Zitto Vs Spika

Nimpongeze class mate wangu mheshimiwa Zitto kwa barua hiyo, lazima ahakikishe kuwa haki inatendeka. Binafsi sitarajii sisiemu kama chama ama wabunge wake, ama spika kuomba radhi na kuonesha kuwa walikosea katika suala zima la adhabu kwa mbunge huyu, hata kama kosa lao limeoneshwa wazi na Kikwete, kwamba wapi walichemka na inabidi warekebishe. Kamati waliyoipinga bungeni ndio hiyo Kikwete kaiunda kwa mlango wa nyuma. Sio hulka ya sisiemu kujikosoa, kwa mtazamo wao, wao wako sahihi kila wakati.
Pamoja na hayo, na uwingi wao katika bunge hii haumfanyi Zitto kutokupeleka barua yake kwao kwa kuhofia kuwa itatupwa kapuni, hata kama wataikalia ama hawataifanyia chochote, cha muhimu ifike kwa wahusika. Hatuwezi kufika popote kama tutakuwa na mawazo mgando na ya kukata tamaa kama ya mheshimiwa Masatu katika pointi yake hapo juu, kwamba Zitto anapoteza muda. Hakuna muda unaopotea hapo, lazima haki itendeke.
Long live Zitto!
 
Masatu I fully agree with you, but look the bigger picture comrade, Tanzania is not an NGO neither is it a private property. Kwamba haki haitatendeka na majority ya CCM I agree we dont need to be Einstein kujua hili, lakini jee tuache tuu hivyo hivyo? mkuu kwamba mahakama imejaa rushwa kwa hiyo wahalifu tuwahukumu wenyewe au kuwachoma moto can not be a right approach katika REPUBLIC yoyote. Kuna kipindi unajua fika kabisa kwamba nikimshtaki fulani polisi au mahakamni ataachiwa, lakini unaamua kwenda maana hapa unadeal na nchi na wala sio kampuni ya mtu binafsi.

Zitto anaweza asiachieve chochote kama unavyosema, lakini mere fact kwamba amepeleka malalamiko kwa Spika it will make a difference hata kwenye records na archives za bunge miaka mia ijayo vizazi vyetu vitasoma jinsi babu zao walivyokuwa wanaendesha mambo kwa kuoneana na kulindana. kifupi history will be made. Kwamba approach ya Slaa ya kwenda Mwembe Yanga ni nzuri, Yes-sometimes, lakini sio kila swala linaweza kuhukumiwa na kupatiwa ufumbuzi mwembe yanga au Jangwani.

Mkuu rushwa na uzembe vimejaa kote lakini hiyo haimanishi kwamba hizo sheria tusizifuate au tusizitumie tunapokuwa na haja. huwezi amua kumchoma moto kibaka simply because unaamini kwamba ukimpeleka polisi ataachiwa huru kwa sababu za rushwa! utakuwa hujamtendea haki! Anything wrong with our laws and that mode of justice? Perhaps! But for now, we have to live with it!
 
Msameheni Masatu yuko hapa kwa kazi ya kupinga pinga hata kama kuna ukweli wa 200% lakini anapinga kwa kuw akaetwa kupinga hapa .Mawazo dhaifu yako Masatu yana kudhalilisha .kwa jinsi ninavyo kujua na uwezo wako wa kujua mambo muda wote nimekaa kimya najiuliza je huyu ni Masatu aka....... ninaye mjua ama ni nguvu ya Mlungula na kukosa uzalendo ?
 
Masatu,

Sasa umekuwa kwenye mtazamo ambayo unamwelekeo mzuri, si ile unasema ati Zitto kaona umaarufu umeisha anaibuka na hili kuufufua.
Kwa maoni yangu hatua hiyo aliyochukua pia inasaidia kuleta changamoto kwa bunge, kwani si wote wameoza humo..anaweza ku nock some sense kwa baadhi na mambo yakaonekana tofauti na kusaidia baadaye hiyo taasisi kuwa makini mara nyingine. Pia ile ya kwenda mahakamani au kwa wananchi ni nzuri lakini Zitto yeye kaonelewa afanye kurekebisha sio kubomoa hilo bunge letu. Struggles kama hizo za Zitto ni constructive na hatimaye huzaa matunda, zinahitaji kuungwa mkono.
 
Pamoja na hayo bado naamini mlango wa Mahakama uko wazi na anaweza kwenda muda wowote kama ataona Bunge linakalia issue . Ni vyema aanzie Bungeni ili Mahakama isije pata kisingizio cha yeye kuto kuanzia Bungeni .
 
Masanja hata nami naungana na wewe na maelezo yako mengi tu. Labba nianze kwa kusema suala la kuhukumu wezi mitaani kwa sababu tu tunajua hatuwezi kupata sheria mahakamani nami pia nalipinga, lakini mkuu ktk hili la Zitto ni zaidi ya hapo.

Mengi yamesemwa kwenye mikutano na forums na kila mtu anajua kuwa uamuzi ule ulikuwa ni wa kionevu, kinachoni kereketa mimi hapa ni kuona Zitto anataka kulifanya jambo hili kama mtaji wake wa kisiasa, na kusahau kuwa anaendeleza yale yale maana ushakuwa mduara sasa kuanzia hoja binafsi, maelezo ya Zitto, maelezo ya waziri, azimio la kumfungia, mikutano mwembe yanga, jangwani na mikoani na sasa tunarudi tena bungeni. Kitu cha muhimu kujua hapa ni haya yote yana gharimiwa na sisi walalahoi!

Mimi nadhani hapa tujaribu kuwa na 3D approach in our assessment on this saga. Kama historia kwa vizazi vijavyo mbona ishaandikwa na kila mtu analijua hilo sasa. Ndio maana nikasema approach ya Dr Slaa ni nzuri zaidi yeye kaenda kwenye mzizi badala ya matawi, tuwashtaki hawa mafisadi kwa wananchi wananchi watawang'oa bungeni na baadae kwenye urais then tutafika lakini kwa mtindo huu wa kuwarudishia kesi wajihukumu "wenyewe" Im afraid to say tunacheza mduara.

Lunyungu

Hayo ndio yanaitwa mawazo hodhi.. unadhani vita hii ya ufisadi ni yako wewe na wengine wachache la hasha.. ur missing the point na ndio maana utabaki kusema "nimetumwa" nimepewa mlungula and other name calling bs usidhani ni vita yako peke yako tupo wengi labda bahati mbaya sana approach zako mwenzetu ni too amateurish!

Una haki ya kusema na kudhani utakavyo!
 
Hili suala lipo crystal clear ni upotezaji wa muda. Hivi tunategemea nini kutoka ktk Bunge lenye kutawaliwa na over 90% CCM? Huhitaji kuwa rocket scientist kujua hili.

Mkuu wangu, baada ya Zitto kusimamishwa bunge, kumetokea sauti nyingi na hasa ndani ya CCM zikidai kuwa alionewa, na kwamaba alikuwa na haki katika madai yake na kanuni za bunge hazikufutatwa kwenye kumsimamisha, moja kati ya hizo sauti muhimu kwa taifa letu ilikuwa ya Mama Anna Makinda, naibu Spika wa bunge letu pamoja na Mkurugenzi wa Maelezo nchini Judge Bomani, na makamu wa CM Msekwa,

Sasa ni wakati muafaka wa ku-test hizo kauli zao, kama zilikuwa ni kweli au walikuwa wanajaribu ku-ride kwenye political air na wananchi wengi ambao kwenye ziara ya Viongozi wetu wa CCM kuwaweka sawa wananchi, they made it clear to them kwa kuwazomea kuwa they agreeed with Zitto and Dr. Slaa, kuwa madini yetu yanahitaji better handle than what our current government was doing,

Sasa ni wakati muafaka ka Zitto, kutafuta haki ambayo sio yake tu, bali tunahitaji a future legal pattern ya bunge ambayo ni sambamba na consistent, according to our constitution, ndio maana ninasema kuwa kitendo cha Zitto, kuandika hii barua sasa ni wakati muafaka kabisa, ili tuone kina Msekwa watafanya nini na maneno yao waliyoyasemahivi karibuni, je walikuwa serious au walikuwa wanjaribu kutafuta cheap political umaarafu na wananchi?

Mkuu the big picture hapa ni taifa letu, sio Zitto wala CCM, isipokuwa ni taifa la kesho, tutawaambia nini watoto wetu Masatu, kuwa tuliogopa kuwauliza wakubwa tuliowachagua wenywe kutuongoza eti kwa sababu wao walikuwa 90% ndani ya bunge? Mkuu Masatu kichwa kama wewe this makes a sense kweli kwako?

Bravo na long live Zitto, na fikra zako mkuu zidumu!
 
Masatu what solid evidence do you on your claims kwamba Zitto kaona umaarufu unaisha na kaanza kuleta hoja ambayo kwako unaona haina msingi ? Is this the way yo fight Ufisadi ? Unataka nikuamini kwa hili na nisidhani kwamba unatumiwa ama uko kazini kulinda kitumbua chako ? Umeona hoja hapo juu ? Ok Bunge lina wengi wa CCM ambao tunasema ni mafisadi lakini siamini kama wote wameoza . Je unajua ni wabunge wangapi wa CCM na baadhi ya Mawaziri wanao Muunga Zitto mkono kwa harakati zake ?
 
ES & Lunyungu,

Mbona mnai over-look nidhamu ya chama? wanaweza wakawepo wabunge wengi wa CCM wenye ku sympathize na Zitto kwa nia njema tu lakini inapofika mahala pa ku-stand and be counted ndio kimbembe...
 
Mbona mnai over-look nidhamu ya chama? wanaweza wakawepo wabunge wengi wa CCM wenye ku sympathize na Zitto kwa nia njema tu lakini inapofika mahala pa ku-stand and be counted ndio kimbembe...

Kwa hiyo mkuu Msatu, unasema wananchi Millioni 40, tusifanye kitu ka sababu tu ya hii argument yako mkuu? Kwamba kwa sababu viongozi hawawezi kusimama wahesabiwe basi tusiwabughudhi hata kama ni faida ya taifa letu la baadaye?

Kweli unasema hii ni right approach mkuu?
 


Kwa hiyo mkuu Msatu, unasema wananchi Millioni 40, tusifanye kitu ka sababu tu ya hii argument yako mkuu? Kwamba kwa sababu viongozi hawawezi kusimama wahesabiwe basi tusiwabughudhi hata kama ni faida ya taifa letu la baadaye?

Kweli unasema hii ni right approach mkuu?

Mkuu sie wananchi Milioni 40 tumewachagua wawakilishi 300 na ushee kule Bungeni hao ndio ninawazungumzia kuwa hawawezi ku stand up and be counted.

Solution ya hii ipo ktk posts zangu za awali yaani kufuata Dr Slaa approach kuwashtaki hawa wawakilishi wetu kwa hao Mil 40 ili tuwang'oe.

Hope its clear now
 
Can the parliament undo what it has already done and implemented? Is this matter not overtaken by event?. can 'kamati ya kanuni' overrule what was decided by the whole sitting National Assembly? is 'uamuzi wa spika' which can be reviewed by Kamati ya kanuni under the cited kanuni same as uamuzi wa bunge? aside from politics let us brainstorm on what may become a contentious legal issues.
 
Solution ya hii ipo ktk posts zangu za awali yaani kufuata Dr Slaa approach kuwashtaki hawa wawakilishi wetu kwa hao Mil 40 ili tuwang'oe.

Hope its clear now

Yaah! solution yako iko clear, lakini binafsi ninaiona kuwa inapaswa kuwa the last resort, maana hatuwezi kukaaa from now mpaka to the next 3 years tukisubiri uchaguzi wa hao wawakilishi wetu 300, hapana ni lazima in the meantime tujaribu kila njia kwanza ikiwa ni pamoja na hii ya Zitto, kabla ya kufikia uchaguzi

Otherwise nimekuelewa mkuu, lakini kusema Zitto, anajaribu kuufufua umaarufu uliofifia kwa kuwauliza watawala kuangalia upya sheria za bunge na kama haki ilitendeka, naona on your part ilikuwa ni understatement mkuu na kumkatisha tamaa katika kipindi hiki kigumu ambachi taifa letu tunawahitaji viongozi wanaoweza kusimama wahsabiwe kama yeye!

Sina sababu yoyote ya suspicion in Zitto's actions, kwa sababu tayari rais wetu ame-cave in kwenye madai yake kwa kukubali kuanzisha kamati ya madini, sasa dawa ni kuendelea ku-push the envelope, badala ya kutafuta easy na short cut solutions za uchaguzi, ambazo bado kuna miaka mitatu zaidi, maana in his 3 years, tukinyamaza kimya hawa viongozi wetu wanaweza ku-inflict more damages kwa taif letu, pamoja na kwamba they are doing it anyways, lakini ni lazima tuendelee ku-push tu!
 
Masanja hata nami naungana na wewe na maelezo yako mengi tu. Labba nianze kwa kusema suala la kuhukumu wezi mitaani kwa sababu tu tunajua hatuwezi kupata sheria mahakamani nami pia nalipinga, lakini mkuu ktk hili la Zitto ni zaidi ya hapo.

Mengi yamesemwa kwenye mikutano na forums na kila mtu anajua kuwa uamuzi ule ulikuwa ni wa kionevu, kinachoni kereketa mimi hapa ni kuona Zitto anataka kulifanya jambo hili kama mtaji wake wa kisiasa, na kusahau kuwa anaendeleza yale yale maana ushakuwa mduara sasa kuanzia hoja binafsi, maelezo ya Zitto, maelezo ya waziri, azimio la kumfungia, mikutano mwembe yanga, jangwani na mikoani na sasa tunarudi tena bungeni. Kitu cha muhimu kujua hapa ni haya yote yana gharimiwa na sisi walalahoi!

Mimi nadhani hapa tujaribu kuwa na 3D approach in our assessment on this saga. Kama historia kwa vizazi vijavyo mbona ishaandikwa na kila mtu analijua hilo sasa. Ndio maana nikasema approach ya Dr Slaa ni nzuri zaidi yeye kaenda kwenye mzizi badala ya matawi, tuwashtaki hawa mafisadi kwa wananchi wananchi watawang'oa bungeni na baadae kwenye urais then tutafika lakini kwa mtindo huu wa kuwarudishia kesi wajihukumu "wenyewe" Im afraid to say tunacheza mduara.

Lunyungu

Hayo ndio yanaitwa mawazo hodhi.. unadhani vita hii ya ufisadi ni yako wewe na wengine wachache la hasha.. ur missing the point na ndio maana utabaki kusema "nimetumwa" nimepewa mlungula and other name calling bs usidhani ni vita yako peke yako tupo wengi labda bahati mbaya sana approach zako mwenzetu ni too amateurish!

Una haki ya kusema na kudhani utakavyo!

Mkuu Masatu,

Mimi nakuelewa una maana gani lakini ni ngumu kwa watu wengi kukuelewa kwasababu ya mapenzi na mara nyingi tunaangalia jambo kwa black and white.

Ila tu mimi naona approach wanazotumia Zitto na Dr. Slaa zote zinafaa. Dr. Slaa ni mtu mzima, busara nyingi na umakini mwingi na anawafunga kamba mafisadi taratibu, wanaotaka kujiokoa hujikuta wananaswa zaidi na zaidi kama samaki mjanja kwenye wavu.

Mapambano ya Dr. Slaa hayawezi kufanikiwa bila nguvu ya vijana kama Zitto. Huyu ni jemadari, anasema give me my machine gun, I want to fight, hawa ndio akina Zuma wetu ambao bila kukubali kupambana na kuwa tayari kujitoa mhanga, hatuwezi kufanikiwa, wala akina Dr. Slaa hawawezi kufanikiwa.

Demokrasia ina gharama zake na kinachoendelea sasa ni sawa na mzunguko lakini pia unaweza kuwa muarobaini wa siasa ili kusafisha bunge na pia kuwaumbua hawa viongozi wetu ili wajue maamuzi yasiyo ya haki wanayochukua, kuna siku yanaweza kuwatokea puani. Ni bora tuendelee na mduara wetu mpaka kieleweke.

Zitto anaweza kufaidika na mapambano haya, lakini atakayefaidika zaidi ni sisi wananchi ambao tumechoka kuburuzwa.
 
Mkuu Masatu,

Mimi nakuelewa una maana gani lakini ni ngumu kwa watu wengi kukuelewa kwasababu ya mapenzi na mara nyingi tunaangalia jambo kwa black and white.

Ila tu mimi naona approach wanazotumia Zitto na Dr. Slaa zote zinafaa. Dr. Slaa ni mtu mzima, busara nyingi na umakini mwingi na anawafunga kamba mafisadi taratibu, wanaotaka kujiokoa hujikuta wananaswa zaidi na zaidi kama samaki mjanja kwenye wavu.

Mapambano ya Dr. Slaa hayawezi kufanikiwa bila nguvu ya vijana kama Zitto. Huyu ni jemadari, anasema give me my machine gun, I want to fight, hawa ndio akina Zuma wetu ambao bila kukubali kupambana na kuwa tayari kujitoa mhanga, hatuwezi kufanikiwa, wala akina Dr. Slaa hawawezi kufanikiwa.

Demokrasia ina gharama zake na kinachoendelea sasa ni sawa na mzunguko lakini pi unaweza kuwa muarobaini wa siasa ili kusafisha bunge na pia kuwaumbua hawa viongozi wetu ili wajue maamuzi yasiyo ya haki wanayochukua, kuna siku yanaweza kuwatokea puani. Ni bora tuendelee na mduara wetu mpaka kieleweke.

Zitto anaweza kufaidika na mapambano haya, lakini atakayefaidika zaidi ni sisi wananchi ambao tumechoka kuburuzwa.

Mtanzania

At last tunaanza kujadili issues badala ya name calling kama tungekuwa na wana JF wakutosha wa calibre yako tungekuwa mbali sana ktk mapambano haya... any way acha twende hivi hivi tutafika tu
 
Mawazo ya busara? nani Six huyu huyu au mwingine?

Hapa hakuna lolote ni wastage of time and resources Zitto ushaona mtaji wako wa umaarufu unafifia umeona bora uufufue upya!!

Good try mate....

Lunyungu, kama ungejibizana ma mjinga ningekuelewa maana ipo siku angeelewa. Si huyu Masatu... Huyu ana sifa yake na jina lake jingine, nahapo ndipo upeo wake ulipoishia. Ndiyo maana wenye akili wamemuacha tu abwabwaje!
 
Back
Top Bottom