Zitto Vs Spika

Siyo kila kosa linalofanywa na viongozi jeuri wa CCM linahitaji kusuburi mpaka wakati wa uchaguzi ili wananchi wawashikishe adabu. Kwanza tunajua jinsi CCM walivyokuwa na mtandao wa kuiba kura. Hivyo inawezekana kabisa kwamba hiyo 2010 wasiadhibiwe kwa makosa yao chungu nzima.

Nchi ina sheria na kama zinakiukwa basi kuna mahakama ambazo zinaweza kusaidia kujua ni nani aliye mkosaji na adhabu ipi ambayo mkosaji huyo anastahili. Zitto ameonyesha uungwana wa hali ya juu kusubiri mpaka alipomaliza adhabu yake ili kuomba haki itendeke dhidi ya adhabu hiyo. Kuna ushahidi wa kutosha tu kuhusiana na nani alikuwa mkweli katika swala la Buzwagi.
 
Kwanza kabisa pongezi kwa Mheshimiwa Zitto kwa kuwa na humility ya kukubali adhabu, adhabu ambayo kwa mujibu wake hakustahili lakini alikubali ili tu kutii maamuzi ya bunge if I am not mistaken.Discipline ya aina hii, kukubali adhabu hata kama hujakosea na baadaye kuleta appeal zako formally inaonyesha character, serenity na indeed leadership.

Kuna namna mbili ya kuangalia hili suala.

1.) Huu ni wakati wa kwenda na rule of law na kila juhudi ichukuliwe kutafuta ukweli na kama Spika na wabunge wa CCM walikosea inabidi waombe msamaha kwa Zitto na wananchi wa Tanzania.There is no compromising anything that is in the way of the truth and the good fight.

OR

2.) Zitto inabidi a-concentrate kwenye kazi zake za kamati ya madini kwani ripoti itakayojidhihirisha kutoka kamati hiyo inaweza kuwa na nafasi kubwa zaidi ya kudhihirisha nani alikuwa sawa at the end of the day.That this bickering with CCM may not be a productive use of time and resources and may end up making the fight for the truth harder kwani kama tunavyojua "Kigumu Chama Cha Mapinduzi" wote tunajua bunge linatumika kama "rubber stamp" ya chama na serikali, sasa ni muhimu ku concentrate kwenye kazi za kamati especially kwa sababu rais pamoja na watu influential kama Judge Bomani wanaonekana kuwa na confidence na uwezo wa Zitto (at least by the president's appointment and Bomani's public statement).

Now which is which? Uncompromising resoluteness or political tact?
 
At last tunaanza kujadili issues badala ya name calling kama tungekuwa na wana JF wakutosha wa calibre yako tungekuwa mbali sana ktk mapambano haya...

Baadhi ya tabia mbaya za kisiasa walizotufundisha wakoloni, ni pamoja na tabia moja mbaya sana kuliko zote duniani, ya divide and conquer!
 
Zitto kulishitaki Bunge

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuberi Kabwe (CHADEMA), ambaye amemaliza adhabu ya kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kutokana na kusema uongo bungeni, amemwandikia Spika, akilitaka Bunge lipitie upya adhabu aliyopewa.
Ingawa ameahidi kuyaheshimu maamuzi yatakayofikiwa iwapo hatua hizo zitafuatwa lakini haki isitendeke, Zitto ameonya kuwa anaweza kuchukua hatua ya kulifikisha suala hilo mahakamani, ili kuhakikisha anatetea haki yake.

Zitto analitaka Bunge kupitia Kamati ya Kanuni, lipite adhabu hiyo kwa kuwa anaamini kuwa haikuwa ya haki, imemuonea na kumdhalilisha mbele ya macho ya jamii ya Kitanzania na kimataifa.

Anaainisha maombi sita, akiamini kuwa kupitia hatua anazoliomba Bunge kuzipitia, ametoa nafasi kwa mhimili huo wa utawala kujikosoa, kujisahihisha na kujirekebisha kutokana na makosa liliyoyafanya kwa kumuadhibu pasipo kuzingatia kanuni.

"Mheshimiwa Spika, mimi kama mbunge katika Bunge lako, naamini ya kwamba adhabu niliyopewa ilifikiwa kwa shinikizo la kiitikadi na hata kufikia kundi moja la wabunge kutumia vibaya wingi wao bungeni (abuse of majority) na kuniadhibu bila kufuata kanuni za Bunge," anaeleza Zitto katika barua hiyo ya kurasa nne ambayo Tanzania Daima imeiona.

Alipotakiwa na gazeti hili aeleze ni kwa nini ameamua kuchukua hatua hiyo hivi sasa na si kabla, Zitto alisema kuwa hakutaka kuingilia maamuzi yaliyofikiwa ndiyo maana aliamua kumaliza kuitumikia adhabu kabla ya kuchukua hatua hiyo.

Alisema kuwa alikuwa na uwezo wa kwenda mahakamani kutafuta haki yake lakini ameamua kuchukua nafasi hiyo ili kulipa Bunge nafasi ya kujirekebisha lenyewe.

"Nilikuwa na nafasi ya kwenda mahakamani na mawakili wengi walijitolea kunitetea lakini nimeona kufanya hivyo ni kuipambanisha mihimili ya utawala wakati ipo nafasi ya kulipa Bunge nafasi ya kujirudi.

"Nafahamu kuwa upo uwezekano kama ningekwenda mahakamani, ingeniuliza iwapo nimejaribu kufanya njia zozote za kulitatua tatizo hili nje ya mahakama… na ndivyo ninavyofanya hivi sasa, na iwapo itafikia mahali nitaona bado sijatendewa haki, nitakwenda mahakamani nikiwa na rekodi za adhabu ya awali na yatakayojadiliwa katika kamati," alisema.

Aliliambia gazeti hili kuwa, kwa kuwa Bunge ni taasisi ambayo inaendeshwa kwa kanuni, anaamini kuwa safari hii litazingatia kanuni hizo na kubaini makosa yaliyofanyika ili kutoa haki.

Katika maombi yake sita, Zitto analiomba Bunge, kupitia Kamati ya Kanuni za Bunge, kupitia adhabu aliyopewa Agosti 14 mwaka huu na lijiridhishe kama kanuni za Bunge zilifuatwa.

Aidha, baada ya kupitia vifungu vyote na kumsikiliza yeye katika kikao cha kamati, Zitto analitaka Bunge lipitie kauli za viongozi wote wa Bunge na serikali kuhusu adhabu aliyopewa na kuona kama hawakuvunja kanuni za Bunge na sheria namba 3 ya mwaka 1988.

"Kama Bunge likiridhika kuwa matamshi ya viongozi niliowataja yanakiuka kanuni za Bunge, kwa hali yoyote ile, basi wapelekwe katika kamati husika ya Bunge," anasema.

Pia, mbunge huyo kijana, anataka iwapo itabainika kuwa kulikuwa na makosa katika kumuadhibu, basi Bunge limuombe radhi kwa kumpa adhabu isivyo halali.

Pia analitaka Bunge lijutie maamuzi liliyoyachukua na kuahidi mbele ya jamii kuwa halitarudia kuvunja kanuni za Bunge kwa makusudi na kumuadhibu mwakilishi wa wananchi mwingine bila makosa.

"Bunge liahidi kuwa kamwe haitatokea mbunge kuonewa kwa sababu za kiitikadi au kukomoa na kupiga marufuku vikao vya kamati za vyama vya siasa ndani ya Bunge kupanga njama za kuadhibu wabunge bila makosa," anabainisha Zitto katika ombi lake la sita.

Akieleza kwa nini anaamini kuwa dhabu hiyo haikuwa ya haki, Zitto anasema kuwa hatua za kumuadhibu hazikufuata kanuni za Bunge, hazikuzingatia tamaduni za Bunge na kubwa zaidi hazikumpa nafasi ya yeye kujitetea.

"Muda wa kuwasilisha hoja yangu, ambao kwa masikitiko makubwa, viongozi wa Bunge mmeuelezea kama ndio muda niliopewa kuthibitisha maneno yangu, ni muda wa kikanuni ambao niliomba mimi ili kuleta hoja binafsi na wala si muda niliopewa kuthibitisha jambo lolote," anasema.

Akichanganua kanuni, Zitto anabainisha katika barua hiyo kuwa Bunge lina taratibu za kuleta hoja bungeni ambazo zimefafanuliwa kinagaubaga katika kanuni ambazo zinaanisha wazi kabisa kuwa hoja haiwezi kutolewa juu ya hoja nyingine na kwamba muda wa kutoa taarifa ya hoja umewekewa utaratibu ndani ya kanuni za Bunge.

"Kanuni zetu zinasema wazi kabisa (59-3) kuwa iwapo mbunge anashutumiwa kusema uongo bungeni, au kutoa lugha ya kuudhi, atapewa muda ili kuthibitisha hili analoshutumiwa.

"Mimi Mheshimiwa Spika, si tu sikuwahi kushutumiwa kuserma uongo, bali pia wewe binafsi unajua sijawahi kupewa muda kuthibitisha chochote," anasema Zitto.

Anaongeza kuwa alisimamishwa kwa kusema uongo bungeni, lakini hajaelezwa mahala popote uongo huo ni upi.

"Mbaya zaidi baadhi ya viongozi wa Bunge, ukiwemo wewe Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Katibu wa Bunge mliendelea kuonyesha kuwa dhabu ile ni sahihi na kuwaaminisha wananchi kuwa mimi ni mbunge muongo.

"Vile vile viongozi wa upande wa serikali, akiwemo waziri mkuu, mawaziri na manaibu mawaziri wamenukuliwa na vyombo vya habari wakisema mimi ni muongo kufuatia adhabu hiyo," anasema.

Anasema kuwa licha ya kumdhalilisha yeye kama mtu binafsi, adhabu hiyo ni ishara mbaya sana kwa demokrasia ndani ya Bunge. Alisema angependa kuona Bunge likiheshimika na ndiyo maana akaamua kuitumikia adhabu yote na kutotoa kauli yoyote iliyoingilia mamlaka ya Bunge kuhusiana na dhabu hiyo.

"Mheshimiwa Spika, ombi langu hili mbele yako ni muhimu sana katika kulifanya Bunge lijiangalie na kujirekebisha, kama inabidi, pale ambapo litakuwa limekosea. Hii itasaidia kuepuka makosa kama haya siku za usoni," anasema Zitto.

Agosti 14 mwaka huu, wakati wa kikao cha bajeti, Bunge lilimsimamisha Zitto kuhudhuria vikao vya Bunge kutokana na hoja iliyotolewa na Mbunge wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir, akidai kuwa Zitto alikuwa amelidanganya Bunge katika hoja yake binafsi aliyoiwasilisha awali.

Katika hoja hiyo binafsi, Zitto alikuwa analitaka Bunge liunde kamati teule kuchunguza hatua ya Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, kusaini mkataba wa mradi wa mgodi wa Buzwagi nje ya nchi.

Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge wengi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao siku hiyo hiyo walipitisha azimio la kumsimamisha mbunge huyo.
 
well, hii move ya Mh. Zuberi Zitto nadhani ameicheza katika wakati muafaka, wote tunafahamu, ukipuliza moto ili uwake hupulizi mara moja. tena unapuliza kwa interval.

hapa tusiangalie Zitto as Zitto per se, kama an object of the move, bali tuangalie misingi ya accountability itakayowekwa na move nzima.

Huwezi kusema unaendesha mambo kwa kanuni na taratibu halafu unazivunja kanuni hizo unless umezivunja kwa bahati mbaya, lakini hata kama umezivunja kwa bahati mbaya uking'amua kwamba ulikosea huna budi kukiri kuwa ulikosea na wakati huo ukijaribu kuweka mambo sawa ili ikiwezekana usikosee kosa la namna hiyo tena na tena.

Kumcriticize mh. kwa move, ambayo mosi ana haki nayo kutokana na yeye kuwa mhanga wa maamuzi ambayo ana imani hakutendewa haki ni zaidi ya kutomtendea haki. unataka wananchi wa Kighoma waliomchagua mh .Zuberi Zitto waamini kwamba mbunge wao ni muongo kwa hiyo hafai?.

Pili as a politician, wakati wowote wa kugrab opportunity haipaswi kuiachia hivihivi. Nyerere alipata kuishinda hoja ya serikali Tatu kwa kurejea katika kanuni tu za chama, G55 na mahoja yao mazito wakakwama kuvunja hoja ya kanuni za chama. sasa sembuse leo kanuni za bunge ndo zivunjwe?.

Tatu, popote pale katika mihimili yote mitatu ya uongozi, kunahitajika changamoto, na hii ndiyo dhana nzima ya demokrasia, kutoitumia demokrasia vizuri hatuwezi kumlaumu yeyote, leo hii tukiendelea kutoa changamoto za kuiweka mihimili yote hii katika msitari ulionyooka ni matumaini yangu kutakuwa na umakini katika maamuzi yanayohusu maslahi ya umma.

Simba na nguvu zote alizonazo kofi moja halimwangushi nyati. Wapinzani wanatakiwa kuweka presha na kwa calculated timing.
 
Lunyungu, kama ungejibizana ma mjinga ningekuelewa maana ipo siku angeelewa. Si huyu Masatu... Huyu ana sifa yake na jina lake jingine, nahapo ndipo upeo wake ulipoishia. Ndiyo maana wenye akili wamemuacha tu abwabwaje!

Kazi kweli kweli..... hata kwa mijeledi tutafika tu.....
 
Lunyungu, kama ungejibizana ma mjinga ningekuelewa maana ipo siku angeelewa. Si huyu Masatu... Huyu ana sifa yake na jina lake jingine, nahapo ndipo upeo wake ulipoishia. Ndiyo maana wenye akili wamemuacha tu abwabwaje!

Kichwamaji,

Hivi hii ni hoja ya manguvu au ni nguvu ya hoja. Hata kama hukubaliani na Masatu basi toa hoja yako lakini kuanza kutumia lugha kama hiyo hapo juu, sioni kama inatusaidia kuelemishana kwenye hii mijadala.

Mijadala ya siasa sio hesababu, hakuna mwenye jibu sahihi, hivyo ni vizuri tukapambana kwa hoja, dataz, facts nk. badala ya kuanza kutumia lugha ambazo kwa kweli naamini hata wewe usingependa mtu azitumie kwako.
 
shukurani mkuu kwa kutuwekea barua hii. Aidha nakupongeza kwa changamoto unazozitoa katika kutetea uchumi wetu na uimarishaji wa demokrasia nchini.

napenda kuuliza, na naamini jibu laweza kutolewa na mwana jf yeyote, jee sentensi hii haiwezi "kaburi ya hoja yako"?
Dar es Salaam.
24/12/2007



Spika wa Bunge,
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dar es Salaam.



BUNGE KUPITIA UPYA ADHABU DHIDI YANGU

...Nimeona, kwa kuwa demokrasia inakua nchini kwetu, ni vema niliombe Bunge kupitia upya adhabu ile na kama Bunge kupitia kamati ya Kanuni za Bunge likiona Kanuni za Bunge zilifuatwa nitaridhika na adhabu ile. Vile vile kama Bunge likiona kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa kanuni za Bunge, kwa bahati mbaya au kwa makusudi, basi niombwe radhi...

Kabwe Zuberi Zitto (Mb)
Mbunge wa Kigoma Kaskazini.


Nakala

1. Katibu wa Bunge
2. Kiongozi wa Upinzani Bungeni

jee ni kitu gani kitazuia kamati kufanya kazi yake kiitikadi?

mola ibariki nchi yetu
 
Kafara swali lako ni zuri sana, na huu mjadala unaweza kugusa kitu kizito kuliko hii issue ya Zitto. Mjadala huu unaweza kugusa ukomavu wa kanuni za bunge katika mazingira ya demokrasia yavyama vingi.

Kama bunge linaweza kuchukua maamuzi ya "kiitikadi" (as I understand, to act in the interest of CCM and not necessarily of the truth or reforms) basi zichukuliwe hatua za makusudi kubadilisha kanuni za bunge ili kusiwe na mianya ya abuse ya kanuni hizi .

Inabidi tuelezwe wazi kwa nini bunge linafikia maamuzi yake, kwa kutumia vipengele gani.Na zaidi ya hapo, kama vipengele vinaonekana haviko fair inabidi viondolewe na vibadilishwe tutumie vipengele vinavyo-evolve na mazingira ya upinzani wa vyama vingi.
 
Masatu I fully agree with you, but look the bigger picture comrade, Tanzania is not an NGO neither is it a private property. Kwamba haki haitatendeka na majority ya CCM I agree we dont need to be Einstein kujua hili, lakini jee tuache tuu hivyo hivyo? mkuu kwamba mahakama imejaa rushwa kwa hiyo wahalifu tuwahukumu wenyewe au kuwachoma moto can not be a right approach katika REPUBLIC yoyote. Kuna kipindi unajua fika kabisa kwamba nikimshtaki fulani polisi au mahakamni ataachiwa, lakini unaamua kwenda maana hapa unadeal na nchi na wala sio kampuni ya mtu binafsi.

Zitto anaweza asiachieve chochote kama unavyosema, lakini mere fact kwamba amepeleka malalamiko kwa Spika it will make a difference hata kwenye records na archives za bunge miaka mia ijayo vizazi vyetu vitasoma jinsi babu zao walivyokuwa wanaendesha mambo kwa kuoneana na kulindana. kifupi history will be made. Kwamba approach ya Slaa ya kwenda Mwembe Yanga ni nzuri, Yes-sometimes, lakini sio kila swala linaweza kuhukumiwa na kupatiwa ufumbuzi mwembe yanga au Jangwani.

Mkuu rushwa na uzembe vimejaa kote lakini hiyo haimanishi kwamba hizo sheria tusizifuate au tusizitumie tunapokuwa na haja. huwezi amua kumchoma moto kibaka simply because unaamini kwamba ukimpeleka polisi ataachiwa huru kwa sababu za rushwa! utakuwa hujamtendea haki! Anything wrong with our laws and that mode of justice? Perhaps! But for now, we have to live with it!


...........thats why I Love JF kwani watu wenye upande wa pili wa shilingi huwa accomodated............WELL SAID MASANJA!!.......nafikiri mwenzetu Masatu atakuwa ameelewa
 
Hapo ndio linakuja swala la katiba mpya ambayo hata Warioba amelipigia debe na CCM haitaki kabisa kulisikia kwa sababu Katiba mpya inaweza kabisa kupunguza nguvu ya Rais kwa kiasi kikubwa. CCM wanajua siku zote Rais atakuwa ni CCM hivyo kumpunguzia nguvu Rais anayetoka CCM ni kukipunguzia nguvu CCM.

Wana vision fupi sana hawa jamaa hawataki kuangalia mbali na kuona katiba mpya itakuwa ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali wanatoka chama kipi.
 
Moreover,

God forbid siku rais akitoka chama kingine na bunge likawa la CCM what a constitutional showdown!
 
Mkuu Zitto, na Wakuu wote JF, toka ulipoiweka barua yako hapa nimewa-forwardia wakuu wengi wetu wa serikali na hasa unaokutana nao bungeni na wanaoijua ishu yako vizuri zaidi, yafuatayo ni yale waliyoniambia kulingana na the ishu na barua hii yako, na kwenye hili ni lazima niwe mkweli kuwa walikuwa wakiniambia very arrogantly, tena wengine ni wale ninaoita vinyonga waliokuwa wakikusifia recently,

Kwamba, eti bunge likisha aamua kama lilivyokwisha amua on your ishu, ina maana kwa maneno mengine automatically inakuwa ni sheria, kwa hiyo on your ishu walishapitisha sheria, ili kui-un do it, ambayo ni one of the legal condotion ya kuijadili tena hii ishu bungeni, kunahitajika majority ya kura 2/3 za wabunge, ambao ndio hasa waliopitisha mswaada in the first place, yaani wa CCM, kiongozi mmoja ananiambia eti, hawa wabunge wa CCM watakuwa wamepewa dawa gani ambayo imewabadilisha in only two months, baada ya kupitisha kwa kukubaliana na uamuzi uliokusimamisha bunge, kwa maneno mafupi wanasema uwezekano ni none.

Sawa nimewasikia kama messenger, lakini ninasema hivi haina maana usijaribu, please keeep it up na kuna ambao tuko nyuma yako na tutaendelea kuwachokonoa tu, maana you ill' never know kunaweza kutokea majority huko bungeni wa kuku-support hoja yako ambayo abayo pia ni yetu wananchi wote na taifa zima.

Ahsante Wakuuu.
 
Moreover,

God forbid siku rais akitoka chama kingine na bunge likawa la CCM what a constitutional showdown!

Kama wapo pale kwa manufaa ya Tanzania basi watakuwa wanafanya maamuzi kwa manufaa ya Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao, na hivi ndivyo Watanzania wengi tutagemea toka kwao.

Wakiweka mbele maslahi ya vyama vyao badala ya nchi wanaweza kuiangamiza nchi katika janga kubwa.
 
Zitto,

Kazi nzuri...wote tunajua bunge lilicheza rafu lakini namna ulivyokwenda nayo hii issue ni classic katika siasa za nchi yetu. Endelea kuonyesha njia, demokrasia yetu bado ni changa sana..Mungu awe nawe.

Wana JF

Masatu ameonyesha kukomaa kufikiria alichofikiria, inanishangaza kuona wana JF wengi hivyo imewachukua (na wengine bado) hawajamuelewa.

Forum idumu.
 
Wanabodi,
Mimi nadhani swala la Masatu ni zuri na wazi kabisa kuwa kuna utata mkubwa ktk barua ya Zitto hasa inapokwenda kwa spika wa Bunge ambaye kwa kutumia kiti chake na back up ya wabunge asilimia 90 wa CCM uamuzi wa kwanza ulitokea.
Kweli kunahitajika maelezo zaidi na kubaini nani alomweka jela Zitto na katumikia kifungo chote!... sasa anapohitaji DNA kuhakikisha kuwa sii yeye alohusika na atafutwe witness wa uongo aliyesababisha kifungo hicho huwezi kuipeleka kesi kwa hakimu yule yule ambaye anafahamu kabisa alitumia ubabe nje ya sheria kumweka kifungoni Zitto.
Sielewi njia gani bora ingetumika lakini labda kupitia kwa rais na barua ya waiz kama hii tungetarajia kusikia at least tofauti kidogo kuliko kuipeleka kesi ya Nyani kwa nyani mwenyewe..acha huyo ngedele!
Labda nachoweza kusema ni kwamba Masatu anapoingia huwa anakuja na UCCM kwanza badala ya kuwa muwazi na kuziweka point zake ambazo zinahitaji kutazamwa kwa umakini.
Hata swala ya Mafisadi, nakumbuka Dr. Slaa aliweza kuliondoa Bungeni kwa sababu kama hizi na kuliweka wazi kwa wananchi .. kishindo chake kiliweza kuonekana tofauti kabisa na kama angeendelea kufikiria kuwa Bunge letu linaweza kuwa against waajiri wao sidhani kama habari hii ingekuwa na uzito, utata ulokuwepo hadi Balali kakimbia nchi.
Muhimu wa kijiwe hiki mbali na tofuti zetu nadhani ni muhimu sana tuwe na mtazamo wenye malengo ya kumkomboa Mtanzania...sikatai kabisa Zitto kupigania haki yake kama mwakilishi wa kijiji cha Kigoma na kupata ufumbuzi wa haki yake kimsingi kama mbunge lakini bado kabisa swala letu la Buzwagi limetanda ukungu mkubwa, halijapatiwa jibu hata kidogo na pengine kukubali kwake kuwa ktk kamati hiyo mpya ni dhahiri kuwa Mheshimiwa JK atakuwa na wakati mgumu zaidi kujibu barua kama hii ikiwa yeye mwenyewe ndiye kitovu cha balaa lote bungeni.
 
Hapa inabidi kuwe na transparency.

1.Hoja iwekwe bungeni ili kupigiwa kura.(kuna haja ya kubadilisha hiyo 2/3 majority kwenda kwenye simple majority)

2.Kura isiwe ya siri, ili tujue mbunge gani amepiga kura vipi.Ni muhimu tujue voting records za wabunge wetu.Hii ni moja ya evolutions tunzozihitaji katika bunge letu.Sio tunakuwa na wabunge ndumilakuwili wanaosema sana kumbe ikija wakati wa kupiga kura wanapiga vingine.

Bunge litakuwa na nafasi ya kuonyesha kukomaa kisiasa na kujirudi pamoja na kumuomba Zitto msamaha au kuonyesha arrogance.In either case inabidi tujue kila mbunge anavyopiga kura, kusiwe na kura ya siri kuhusu hili jambo hapo tutajua priority za kila mbunge zilipolala, kama priority ni taifa au CCM.
 
Pundit kama ingalikuwa ni kumchuna mbuzi basi kisu umekipeleka hadi kwenye mfupa kama ni bomu umepiga ikulu. Ukisema haya CCM wanaogopa mno maana wanajua watu wa JF ni think tank ya nchi achana na wale wao wanaokaa nao kule .
 
Wanabodi,

Mimi nadhani swala la Masatu ni zuri ....
Labda nachoweza kusema ni kwamba Masatu anapoingia huwa anakuja na UCCM kwanza badala ya kuwa muwazi na kuziweka point zake ambazo zinahitaji kutazamwa kwa umakini. .

point taken
 
Mimi nadhani swala la Masatu ni zuri na wazi kabisa kuwa kuna utata mkubwa ktk barua ya Zitto hasa inapokwenda kwa spika wa Bunge ambaye kwa kutumia kiti chake na back up ya wabunge asilimia 90 wa CCM uamuzi wa kwanza ulitokea.

Mkuu Heshima mbele Bob,

Wa-Tanzania, tayari tumewekewa mfano mzuri sana na mwamba Mtikila, kuwa hata kama wako 90%, na mahakama ni zao, lakini kuna wakati wanaweza kuzidiwa na ukweli, kutoka kwa wananchi, in general ninaiona hoja ya Masatu, kuwa ni kukubali kushindwa kabla ya kuanza, hatuwezi ku-afford that in Tanzania tena kwneye kipindi hiki cha Mikatba ya Buzwagi,

Ni lazima wananchi tukiongozwa na kina Zitto, tu turn up the heat every corner na kwenye every ishu, regardless ya umuhimu au matarajio ya matokeo ya any ishu, kwa sababu experience inatuonyesha tukisema na kuwazomea, huwa wanasikiliza.

Mkuu Zitto, keeep it up the pressure mkuu, leo nimepata dvd za Patrice Lumumba, Mobutu-King Of Afrika, na Idd Amin Dada-1974, ambazo nilikuwa nimeziagiza muda mrefu sana, ninaingia sasa kuziangalia kwa makini kuona nini cha kujifunza huko.
 
Back
Top Bottom