Naomba msaada kwa wale wataalamu wa kuroot simu nina simu aina ya Tecno k7 naitaji kuiroot naweza kutumia njia gani rahisi bila kurumia computer.
Asanteni.
Habari ndugu mimi natumia laini ya ttcl ila kuanzia juzi haisomi kwenye data ninaomba msaada anaefahamu namna ya kuiwezesha ili iweze kusoma data nimejaribu kuwasiliana na ttcl na nimefuata maelekezo yao lakini bado inaonyesha kialama cha R ukiwasha data,asante.
Habari,
Mimi ni mtumiaji wa hii App ya X zamani twitter ila inapotokea inahitajika kuifanyia update inashindikana kwasababu simu yangu ni android version 7.
Halafu ni tecno na sasa hivi hii App inahitaji simu yenye android version 8 na kuendelea na uwezo wa kununua simu nyingine sina sasa kwa...
Habari ndugu,
Naomba msaada nina wiki mbili laini yangu ya ttcl haisomi data pamoja ya kuweka data roaming lakini bado ila kwa wengine inasoma tatizo ni nini! nikiwapigia huduma kwa wateja wananiambia niangalie kwenye setting na hiyo sett iko sawa sasa naomba msaada.
Habari ndugu, ninaomba msaada wa jambo hili,nime-renew namba yangu ya zantel ktk laini ya tigo kama invyofahamika makampuni haya ni mamoja ,tatizo linakuja kwenye data ni kwamba haisomi kabisa nimejaribu data setting za tigo na hata zantel hazionyeshi mtandao kama ni 2g,h+ au 4g ,naomba msaada...
ndugu kwa uzoefu wenu twitter na instagram mtandao upi uko vizuri kufuatilia mimi binafsi natumia zaidi hizi blogs kwahiyo nataka kuingia huko kwenye mitandao ya kijamii,asante.
Wadau habari naomba kwa wale wazoefu wa telegram wanisaidie link nzuri za habari na matukio za ndani ya nchi hata za nje ya nchi na ya michezo hasa ligi ya hapa kwetu.
Asanteni.
habari ndugu zangu kwenye jukwaa hili, ninaomba mwenye kufahamu vitu muhimu vya kuseti kwenye developer options kwa simu inayotumia mfumo wa android na kazi yake,shukrani.
Sent from my TECNO K7 using Gazeti Lite
Habari wanajamii, ninaomba kufahamu kuhusu hii app ambayo inasaidia speed ya kufungua picha kwenye app mfano instagram lakini tatizo linakuja kuna wakati inafanya app nyingine zishindwe kufanyakazi mpaka uitoe au kuna kama kuna app nyingine zaidi ya hiyo naomba kufahamishwa.
Sent from my TECNO...
Wadau naombeni link ya og insta kwa wenye kuifahamu ambayo iko kwenye sasisho jipya (update) maana kila ninayopakua haifungui video, msaada.
Sent from my TECNO K7 using Gazeti Lite
Habari wanajamii nimetumia kwa muda mrefu hii application ya facebook lite sasa nimeona nijaribu kutumia hii nyingine facebook ingawa inachukua space kubwa.
Sasa nimeshtushwa na ulaji wake wa bando maana linakwenda haraka mno ninaomba kama kuna anaefahamu namna ya kuseti ili isile bando sana...
Wadau kwa wale wanaotumia hii App j football tv naomba kujua kama channels zinazonekana kwenye hii app zinafunguka zote maana app yenyewe ni ya malipo kidogo tsh2000 kwa mwaka isiye ikawa ndio wapigaji.
Wadau habari,
Nataka kununua simu duka la tigo, sasa naomba ushauri kati ya tecno spark3 pro na samsung A10s maana zote naona sifa zinafanana.
Nichukue ipi?
Wadau naomba kufahamu,kwenye setting za simu kuna hii kitu restrict app background data,je! ninatakiwa niweke on au off, naomba mwenye kufahamu aniweke sawa kwenye hili,asanteni.
Habari wanajamii,
Ninaomba kufahamu hii Android security patch inasaidia nini kwenye simu sababu kwenye simu yangu huwa inakuja system update ya hiyo kitu.
Shukrani.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.