Zitto Vs Spika

Nakumbuka wakati Zitto was votted out Anna Kilango Malecela alitoka nje akiashiria kutokubaliana na Wabunge wengi wa CCM.Pia nawajua mawaziri kama 5 walikuwa in support of kijana wetu Zitto . Ila John Malecela alimwita Zitto Mwiba . Swali , Je Mzee ES katika hao ulio sema nao na huyu Dr.Malecela umemuonyesha hili ?Maana yeye hakutaka hata maelezo ila kuelekeza Zitto afungiwe .
 
Fieldmarshall Es,
heshima mbele kuu wangu!
No bob hukunielewa, kuongozwa na watu kama Zitto nipo nawe kabisa na gobole nitalibeba tena basi mimi nadhani huyu jamaa ana ubavu sii wa kawaida kabisa isipokuwa tu swala langu kubwa ni wapi kaipeleka ile barua nzito. Kama nimemwelewa vizuri Masatu achana na zile habari za kujitafutia maarufu nafikiri alikuwa hana imani na Spika pamoja na bunge letu ktk hoja hii kuliko Zitto mwenyewe na labda kilichomshangaza yeye ni kwamba ikiwa Zitto hategemei lolote toka kwa Spika ama Bunge then why did he address kule badala sehemu nyinginezo ambazo kuna at least uhakika wa kupata majibu. ndivyo nilivyoelewa mimi baada ya kuchambua pumba toka ktk mchele.
 
Let's lean on each other in order to rescue our beloved country from the hands of Mafisadi and for the benefit of all Tanzanians.
[media]http://www.youtube.com/watch?v=JR0NZqu6igg&feature=related[/media]
 
Sasa Zitto apeleke wapi issues za bunge? Mahakama Kuu? Si itakuwa kichekesho.Mambo ya bunge yapelekwe huko huko bungeni.Tunachotaka kura ya wazi tumjue nani rafiki wa maendeleo na nani rafiki wa ufisadi na kulindana.
 
Pundit,
Ikiwa Zitto kisha tumikia kifungo chake, leo analitaka bunge letu liweke kikao kwa ajiri yake kwa fedha za walalahoi, hivi kweli huoni kama hapa kuna utata kidogo maanake ingekuwa busara sana kama angeyafanya haya ktk kukata rufaa ya hukumu ile.
Tumekwisha toka huko na wananchi tunafahamu kuwa Zitto was right na tumeweza kumuunga mkono kila mahala.
Binafsi barua kama hii angeipeleka kwa JK, copy Bunge kutoa ufafanuzi kwa rais na wananchi maanake kama mbunge alikuwa na haki zote kuendelea kuwawakilisha wananchi wa Kigoma. na muhimu akisema hatua ambazo anataka zichukuliwe dhidi ya viongozi waliojaribu kulipotosha bunge na wananchi. Wabunge wanaweza pendekeza mbunge fulani kujiuzuru kwa kulipotosha bunge na kumbuka pia President ana uwezo na nguvu ya kuvunja hata bunge zima maadam pawe na sababu ya kufanya hivyo.
Ok tuseme Bunge wakubali kulitokea makosa ya taarifa kuwakilishwa na kila mmoja wao ajenge hoja ya kusema nilipiga kura yangu kutokana na ushahidi uliokuwepo wakati huo. Sitta apitishe kuwa hapakuwa na kosa -Then nani wa kumlaumu?... sii ndio yale ya wabunge wa marekani walipopiga kura kuunga mkono vita ya Iraq? leo hii wanashindwa hata kuchomoa na hata yule aliyekubali makosa anashindwa kusema wazi kuwa tuondoke Iraq no more support ya majeshi yetu Iraq isipokuwa wanazunguka tu....Tunachotaka ni hitimisho la swala la Buzwagi hayo ya bunge sisi tayari tumekwisha jua nani mgonvi wetu mpango wa kutubu hauwezi badilisha ukweli.
 
Spika amshangaa Zitto

na Tamali Vullu


SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta, ameeleza kushangazwa kwake na kitendo cha Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, kumuandikia barua akimtaka aiagize Kamati ya Kanuni ya Bunge kupitia upya adhabu aliyopewa.
Zitto alisimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge Agosti 14, mwaka huu, kwa madai ya kusema uongo wakati akiwasilisha hoja binafsi akitaka Bunge liunde kamati kuchunguza, pamoja na mambo mengine, kusainiwa kwa mkataba wa mradi wa mgodi wa Buzwagi nje ya nchi.

Mkataba huo ulisainiwa na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi mapema mwaka huu katika hoteli moja jijini London, Uingereza.

Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Sitta, alisema ingawa bado hajapata barua hiyo, lakini amezisoma habari kuhusu hatua ya Zitto katika vyombo vya habari.

Alisema kuwa baada ya kusoma, hakutegemea barua ya aina hiyo inaweza kuandikwa na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Bado sijapata barua, ndiyo kwanza narejea kutoka India, lakini sikutegemea mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaweza kuandika barua ya aina hiyo, ingawa kila mtu ana uhuru wa kuzungumza.

"Barua hiyo nimeisikia kwenye vyombo ya habari, ina maneno ya ajabu, nasubiri nipate barua hiyo ndiyo nitajua la kufanya," alisema Spika.

Source: Tanzania Daima
 
Nadhani mahakama ya maana kwa mwanasiasa ni wananchi. Katika hili jambo kila mwananchi mwenye akili timamu alisha-make opinion na kutoa hukumu kwamba bunge lilikosea na Zitto alikuwa right. Sasa mimi sioni verdict kubwa na ya maana zaidi ya ile inayotolewa na wananchi.
 
Sita anasema barua ina maneno ya ajabu na hakutegemea kama mbunge anaweza kuandika barua hiyo. Huyu ndiye spika wetu. Nakumbuka mara baada ya kikao cha bajeti kumalizika akiwa na Tido Mhando, Prof Peter Maina na wengine, alisema anamshangaa Dr Slaa kuibua mambo kwenye internet na kuwasukumia tuhuma nzito ambazo hazina uhakika. Nakumbuka Sita akisema kuwa laiti Slaa asingezitoa tuhuma hizo bungeni ambako ana kinga basi watu hao wangempeleka mahakamani. Nilitaraji kuwa baada ya Slaa kuzimwaga pale Mwembeyanga huyu Sita angewahimiza kuwahi mahakamani. Maneno ya Sita ndiyo ya ajabu na ya kushangaza.
 
Nadhani mahakama ya maana kwa mwanasiasa ni wananchi. Katika hili jambo kila mwananchi mwenye akili timamu alisha-make opinion na kutoa hukumu kwamba bunge lilikosea na Zitto alikuwa right. Sasa mimi sioni verdict kubwa na ya maana zaidi ya ile inayotolewa na wananchi.

hii ni generelization , unapozungumzia wananchi unazungumzia wananchi wepi, kwa maana hapa ni katika kuweka sawa kanuni ya mambo kama anavyosema mheshimiwa.

hii itasadia kuleta challenge katika maamuzi mazima ya bunge, iwapo hili litaingia katika rekodi za bunge kwamba bunge limewahi kujirudi kwa kupitia maamuzi yake hamuoni kuwa itakuwa ni tofali jingine katika ukuta wa demokrasia?

hili jambo lina hoja ya kanuni na kwa upande mwingine lina karat ya kisiasa, ambayo ni muhimu kwa mh kuifanya turufu.

guys dont misunderstand the move as if it is ZITO against BUNGE.instead let us view it as ZITTO against breach of rule of law actions. dont you guys see it in this light?
 
115256 said:
Spika amshangaa Zitto


Yaani hiyo ni halali kabisa, lazima Six ashangae, kwani yeye alijua tayali ameisha nyonga (na kuminya) na aliamini so limeisha tulia!!

Sasa anaona ndo kwaaaaanza limezaliwa upya!,. lazima ashangae na afikirie mara tatu tatu, kwani bao alilo jipiga wakati ule wanaweza jiongezea bao la pili wasipo kuwa makini!!

Pamoja na mitazamo tofauti,
Binafsi mi naona Zitto kafanya vyema kabisa, kwani kunyamaza na kuacha bunge liendelee kujikosha kwamba lilicho fanya ni sahihi, japo wananchi tunajua kwamba si sahihi, haitosaidia lijirekebishe, Hii ni nafasi nzuri sana aliyo itoa Zitto kwamba hata bunge lifikie mahali likiri kwamba halikuwa sahihi kama wananchi tunavo jua kwamba halikuwa sahihi!

Na ndo maana kasema kwamba haki isipotendeka hataishia hapa, bado kuna mahali pa kukata rufaa.. sasa hapa bunge lijipime kukubali yakaisha ama lijikaange na kupelekwa muhimili mwingine likahukumiwe huko!

Pamoja na kwamba mahakama ya wananchi ni nzuri, shida kubwa ya mahakama hii utunzaji wa kumbu kumbu zake ni mdogo!! Ndo maana hata hii ya Ufisadi na Dr Slaa inahitaji moto upya, vinginevyo itaanza sahaulika soon!
 
hii
hii itasadia kuleta challenge katika maamuzi mazima ya bunge, iwapo hili litaingia katika rekodi za bunge kwamba bunge limewahi kujirudi kwa kupitia maamuzi yake hamuoni kuwa itakuwa ni tofali jingine katika ukuta wa demokrasia?

Mkuu nafikiri Zitto anaweza kuweka historia kwa kuondoa ushabiki ktk mambo yanayohusu maslahi ya taifa.

Kazi hii ni ngumu hila inaonekana kuwa na mwelekeo mzuri, alichokifanya ni kutii amri halali ya kijeshi(walio kwenda jeshini wanajua hili).

Sasa kamaliza kazi mimi nafikiri hapa ndio muda muhafaka wa kuhoji. Kwa Spika Sita nilitegemea atahamaki napenda waandishi waendelee kumuingiza hili ajimalize mwenyewe.

Angalau sasa baada ya hili badala ya bunge kugeuka kuwa kijiwe cha CCM, litakuwa bunge lenye kujua kuwa ni muhimili mmojawapo ktk nchi.

Moto hule hule, lazima watu wakome kuchanganya maamuzi muhimu ya taifa na itikadi za vyama, mahakamani anatakiwa pia spika afike hili aelimishwe kama hakupata Elimu ya Prof. Shivji au kama ilimzidi uwezo.
 
Bravo Zito kwa hii barua. Hiki ni kitendo kizuri ambacho Zito amechukua ili kuona kwamba Uvundo kama huu hautokei tena. Inabidi Bunge lione na kukubali kwamba lilifanya makosa ambayo hayatakubalika kurudiwa tena kwani ujinga kama huu ndio unaongeza gharama ambazo hazina umuhimu katika kufuja pesa ya walipa kodi.

Hatua kali lazima zichukuliwe kwa wale waliolidanganya Bunge na wa kwanza ni Karamagi.
 
Mi nadhani pia lengo la barua ya Zitto ni kupima pia 'busara' za mheshimiwa spika...je atatumia busara zipi katika hili, kuhakikisha haki inatendeka? kwa mtizamo wangu, kama kauli zake ndo kama zilivonukuiwa na gazeti la Tanzania daima, ninaanza kutilia shaka uwezo na kwa kweli niana madhumuni ya kutumia 'busara za spika' katika kutoa maamuzi nyeti yanayohusu maslahi ya nchi yetu!
 
Pundit,
Ikiwa Zitto kisha tumikia kifungo chake, leo analitaka bunge letu liweke kikao kwa ajiri yake kwa fedha za walalahoi, hivi kweli huoni kama hapa kuna utata kidogo maanake ingekuwa busara sana kama angeyafanya haya ktk kukata rufaa ya hukumu ile.
Tumekwisha toka huko na wananchi tunafahamu kuwa Zitto was right na tumeweza kumuunga mkono kila mahala.
Binafsi barua kama hii angeipeleka kwa JK, copy Bunge kutoa ufafanuzi kwa rais na wananchi maanake kama mbunge alikuwa na haki zote kuendelea kuwawakilisha wananchi wa Kigoma. na muhimu akisema hatua ambazo anataka zichukuliwe dhidi ya viongozi waliojaribu kulipotosha bunge na wananchi. Wabunge wanaweza pendekeza mbunge fulani kujiuzuru kwa kulipotosha bunge na kumbuka pia President ana uwezo na nguvu ya kuvunja hata bunge zima maadam pawe na sababu ya kufanya hivyo.
Ok tuseme Bunge wakubali kulitokea makosa ya taarifa kuwakilishwa na kila mmoja wao ajenge hoja ya kusema nilipiga kura yangu kutokana na ushahidi uliokuwepo wakati huo. Sitta apitishe kuwa hapakuwa na kosa -Then nani wa kumlaumu?... sii ndio yale ya wabunge wa marekani walipopiga kura kuunga mkono vita ya Iraq? leo hii wanashindwa hata kuchomoa na hata yule aliyekubali makosa anashindwa kusema wazi kuwa tuondoke Iraq no more support ya majeshi yetu Iraq isipokuwa wanazunguka tu....Tunachotaka ni hitimisho la swala la Buzwagi hayo ya bunge sisi tayari tumekwisha jua nani mgonvi wetu mpango wa kutubu hauwezi badilisha ukweli.

I hear you Mkandara, basically niliainisha argument yako versus haja ya ku set precedent ya rule of law katika post yangu huko nyuma katika thread hii (relentless resolute vs political tact).

Hufikiri kwamba ni muhimu kuweka precedent as a matter of record, na kufuata rule of law ili kesho wanetu wakitaka kufuatilia mambo hata miaka 10-20/ 100 au zaidi baadaye kuwe na historia kwamba bunge lilishawahi kuchemsha na vichwa vikaona na bunge likajirudi? Au hata kama halijajirudi kwa kiburi motion ya bunge kujirudi ilikuwa tabled?

Hii ndiyo sababu nilisema hili swala linachukua umuhimu mkubwa zaidi ya issue ya Zitto kwa sababu linagusa utaratibu mzima wa jinsi bunge linavyofanya kazi.The CCM dominance in parliament can be unhealthy, this has the potential of checking the unhealthy elements.Vitu vyote viwekwe mezani, tujue nani hasomi miswada, nani anapiga kura kwa utii wa chama, nani CCM lakini mwanamapinduzi wa kweli anayeunga mkono hoja za msingi za wapinzani na kadhalika.

Nafikiri hili ni muhimu.Europe na North America hawajapata maendeleo kwa kuwa content au non-confrontational watu wamepigana ma civil war na ma-revolution kuchinjana katika ma guillotine huko France and so on.Tukiogopa kukwaruzana kwa maneno tena kwenye bunge kidemokrasia tutafika kweli?
 
Spika amshangaa Zitto

na Tamali Vullu


SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta, ameeleza kushangazwa kwake na kitendo cha Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, kumuandikia barua akimtaka aiagize Kamati ya Kanuni ya Bunge kupitia upya adhabu aliyopewa.
Zitto alisimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge Agosti 14, mwaka huu, kwa madai ya kusema uongo wakati akiwasilisha hoja binafsi akitaka Bunge liunde kamati kuchunguza, pamoja na mambo mengine, kusainiwa kwa mkataba wa mradi wa mgodi wa Buzwagi nje ya nchi.

Mkataba huo ulisainiwa na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi mapema mwaka huu katika hoteli moja jijini London, Uingereza.

Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Sitta, alisema ingawa bado hajapata barua hiyo, lakini amezisoma habari kuhusu hatua ya Zitto katika vyombo vya habari.

Alisema kuwa baada ya kusoma, hakutegemea barua ya aina hiyo inaweza kuandikwa na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Bado sijapata barua, ndiyo kwanza narejea kutoka India, lakini sikutegemea mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaweza kuandika barua ya aina hiyo, ingawa kila mtu ana uhuru wa kuzungumza.

“Barua hiyo nimeisikia kwenye vyombo ya habari, ina maneno ya ajabu, nasubiri nipate barua hiyo ndiyo nitajua la kufanya,” alisema Spika.

Source: Tanzania Daima

Viongozi wa Tanzania wananichekesha sana.Sasa wewe mtu barua hujaipokea ushaanza kudakia mambo kutoka press, ukikuta barua iliyochapishwa gazetini ni feki si aibu tupu kwa Spika mzima kujiropiokea mineno tu.

Sitta alivyom-succeed Msekwa nilikuwa nin sigh of relief kwa maana ya kufikiri kwamba we could not possibly get anything worse than Msekwa.Yaani sasa naona ingawa Msekwa alikuwa na michemko yake lakini ukimlinganisha Msekwa na Sitta katika ratio ni sawa na kumlinganisha Nyerere na Kikwete!

Tuliza ball babu, ngojea upokee barua halafu utaongea.HAraka ya nini au ndiyo usongo wa kumtoa nishai Zitto pamoja na ushabiki wa CCM?
 
I hear you Mkandara, basically niliainisha argument yako versus haja ya ku set precedent ya rule of law katika post yangu huko nyuma katika thread hii (relentless resolute vs political tact).

Hufikiri kwamba ni muhimu kuweka precedent as a matter of record, na kufuata rule of law ili kesho wanetu wakitaka kufuatilia mambo hata miaka 10-20/ 100 au zaidi baadaye kuwe na historia kwamba bunge lilishawahi kuchemsha na vichwa vikaona na bunge likajirudi? Au hata kama halijajirudi kwa kiburi motion ya bunge kujirudi ilikuwa tabled?

Hii ndiyo sababu nilisema hili swala linachukua umuhimu mkubwa zaidi ya issue ya Zitto kwa sababu linagusa utaratibu mzima wa jinsi bunge linavyofanya kazi.The CCM dominance in parliament can be unhealthy, this has the potential of checking the unhealthy elements.Vitu vyote viwekwe mezani, tujue nani hasomi miswada, nani anapiga kura kwa utii wa chama, nani CCM lakini mwanamapinduzi wa kweli anayeunga mkono hoja za msingi za wapinzani na kadhalika.

Nafikiri hili ni muhimu.Europe na North America hawajapata maendeleo kwa kuwa content au non-confrontational watu wamepigana ma civil war na ma-revolution kuchinjana katika ma guillotine huko France and so on.Tukiogopa kukwaruzana kwa maneno tena kwenye bunge kidemokrasia tutafika kweli?

Well said Pundit.
 
namnukuuu mheshimiwa ".....ili kuweka rekodi sawa" ,unajua hapa nafikiri mh. ametizama mbele sana, chukulia nchi kama marekani ambako ndo tunajifunza demokrasia, member yeyote wa congress akipiga kura yeyote, hata kama ni miaka 20 iliyopita kura ile haifi, itaendelea kumwandama huko mbeleni, iwapo alisimama upande ambao ulikuwa sawa basi itakuwa ni political advantage kwake, lakini iwapo alisimama katika upande ambao ni unpopular kwa wakati huo zimwi hilo haliachi kumwandama. chukulia mfano mwanamama hilary clinton alivyopiga kura ya kuidhinisha vita ya iraq, leo hii wapinzani wake kina obama hawamwaachii, kila akifurukuta watu wanaleta hoja kwamba wewe si ulipiga kura ya kuidhinisha vita sasa leo unasema nini tena!

ukisikia historia ya mtu inaandikwa vibaya ni katika mambo kama haya,ukisikia jina la mtu linatajwa vibaya katika historia ni kwa sababu wenye mamlaka wakati huo wanakuwa wanatumia rekodi zao kuthibitisha madai yao, mathalani ni nani atakayebisha kwamba ZITTO ni mtovu wa nidhamu miaka 100 ijayo wakati rekodi za bunge zinaonyesha hvyo?

hiki kizazi kinachojua Zito alionewa kitapita,sasa je waandishi wa historia wa vizazi vijavyo watapata wapi kumbukumbu za kuandika historia ya wazee wao kama siyo katika nyaraka?. je ile nyaraka yenye sahihi ya kumwadhibu mh kwa utovu wake wa nidhamu. itakuwa imetoweka wakati huo?.
 
Viongozi wa Tanzania wananichekesha sana.Sasa wewe mtu barua hujaipokea ushaanza kudakia mambo kutoka press, ukikuta barua iliyochapishwa gazetini ni feki si aibu tupu kwa Spika mzima kujiropiokea mineno tu.

Sitta alivyom-succeed Msekwa nilikuwa nin sigh of relief kwa maana ya kufikiri kwamba we could not possibly get anything worse than Msekwa.Yaani sasa naona ingawa Msekwa alikuwa na michemko yake lakini ukimlinganisha Msekwa na Sitta katika ratio ni sawa na kumlinganisha Nyerere na Kikwete!

Tuliza ball babu, ngojea upokee barua halafu utaongea.HAraka ya nini au ndiyo usongo wa kumtoa nishai Zitto pamoja na ushabiki wa CCM?

MKuu Umenichekesha Sana hapa.

Ukisikia mwenzako anaanza kuropoka hujue ameshikwa pabaya
 
Back
Top Bottom