratiba tuyangojee kama vile tupo kisimani sasa hivi kijijini na mjini hakuna tofauti au mmeanza kuyafungulia maji kwenye mashamba kama zamani?
mimi namfuatilia sana mh majaliwa ni mtu mwenye kujielewa sana na yupo makini sana kwenye kazi yake kuliko mawaziri wakuu waliopita tabia anafanana na sokoine.
Sijaona au kusikia mh waziri mkuu akimsema vibaya marehemu makufuli sijamsikia kabisa mh majaliwa ni muungwana sana.
Mbali na rais na...
Wanaojua taratibu za kufanya kujua kingingi cha nyumba yako ili utata uishe na jirani. Ndugu yangu amenunua nyumba Ilala mtaa wa Moshi. Hizi nyumba zilijengwa enzi za Nyerere sasa anataka kujua na kupata utaratibu aje apimiwe nyumba yake ajue alama ya nyumba yake ili achane na matatizo na mpemba.
naomba kuwauliza tanesco na waziri mwenye dhamana kwa nini mnatufungia meter fake. mnaondoa meter za kubonyeza mnaleta meter ya remote zina sumbua sana sana kuingiza token namba. Nimefungiwa sasa nina miezi miwili lakini umeme utakapoisha ukiingiza token namba inakataa unaweza ukachukua siku...
Nina jirani yangu tunaelewana vizuri sana ila tatizo akilewa huwa na kelele na mara nyingi ulevi wake kuanzia saa nane usiku anapiga mziki kwa sauti hata mimi jirani yake nakosa usingizi na yeye huanzia nane usiku mpaka saa mbili asubuhi ni mziki na kelele na marafiki zake mchana yeye huwa...
Napenda kujua kwa nini staff wa TANESCO wananunua umeme ofisini?
Mimi nilikwenda pale TANESCO Ilala mkoani kuna dirisha la Teller ambapo Wafanyakazi wote wananunua umeme pale Jumatatu na Jumatano kama sijakosea
Hivi wao wanauziwa umeme bei gani? tofauti na wananchi ? Mwenye kujua anifahamishe
Naomba ushauri ya kutuma pesa India ya matumizi ya mwanafunzi bila kupitia wester union maana wana makato makubwa je kuna kampuni nyingini ya kutuma pesa India?
Tahadharini na tanesco
Jamani serikali imetoa zoezi la kubadilisha mita za luku lakini wafanyakazi wengine wa tanesco wanalitumia hili zoezi kwa manufaa yao wanakuzulia kesi za uongo na wanakuahidi kurudisha units zako hawarudishina wanakuzulia kesi tofauti kama zifutazo:
Hi mita yako mbona ni...
Napenda kuuliza kwa wanaojua na wenye uzoefu: je hizi taasisi unapokwenda kuomba chuo na ukaletewa offer ya chuo mfano gharama ya masomo na malazi $3200 na ilipa hiyo taasisi kwenye acc yake je huwa kuna gharama zao zingine huwa wanakuchaji mbali na hiyo offer au wao hulipwa na chuo kuna...
Wahusika Serikalini tunawaomba sana barabara ya mafao inayotokea Kawawa rd kuingia Uhuru rd Ilala imekuwa na magari mengi sana shida yetu tunaomba mtuwekee taa za kuogoza magari hapa ni kero ukitaka kuingia barabara kubwa ya uhuru hakuna wa kukupisha upite mpaka utegee kosakosa za ajali ni...
Naomba serikali yetu ya mama Samia ifanye juu chini kuondoa vibanda barabarani.
Mji unazidi kuharibika naona wameanza hapo Ilala mtaa wa Uhuru ukuta wa Hospitali ya Amana kuweka vibanda na meza za kudumu.
Sheria zilizotungwa zinatuumiza.
Nilikuwa napiga rangi nyumba yangu nikakamatwa sina kibali cha ujenzi.
Hivi hata kupiga rangi tu kibali? Na kuna sheria ya ku-park gari pembeni ya barabara umewasha hazard unakamatwa hata kama imeharibika.
Watunga sheria hizi ni kina nani?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.