Zimbabwe: The turmoil, reconciliation, and the future!

Zimbabwe: The turmoil, reconciliation, and the future!

Mugerezi,
Mimi mtazamo wangu juu ya mkutano huo ni tofauti kidogo. Na hapa I am just reading between the lines. The fact kwamba Mbeki amechaguliwa azungumze na pande zote---upinzani na serikali ya Zimbabwe---ni dalili njema. Kumbuka zamani tulikuwa na kanuni (OAU) ya kutoingilia mambo ya ndani ya nchi mwenzako. Sasa hiyo kanuni imepitwa na wakati, and that is a good thing. Hatuwezi kukaa kimya tena wakati jirani anampiga mwanae au mkewe. Hatuwezi kukaa kimya wakati mawakala wa Mugabe wanaendesha mkong'oto dhidi ya wapinzani. And that is a good thing.Ukijumlisha maneno ya Mwanawasa na hatua ya kuteuliwa Mbeki, ni dhahiri kuwa Mugabe aliwekwa kiti moto, albeit diplomatically.
 


HALI YAKO MWANANGU FREEMAN, NAFIKIRI HAUJAMBO NA UNAENDELEA VIZURI NA MASOMO YAKO.KWA KIFUPI NI YAPATA WIKI SASATOKA NIMEREJEA NYUMBANI TOKA UINGEREZA NILIPOKUWA MATIBABUNI.

KIJANA WANGU NAONA UNAVYOPAMBANA NA KUJITAIDI KUONYESHA KWAMBA WEWE HAUKUBALIANI NA EFFORT ZOZOZTE ZINAZOFANYWA NA SERIKALI ILIYOPO MADARAKANI KATIKA KUTATUA LILE TUNALOLIITA TATIZO LA SIASA YA NDUGU YETU NA MWANA MAPINDUZI WA KWELI. NIRUHUSU MIMI NIMWITE........" TRUE SON OF AFRICA".

REJEA KAULI AU MAANDISHI YAKO KATIKA SITE ILIYOPO JUU. UMEZUNGUMZA MENGI NDUGU YANGU LAKINI MIMI NINA MASWALA MACHACHE AMBAYO NINGEPENDA UNITABAISHIE ILI TUPATE KUKAA SAWA KATIKA HUU MJADALA JAPO KWAMBA MENGI YAMEZUNGUMZWA.

WEWE ULIKUWA UNATAKA URAISI WA TANZANIA NA JE UNGEFANYA NINI KATIKA HILI LA ZIMBABWE?

NAULIZA HIVI SABABU UNAONEKANA KWAMBA KWAMBA KIMAWAZO NI KAMA WALIVYO WENZETU WA KULE WEST.

NI KOSA GAI AMBALO JAKAYA AMELIFANYA KATIKA HARAKATI HIZI.NINI UNAHITAJI KUJUA ZAIDI YA HAYA YANAYOTOKEA SASA HIVI.

MIE NAFIKIRI UTULIE UANGALIE MAMBO YANAVYOWEKWA SAWA. NINA IMANI MUAFAKA UTAPATIKANA.ACHA USHABIKI WA SIASA NA ANGALIA JUHUDI MADHUBUTI .

MUNGU IBARIKI AFRICA NA MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Wazee Heshima mbele,

Maraisi 15 walikutana hapa bongo kuzungumzia ishu za nchi zao na hasa umoja wao wa kusini, Zimbabwe ilikuwa ni moja ya ishu zilizozungumziwa,

Zimbabwe ni nchi huru kama zilivyo nchi zingine zote za dunia, inao uhuru wa kufanya itakavyo kwa mujibu wa sheria za nchi hiyo, hakuna nchi yoyote nyingine duniani yenye uwezo wa kuiambia kuwa sheria zake hazifai, Rais Kikwete, hana uwezo wowote kisheria zabongo wala za kimataifa kuingilia shughuli za kisiasa au kisheria kwenye nchi huru ya Zimbabwe,

Mugabe ni rais aliyechaguliwa kuwa rais wa nchi kwa mujibu wa katiba za nchi hiyo, anachohitaji sasa hivi ni ushauri wa nini cha kufanya wakati ardhi ipatayo 95% ya Zimbabwe imo mikononi mwa wazungu, huku wazawa yaani wazimbabwe wenyewe wanamiliki only 3.5% ya ardhi yao wenyewe, yeye kama rais wa nchi anatakiwa kuwaambia nini wananchi wake? Kwamba faida ya wao kupigania uhuru wa kuikomboa nch yao ilikuwa ni nini?

Wazungu kama kawaida yao wamepiga kelele sana kuhusu huu mkutano, na kutushambulia sana na hasa rais wetu, lakini wazungu hawa wanashindwa kufanya lolote kuhusu Iran na utengenezaji wa nyuklia, wazungu hawa wanasema ni sawa Israel kuwa na bomu hilo, lakini sio Iran, halafu wazungu hawa majuzi tu wanajeshi wao 15 wamechukuliwa na Iran, mpaka leo hawajafanya kitu, WHY? kwa sababu wanajua kuwa sheria za kimataifa haziwaruhusu kufanya lolote Iran inapodai kuwa sheria zake zilivunjwa na wanajeshi hao wakizungu,

Je Zimbabwe ingekuwa ndiyo imewashika wanajeshi hao 15 ingekuwaje? Matatizo ya Zimbabwe ni ya wa-Zimbabwe wenyewe na yatatuliwa na wazimbabwe wenyewe, wakihitaji msaaada wataziomba nchi za Afrika kwanza ziwasaidie, tumechoka na wazungu na unafiki wao, kama upinzani Zimbabwe wamevunja sheira za nchi hiyo, Muuugwana hawezi kuwasaidia,

na wazungu wanyamaze watuachie Afrika yetu, maana wao wanaweza kuwakamata watu Afaghanstan na kuwaweka rumande Cuba against sheria zote za kimataifa, vijana tuwe waangalifu na hizi propaganda za wazungu
Mzee Es comments zako nzuri sana. Lakini wazungu hawa inatakiwa uwacategorize maana ukisema wazungu tu generally inakuwa kidogo siyo fair. Tunajua kuwa hawa jamaa hawatumind ila wanataka kutunyonya hilo halina ubishi lakini inapokuja issue ya maisha ya watu hapo watu lazima waseme.

Mfano unaposema kuwa mambo ya wazimbabwe waachiwe wao ni sawa lakini kumbuka kuwa kule zimbabwe jamaa wamebanwa hawana pa kujitetea. Pia inatakiwa ifahamike kuwa hata sisi waafrica tuna kasoro zetu tusiseme wazungu tu. Zimbabwe inasema jamaa wamevunja sheria! Ok je wamepelekwa mahakamani? Maana mtu ukifunja sheria unapelekwa mahakamani. Pia tulishaona kwamba walitaka kumfuta jamaa kwenye ramani kwa kumbambikia likesi! Hayo yote yanatosha kuonyesha kuwa jamaa kule wanabaniwa. Huo ndiyo ukweli.

Issue ya guantenamo inajulikana lakini si wazungu wote wanao support hiyo issue. Naweza nikasema hata sisi waafrica hatujafanya kitu kwani sini mamember wa UN body yenye final say lakini kiko wapi!! USA inaogopwa thats why kama ulivyosema kama ingekuwa zimbabwe kuhusu wale wajeshi ingekuwa issue. Pia ukumbuke inawezekana pia hao wajeshi wakafanywa chambo kuichokonoa IRAN kuona itafanya nini maana mateka wa kivita hawauawi.

Wazungu wanaweza kunyamaza iwapo tu tutaacha kuwategemea otherwise tuwapige chini tuanze moja. Ni sawasawa na home mtoto anaweza kujifanya kidume lakini akikumbuka kuwa mzee ndiyo kila kitu anaufyata mpaka ajiweze.

Aksanteni tupo pamoja
 
Chief Ihunyo, Salamu Toka Kwa Wasukuma Na Amani Ya Masanja Na Majebele Iwe Nawe.

Nimeguswa Na Maandishi Yako!

Nini Zaidi Ya Habari, Mrithi Wa Kiti.
 
Kwa mtazamo wangu binafsi, sidhani kama Mbowe amekosea kumkosoa Muungwana, WHY ? Because he can ! Thats right, hata kama International Relations hayapandi ( which i doubt ) still nadhani ni busara kwake kumkosoa mtu anapokosea, after all yule mzee has to get off power maana amekaa muda mrefu na hana jipya lolote au sijui anataka wazimbabwe waulize viongozi wake wapo wapi, na jibu la mugambe andhani litakuwa "TUPO TUMEJAA TELE"..... sasa hii wapi na wapi.

One thing is, yule mzee sidhani kama ana mtandao mkubwa wa kuogopwa kiasi kwamba hata wengine waweze kumuogopa hivyo ! Sitoshangaa nikiona wazee walafi wa madaraka wakispend the rest of their lives JELA !!

HALI YAKO MJUKUU WANGU MPINZANI WA WANA MLENGO WA KIMAPINDUZI.

NAOMBA NITUMIE SALAMU MAMBO VIPI......

SAMAHANI KAMA NITAKUWA NAKUCHOSHA , JE HAYA NDIYO ULIYOKUWA UNATAKA SEMA AU VIPI?

MIE NAKUAMBIA NAOMBA NA WEWE UKAFANYE SHULE KIDOGO. MAANA NAJUA MDOGO WANGU HAUJUI HATA INTEREST INAHUSU NINI NA KWA NINI TANZANIA IPO PALE....KAMA UNAJUA NAOMBA UNIELEKEZE MIMI BABU YAKO MASANJA WA MAJEBELE.

KARIBU SANA, MWANA KADA MPINZANI.
 
Tupo pamoja jasusi. Hope so kuwa jamaa alibanwa. And if that is the case matunda yatakuwepo.
 
Leo nita waacha wengine nanitasema neno moja tu kwamba Hapa ndipo Mwalimu angali ifanay Africa iwe na heshima . Mwalimu angalikuwa jibu la huu mgogoro na Mugabe angalipewa vidonge kwa uwazi na si unafiki wa JK .watu wanaumia sisi waafrika tunawaona watawala wakoloni kama wamefanya jambo la maana . Mugabe need to to be told lakini hakuna katika genge la wapenda madaraka anaweza kumweleza.
 
Mzeeshughuli Bwana,
nina wasiwasi mkubwa sana kama Mwalimu angekuwa na msimamo tofauti na huu wa viongozi wa Kusini mwa Afrika. Raisi Kaunda, rafiki mkubwa wa Mwalimu, na mshiriki wa mazungumzo ya Lancaster House, amekuwa akitoa kauli ambazo ni "sympathetic" kwa Mugabe. Raisi Ben Mkapa, chaguo la Mwalimu, na mshiriki wa mazungumzo ya Lancaster House, naye amekuwa mkereketwa mkubwa sana wa Mzee Mugabe.

Binafsi napendekeza kwamba Mugabe ampishe Mzimbabwe mwingine aongoze. Ninasema hivyo kwasababu Zimbabwe hawana nguvu za kiuchumi kujiamulia na kuendesha mambo yao wenyewe. Wanategemea WAKUBWA--nchi za magharibi. Nchi hizo zimekataa kufanya kazi na serikali itakayoongozwa na Robert Gabriel Mugabe.

Wakubwa wakiamua kukushughulikia wanaweza kusambaratisha nchi nzima bila huruma kwa wananchi wa kawaida. Rejea yaliyowakuta Wacongo, na Raisi wao Laurent Kabila. Wakubwa walikuwa wanamlazimisha Kabila aruhusu makaburi ya Wahutu waliouawa yafukuliwe kule Goma. Zaidi walikuwa wakimlazimisha aitishe uchaguzi kabla hata nchi haijatulia.

Wakati mvutano wa kuitisha uchaguzi na kufukua makaburi ukiendelea, Kabila alishikwa "wendawazimu" akasitisha mikataba ya madini ya nchi za magharibi, na kuamuru askari wa Rwanda waondoke ktk ardhi ya Congo. Kabila aliamuru Wanyarwanda waondoke kwasababu walikuwa hawana nidhamu, na zaidi kuruhusu uchunguzi kufanyika kuhusu mauaji ya kiimla dhidi ya Wahutu waliokimbilia Congo.

Maamuzi ya Kabila yaliwakera sana Wakubwa, wakasahau kuhusu yale makaburi walimozikwa wahutu, na kuamua kumshughulikia Mzee Laurent Kabila. Huyu Kabila mtoto aliporithishwa madaraka kitu cha kwanza kufanya ilikuwa ni kwenda kusujudu kwa wakubwa na sasa Congo pameanza kutulia.

samahani kwa kuserereka nje ya topic. habari hii nimeileta kwasababu naamini ili kuinusuru nchi yao, WaZimbabwe, na Mugabe, wanaweza kujifunza toka kwa Wacongo.
 
Niamini Mwalimu hakuwa na mzaha na wapuuzi kama Mugabe .Mwalimu alipenda watu wa Afrika na si watawala wa Kiafrika kama Mugabe na JK
 
Sipendi kusema sana lakini naona tunauangalia huu upatanishi wa Mgogoro wa Mugabe Vs Wapinzani (MDC) kwa Mtazamo Finyu.Katika Timu yote ya Viongozi wa SADC hakuna mwenye Ubavu wa kumwambia lolote Mugabe!!.Kwa Mtazamo wangu ni Mwanawaswa (Zambia) tu,ambaye anaweza kumwambia ukweli huyu Mzee,ilishawahi kutokea huko nyuma,na Mwanawaswa alimwambia Mugabe wazi kuwa anakiuka haki za Binadamu.Huyu Mzee kwa ukorofi wake akafunga Barabara kuu iendayo South Africa.
JK ni muoga na mnafiki hawezi kabisa kumkemea Mzee Robert,kwani Mzee Mkapa aliwahi kujaribu na alitolewa mbio na Dikteta huyo na alielezwa akawaambie wazungu waliomtuma kuwa hatowasikiliza!,Jk alijaribu kuwatuma Tanga Boys Rashid Othman na Adadi lakini nao waligonga Ukuta.Mama Tibaijuka alikwenda kwa Mwamvuli wake wa Habitat pia nae aliambulia patupu.Sasa kama hao wazoefu akina Mkapa wamekwama unafikiri Joseph Kabila (Mtoto wa Laurent),Ian Khama (Mtoto wa Seretse) au Bingu wataweza kumshinikiza Robert? Huyo Mbeki ndiye rafiki Mkubwa wa Robert,na sasa ndio amepewa jukumu la kuzungumza nao, nawaambia wazi kuwa hakuna lolote linaloendelea hapa.Tunawapa wakati mgumu MDC.Morgan Tsvangirai alikwishasema kuwa haoni kama kutakuwa na matokeo mazuri kwenye Mkutano wa Dar,alichoomba yeye ni kwamba Viongozi hao wamuengue Mugabe kutoka kwenye SADC kwa sababu ndio sehemu pekee iliyobaki anayotambuliwa!Ngoja tuone Drama nyingine !
Ngoja sisi (JK) tusawazishe ya Zimbabwe na ya kwetu na Zanzibar,Tumuombe Kuffour aje kutupatanisha!
 
ama kweli Mugabe mwendawazimu. magazeti ya MDC yanamkejeli Mkapa kama "mwanae" Mugabe, na kwamba amemteua mwenyewe kuwa msuluhishi wa huu mgogoro. sasa hivi zinakuja habari mpya kwamba Mugabe hamtambui Mkapa kama msuluhishi na alimshamfurumusha!

SADC inamtambua Mugabe kama Raisi aliyeshinda uchaguzi HURU na WAHAKI zimbabwe. MDC,UK,USA,bbc, hawatambui hilo. nashauri kila anayesoma habari na maoni ya pande mbili zinazokinzana, azingatie ukweli huo.
 
Leo nita waacha wengine nanitasema neno moja tu kwamba Hapa ndipo Mwalimu angali ifanay Africa iwe na heshima . Mwalimu angalikuwa jibu la huu mgogoro na Mugabe angalipewa vidonge kwa uwazi na si unafiki wa JK .watu wanaumia sisi waafrika tunawaona watawala wakoloni kama wamefanya jambo la maana . Mugabe need to to be told lakini hakuna katika genge la wapenda madaraka anaweza kumweleza.
Huko nyuma kidogo kwenye topic hii hii nilisema hivi:


http://jamboforums.jamboo.co.tz/showthread.php?t=2261&page=15
 
Mnakumbuka ziara aliyofanya Nyerere kwa Chiluba baada ya Chiluba kuanza kumnyanyasa Kaunda....!!?
 
Zanu-PF backs Mugabe election bid

Zimbabwe's ruling Zanu-PF party has endorsed President Robert Mugabe as its candidate for elections in 2008.

Mr Mugabe, 83, has been in power in Zimbabwe since independence in 1980.
There had been reports that one faction in the party had wanted Mr Mugabe to stand down to end a political and economic crisis in the country.
But Zanu-PF's central committee backed his decision to run for a new term in office, a party spokesman said at the meeting in Harare.


Hakuna cha SADC wala JK and company. Mugabe huyoooooo..............ataondoka kama alivyoingia kwa mtutu wa bunduki.
 
Hakuna cha SADC wala JK and company. Mugabe huyoooooo..............ataondoka kama alivyoingia kwa mtutu wa bunduki.[/QUOTE]

Dua !
Amekubali kufanya uchaguzi 2008?
 
Mzee Mugerezi,

Nimekusikia mkuu, ila Mbeki hawezi fanya kitu maana na yeye kwake ana ishu ya wananchi kudai ardhi, na sio siri katika diplomatic community kuwa Mugabe ni hero wa wananchi wengi wa Mbeki, ambao wamebandika picha Mugabe majumbani mwao, sana sana Mbeki haipendi hii ishu ya Mugabe maana hasimami kwenye clean ground,

Ni kweli sio wazugnu wote wanaofurahia ujinga wa wazungu wengine, lakini kwenye la Zimbabwe, wanahitaji kuja na solution ambayo itakuwa fair kwa waaa-Afika kwanza, yaani wazimbabwe na hao wazungu pia, lakini kwanza walenge wazawa kwanza,

Kuhusu the rule of law huko Zimbabwe, nafikir kwenye hilo kuna utata tena mkubwa sana, inafahamika kwamba serikali ikisha kaa sana madarakani, basi huanza kuchoka na kudharau sheria, tunasikia hata serikali ya Bush sasa hivi nayo imo matatni na sheria, na imekaa miaka 6 tu, sasa itakuwa miaka 28?

But, my point ni kwamba tusichanganye ishus katika hili suala la Zimbabwe, kuna ishu ya rais kukaa miaka mingi madarakani, kuna kutoheshimu the rule of law, na kuna waa-Zimbabwe na ardhi yao ambayo ndio muhimu zaidi ya ishu zote! Ninaamini la kutoheshimu the rule of law ni la kimataifa, na la ardhi ni la kimataifa, isipokuwa la kukaa madarakani muda mrefu ni la wa-Zimbabwe wenyewe!
 
Lipumba asema tatizo la Zimbabwe ni Mugabe

Na Mwandishi Wetu

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki, atafanikiwa kusuluhisha mgogoro wa kisiasa wa Zimbabwe iwapo tu rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe, atang'atuka madarakani ifikapo mwakani.

Amesema ana wasiwasi na azimio lililofikiwa na mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) uliofanyika jijini Dar es Salaam katikati ya wiki hii, kwa kuwa tatizo linaloikabili Zimbabwe ni kuendelea kuwapo madarakani kwa Rais Mugabe.

Lipumba aliyasema hayo alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana.

"Imefika wakati Rais Mugabe kung'atuka na kumwachia mwingine kuiongoza Zimbabwe ili tuweze kujenga demokrasia," alisema Lipumba na kukishauri chama tawala cha Zanu-PF, kuteua mwanachama mwingine kuwania urais mwakani badala ya Mugabe.

Lipumba alisema Rais Mugabe ana kila sababu za kung'atuka kwa kuwa ameiongoza Zimbabwe kwa kipindi kirefu na kwamba mchango alioutoa kwa nchi hiyo unatosha na badala yake amegeuka chanzo cha matatizo ya nchi hiyo.

"Tangu Mwalimu Nyerere awe madarakani kwa miaka 24, kaingia mzee Mwinyi akatoka, kaingia Mkapa akatoka na sasa mheshimiwa Kikwete, Rais Mugabe bado yuko madarakani. Pia Afrika Kusini, makaburu wametawala, kaingia Mandela na sasa Rais Thabo Mbeki, Mugabe bado yuko tu madarakani. Umefika wakati mzee huyu akang'atuka," alisema Lipumba.

Lipumba alisema suala la mashamba linaloonekana kuwa chanzo kikuu cha mgogoro wa kisiasa wa Zimbabwe, limetokana na kuchelewa kwa serikali kushughulikia suala hilo tangu mkataba wa Lancaster, utiwe saini baina ya Waingereza na wapigania uhuru wa nchi hiyo mwaka 1980.

Alisema hata mgawo wa mashamba hayo ulipofanywa na serikali, ulifanyika kwa upendeleo kwa kugawiwa wakubwa peke yake na kuwadhulumu wanyonge.

Badala yake, alisema wananchi wa hali ya chini wanaoishi mijini, wamekuwa wakifanyiwa dhuluma na ukandamizaji mbalimbali na serikali, ikiwa ni pamoja na kuvunjiwa makazi yao.

Alisema pia hali ya kiuchumi ya Zimbabwe, imekuwa mbaya na kutokana na hali hiyo, mfumko wa bei umekuwa ukiongezeka siku hadi siku kiasi kwamba, hivi sasa Dola moja ya Kimarekani, inanunuliwa kwa Dola 17,500 za Zimbabwe.

Kutokana na matatizo hayo, alisema hivi sasa zaidi ya Wazimbabwe 3000,000 wameikimbia nchi hiyo na kwenda kuishi katika nchi mbalimbali duniani, ikiwamo Afrika Kusini.

Alisema pia kitendo cha hivi karibuni cha kupigwa kwa kiongozi wa chama cha MDC cha Zimbabwe, Morgan Tsivangirai, kimezidi kuiongezea aibu serikali ya Rais Mugabe katika uso wa dunia.

Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo Rais Mugabe hatang'atuka madarakani mwakani, heshima ya SADC na Mugabe mwenyewe, itapungua.

Alisema mbali na heshima kupungua, pia mkutano wa wakuu wa jumuiya hiyo wa Dar es Salaam, utapoteza maana na fedha za walipa kodi wa nchi wanachama, zitakuwa zimetumiwa vibaya kufanikisha mkutano huo.

Aliitaka SADC kuhakikisha nchi wanachama wake, zinakuwa na uchaguzi ulio huru na wa haki na kuhakikisha Wazimbabwe wanachagua viongozi wanaowataka na kuitaka pia serikali ya Rais Mugabe kutotumia nchi za Ulaya kama kisingizio cha kutokutekeleza matakwa ya demokrasia nchini humo.


mwanakjj
nnaomba utupashe nini kilitokea ktk ziara ya JKN wakati chiluba.
 
Back
Top Bottom