Kaka, ubaya wa Mugabe sasa hivi huko Zimbabwe hauhitaji kuhubiriwa na US au UK. Kila mzimbabwe anaujua isipokuwa aliye waziri wa serikali ya Mugabe na familia na ndugu zake wa karibu sana. Hebu jaribuni kuongea basi na hata wa Zimbabwe; piga simu kwa mtu yeyote ZImbabwe. Uzuri kupiga simu Zimbabwe ni very cheap.
Jamani, tutaacha lini kuwalaumu wazungu kwa matatizo yetu? Halafu hawa wazungu kwa nini wanakuwa wabaya tu pale wanapotukosoa lakini hatuachi kutega mikono yetu kwao? Haya mashamba aliyoyachukua Mugabe aliyapeleka wapi? Kwa nini uzalishaji ulishuka? Kwani hawa US na UK walienda huko wakawataza wananchi wasilime? Hawa US na UK ndio wamepeleka njaa Zimbabwe? Hivi, ni hawa US na UK wanaomwambia Mugabe awape waduasi wake tu mahindi na awanyime wale ambao wanampinga? Hivi ni US na UK waliowaambia wananchi wamchukie Mugabe? And, kwa nini ni Mugabe, ina maana hakuna mtu mwingine anayekubaliana na sera za chama chake na anayeweza kuzisimia zaidi yake? Kwa nini mtu mmoja aruhusiwe kuiharibu nchi nzima kwa kiasi kile kisa aliwanyang'anya wazungu mashamba? I mean, kwa nini hata sisi ambao tunafikiri ni kizazi kipya katika bara letu tunashindwa kukubali kuwajibika kwa kushindwa kwetu kutekeleza wajibu wetu?
Kitila,
Kweli kabisa, matatizo ya Afrika ni yetu sisi wenyewe.
I hope Wazimbabwe watamtema huyu Mugabe na kuanza upya kutengeneza maisha yao. Ila baada ya yale yaliyotokea Kenya, itabidi kusubiri mpaka Mugabe anakubali kushindwa maana unaweza kunywa wine, unalala, kuamka unakuta Mugabe anashangilia.